Skip to main content

NMB Kuwapa Gawio Wanahisa

WANAHISA wa Benki ya NMB watapata gawio la jumla ya Shilingi 15.7 bilioni kwa mwaka 2009,

ikiwa ni ongezeko la asilimia 4.7 ikilinganishwa na mwaka uliotangulia.

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya NMB, Misheck Ngatunga, amesema mgawo wa kila hisa kwa

mwaka utakuwa Shilingi 31.40, ikilinganishwa na Shilingi 30 kwa mwaka 2008.

Alikuwa anawasilisha ripoti ya mwaka 2009 kwenye mkutano mkuu wa mwaka wa NMB uliofanyika

jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.

Ngatunga alisema mwaka 2009 ulikuwa wa changamoto nyingi kutokana na kuongezeza kwa

ushindani katika sekta za benki pamoja na mtikisiko wa uchumi duniani, ambao ulikuwa na

madhara makubwa katika uchumi wa Tanzania kama kwingineko duniani.

Aliisifu serikali kwa kuandaa mkakati wa kukabiliana na mtikisiko wa uchumi kwa kuendeleza

mfuko wa kuokoa na kusaidia sekta na taasisi zilizoathirika na mtikisiko huo.


“Sekta ya fedha ya Tanzania kwa ujumla haikuathirika na mtikisiko huo, na iliendelea kuwa na

mtaji wa kutosha na yenye faida. Ingawa athari hizo zilikuwa tofauti kwa kila benki.”Hata

hivyo, alisema hali ya uchumi na kushuka kwa viwango vya riba vilichangia kushuka kidogo kwa

mapato na faida mwaka 2009, ambapo benki hiyo ilipata faida ya Shilingi 68.04 bilioni (kabla

ya kodi), ikilinganishwa na Shilingi 70.94 bilioni mwaka uliotangulia.


Upungufu huo wa faida ni kwa asilimia nne.Wakati huo huo, NMB imedhamiria kuboresha huduma

zake na kupunguza msongamo wa wateja katika matawi yake nchini na kuwafikia Watanzania wengi

zaidi wanaoshi vijijini.

Katika taarifa yake ya mwaka 2009, benki hiyo yenye mtandao mkubwa nchini imesisitiza kuwa

itazingatia zaidi kupunguza muda wa wateja kusubiri katika matawi na ATM, pamoja na

kuboresha mikopo.

Mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi alisema pamoja na mafanikio mengi yaliyopatikana katika

kipindi kipindi cha mwaka uliopita, ikiwa ni pamoja na kuongezeka kwa matawi na mtandao wa

ATM kutoka 167 mwaka 2008 hadi 281 mwishoni mwa mwaka 2009, bado wanakabiliwa na changa moto

nyingi, ikiwemo tatizo la msongamano wa wateja.

“Nina uhakika kwamba uongozi na wafanyakazi wa NMB watafanikiwa kukabiliana na changamoto

hizo,” alisema Ngatunga.Alisema NMB inakusudia kupanua zaidi mtandao wa matawi nchini ili

kuweza kujikita zaidi katika msukumo wa ‘Kilimo Kwanza’, mpango wa kuboresha uzalishaji wa

kilimo na sekta ya mabadiliko kwa nia ya mapinduzi ya kilimo.

Akizungumza katika mkutano huo, Mtendaji Mkuu wa NMB, Bern Christiaanse, alisema mtandao wa

matawi ya NMB uliongezeka kufikia 133 mwaka 2009, huku matawi mapya nane yakifunguliwa mwaka

huo.

Alisema ongezeko hilo ni matokeo ya mkakati wa benki hiyo wa kutoa huduma za kifedha kwa

watanzania wengi iwezekanavyo.Kwa mujibu wa taarifa ya mwaka 2009, jumla ya raslimali za

benki hiyo zilikua kwa asilimia 20.6 kutoka Shilingi 1,384.3 bilioni hadi 1,669.3 bilioni,

wakati ambapo mtaji wa benki ulikua kwa asilimia 20.4 kutoka Shilingi 159,689 milioni hadi

Shilingi 192,239 milioni.

Taarifa hiyo iliyowasilishwa kwenye mkutano mkuu wa mwaka wa NMB ni ya pili tangu benki hiyo

iwe kampuni ya umma baada ya kuorodheshwa kwenye soka la hisa la Dar es Salaam.

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...