Skip to main content

Kweli Hakielimu!! ...


Kutokana na taarifa zilizotolewa na gazeti la HabariLeo la tarehe 19 Juni ukurasa wa 4, na kurudiwa kwenye tahariri ya gazeti hilo la tarehe 20 Juni ukurasa wa 6, HakiElimu inapenda kutoa ufafanuzi kwa umma kuhusu maana, malengo na ukweli wa takwimu za ujenzi wa nyumba za walimu zilizotumika kwenye tangazo letu kwa wananchi.

Tangazo ujumbe wa maneno yafuatayo:-

..“.Mwaka 2008, Serikali ilipanga kujenga takriban nyumba za walimu 22,000, lakini zilizojengwa ni kama nyumba 300; yaani asilimia moja tu. Kutokana na upungufu wa nyumba za walimu, walimu wachache waliopo shuleni wanalazimika kufundisha kwa muda mrefu na hata kufundisha masomo wasiyoyasomea. Hali hii inadumaza elimu. Kuna upungufu mkubwa wa nyumba za walimu. Japo hazitoshi, ni muhimu sasa Serikali itekeleze ahadi ya kujenga nyumba 22,000 za walimu, kama mpango wa MMEM unavyosema, kwa mwaka 2010/ 2011”.

Tunapenda wananchi wafahamu ukweli ufuatao:-

1. Chanzo cha takwimu zilizotumiwa kwenye tangazo hilo ni Ripoti ya Serikali ya Utekelezaji wa MMEM II kwa mwaka 2007/2008 yenye jina la “Primary Education Development Programme II (2007-2011): Annual Performance Report FY- 2007/2008) iliyotolewa na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi na TAMISEMI mwezi Agosti, 2008. Katika ukurasa wa 11, kipengele 2.1.2 kinachohusu “Miundombinu ya shule” (School infrastructure), aya ya kwanza. Serikali inatamka wazi kuhusu idadi ya nyumba ilizojenga kulinganisha na malengo yake. Tunanukuu:

“…The target for 2007/8 under this component was to construct 5, 732 pre-primary classrooms, 10,753 primary classrooms and 21,936 teachers’ houses in rural and remote areas. Providing teachers with houses is a positive incentive and motivation for retaining them in their working areas. In the year under review a total of 1, 263 classrooms, 277 teachers’ houses...were constructed..”

Ikimaanisha kwamba (kwa tafsiri yetu):

“…shabaha ya serikali kwa mwaka 2007/2008 ilikuwa ni kujenga madarasa 5,732 ya elimu ya awali. Madarasa 10,753 kwa shule za msingi na nyumba za walimu 21,936 katika maeneo ya vijijini na yaliyo pembezoni zaidi. Kuwapatia nyumba za walimu ni kichocheo chanya na motisha muhimu ya kuwabakiza walimu katika maeneo yao. Kwa mwaka wa mapitio (2007/8), jumla ya madarasa 1, 263 na nyumba za walimu 277 zilijengwa….”

2. HakiElimu katika tangazo lake haikuongelea ujenzi wa nyumba za walimu kwa kipindi cha uongozi wa serikali ya awamu ya nne, isipokuwa imezungumzia utekelezaji wa MEMM II (2007-2011), tena kwa kipindi cha mwaka 2008 tu.

3. Katika tangazo hilo, HakiElimu haijasema kwamba kuna uhaba wa nyumba 22,000 kama mwandishi wa gazeti hilo alivyobainisha. Bali imesema, Serikali ilipanga kujenga idadi ya nyumba hizo, kama nyaraka zake, MMEM II na ripoti ya Serikali ya utekelezaji wake kwa mwaka 2007/2008 (Primary Education Development Programme II (2007-2011): Annual Performance Report FY- 2007/2008) zinavyobainisha.

4. Vilevile, tangazo la HakiElimu halijasema Serikali ya awamu ya nne kwa kipindi chote cha utawala wake imemudu kujenga idadi ya nyumba za walimu zipatazo 300 tu, bali imesema serikali imejenga kiasi hiki cha nyumba za walimu kwa kipindi cha mwaka 2008 tu. Ripoti tajwa inathibitisha hilo.

5. HakiElimu siku zote inazingatia ukweli na ushahidi wa kitakwimu kutoka kwenye nyaraka za Serikali yenyewe, tafiti zake na za wadau mbalimbali. Pia kwa kutembelea na kuona hali halisi kabla ya kutoa ujumbe wowote.

6. Lengo la tangazo la HakiElimu ni kuonesha madhara yanayotokana na upungufu wa nyumba za walimu; ambayo ni pamoja na kuchangia walimu kadhaa kuacha kazi na kusita kwenda kufundisha hasa maeneo ya vijijini na yale ya pembezoni. Hii ni kutokana na kutokuwa na uhakika wa mahali pa kuishi. Ripoti ya serikali pia imebainisha hili. Katika tangazo hili, HakiElimu inaiomba Serikali kutenga pesa kwenye bajeti ya 2010/11 kwa ajili ya kujenga nyumba nyingine 22,000 za walimu kama ilivyopangwa kwenye MMEM II (kwa mwaka wa fedha 2010/11).

7. HakiElimu inatambua mchango wa mashirika mbalimbali katika ujenzi wa nyumba za walimu nchini na elimu kwa ujumla, lakini inaamini kuwa mchango huo hauzuii mipango na bajeti iliyotengwa na serikali kutekelezwa.

8. Dhima ya asasi za kiraia kamwe sio kupongeza serikali wala kulumbana nayo; na wala sio kupotosha umma. Ni kukuza na kupanua wigo wa demokrasia na ushiriki wa wananchi katika kuleta maendeleo. Wananchi siku zote wanafahamu na wanapaswa kuendelea kufahamu kwamba; moja ya kazi muhimu za asasi za kiraia ni kufuatilia utendaji wa serikali katika masuala yote yanayohusu maendeleo na ustawi wa wananchi.

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...