Skip to main content

NI UZINDUZI WA MAVAZI MAPYA TINGATINGA FASHION

Kwa mara ya kwanza katika historia ya sanaa nchini Tanzania, mjasiriamali na mbunifu wa mavazi na mwanaharakati kwenye sekta ya utamaduni, Bi. Sophia Urio, kwa kuzingatia ushauri wa wataalam ambao nao pia ni wajasiriamali, amefanya ubunifu wa kipekee na kuanzisha mtindo mpya wa mavazi, unaotambulika kwa jina la “Tinga Tinga Fashions”.
“Nilipewa ushauri wa kufanya kitu kipya, wazo jipya, kwa kuzingatia kwamba wabunifu wengi wa mavazi hapa nchini wanarudia mambo yale yale ya zamani, na wengi wanaiga mitindo ya nje ya nchi. Sanaa ya Tinga Tinga iliasiliwa hapa nchini, ni fahari yetu.
Tunapofanya ubunifu tuzingatie kwanza hazina iliyopo nchini, kabla ya kutoka nje ya nchi. Mbona wabunifu wa nje wanazingatia urithi wao, iweje sisi tuwe waigizaji kila siku?” alisema Bi. Sophia.
Bi. Sophia amesema, alichokifanya ni kuunganisha sanaa ya michoro ya Tinga Tinga, iliyoanzishwa na mchoraji mahiri, marehemu Mzee Saidi Tinga Tinga, na sanaa ya ubunifu wa mavazi, kwa kuzingatia mila na tamaduni za Kitanzania.
“Nimeunganisha sanaa ya uchoraji, kupitia mtindo wa Tinga Tinga, na sanaa ya ubunifu wa mavazi, kwa kuzingatia mitindo ya Kitanzania na Kiafrika, hivyo nikapata kitu kinachoitwa Tinga Tinga Fashions. Hii ndiyo asili ya mtindo huu mpya kabisa, ambao ni muunganisho wa aina mbili sanaa zenye historia moja,” aliongeza Bi. Sophia.
Akizingatia hazina kubwa ya utamaduni iliyoasisiwa na marehemu Mzee Saidi Tinga Tinga, pamoja na wanafunzi wake walioendeleza fani hiyo, Bi. Sophia amesema amewaalika warithi wa marehemu Saidi Tinga Tinga pamoja na wachoraji wanaoendeleza fani hiyo kushiriki kwenye uzinduzi huo, ambao utafanyika kwenye ukumbi wa Kituo cha Utamaduni cha Makumbusho (Makumbusho Culture Centre), kilichopo Makumbusho, Kijitonyama, Dar es Salaam, kuanzia saa 12 jioni, Jumamosi, Agosti 7, 2010.
Amesema ameamua kuwaalika wadau wa sanaa ya Tinga Tinga ili kuwaenzi kutokana na mchango wao mkubwa kwenye sanaa Tanzania, pia kuchangia uhamasishaji wa kazi yao ya kisanii yenye kiwango bora ili ithaminiwe na kufahamika zaidi miongoni mwa Watanzania. Wasanii wa Tinga Tinga wataonesha kazi zao kwenye ukumbi huo wakati wa uzinduzi ili kuitangaza zaidi sanaa hiyo kwa kuwapatia elimu watazamaji.
Uzinduzi utapambwa na onesho la mavazi, ambapo mavazi tano ambayo yatabuniwa kwa madhumuni ya uzinduzi huo. Mavazi yataoneshwa kwenye jukwaa la Makumbusho Culture Centre, yakinadiwa na warembo mahiri ambao wameteuliwa kuonesha mavazi hayo. Bi. Sophia Urio, mbunifu wa mavazi hayo, amesema kwamba yataonesha hali halisi ya utamaduni wa mavazi wa Mtanzania, hususan, vazi linalostahili kuvaliwa na mwanamke anayezingatia mila na tamaduni za nchi yake.
Kwa upande wa burudani, onesho hilo litapambwa na wanamuziki wa bendi ya FM Academia (Wazee wa Ngwasuma), ambao watawaburudisha watazamaji ipasavyo. Pia, Bi. Sophia atasindikizwa na mbunifu chipukizi, Kemmy, kutoka kampuni ya “Binti Afrika”, ambaye naye ataonesha baadhi ya mavazi aliyoyabuni, akiwa na warembo watakaopanda jukwaani kuonesha mavazi hayo. Kiingilio kwa ajili ya uzinduzi huo pamoja na burudani zote zitakazokuwapo ni Shilingi za Kitanzania

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them ...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Mwana muziki Marufu kwa jina la Chuck Brown Afariki Dunia Akiwa na umri wa miaka 75

View Photo Gallery — Chuck Brown dies at 75: The “godfather of go-go” has died By Chris Richards, Updated: Wednesday, May 16, 4:42 PM Chuck Brown, the gravelly voiced bandleader who capitalized on funk’s percussive pulse to create go-go, the genre of music that has soundtracked life in black Washington for more than three decades, died May 16 at the Johns Hopkins University hospital in Baltimore. He was 75. The death, from complications from sepsis, was confirmed by his manager, Tom Goldfogle. Mr. Brown had been hospitalized for pneumonia. Known as the “Godfather of Go-Go,” the performer, singer, guitarist and songwriter developed his commanding brand of funk in the mid-1970s to compete with the dominance of disco. Like a DJ blending records, Mr. Brown used nonstop percussion to stitch songs together and keep the crowd on the dance floor, resulting in marathon performances that went deep into the night. Mr. Brown said the style got its name because “the music j...