Skip to main content

HOFU ILIYOTANDA KWAMBA NDOTO ZA SAMATTA KUCHEZA ULAYA SOMA UFAFANUZI HUU




Samatta-Nape 4
Kuna taarifa za wasiwasi kwamba huenda Mbwana Samatta asijiunge na klabu Genk ya Ubelgiji kwasababu bado ana mkataba na klabu ya TP Mazembe na bosi wa klabu hiyo Moise Katumbi hayuko tayari kuona nyota huyo kipenzi cha wana-Lubumbashi anaondoka kunako klabu ya Mazembe.
Mtandao huu ukabisha hodi kwa manager wa Mbwana Samatta Mr. Jamal Kisongo ambaye yeye ndiye anayesimamia kila kitu kuhusu masuala ya usajilki na mikataba ya mchezaji huyo.
Kisongo amefafanua kila kitu kuhusu mkataba wa Samatta uliobaki kuendelea kuitumikia TP Mazembe pamoja na taratibu zilizofikiwa ili kuhakikisha Samatta anakwenda kucheza soka la kulipwa barani Ulaya. Hii hapa story nzima ya Kisongi akifunguka juu ya mustakabali mzima wa Samatta kuhusu kutimkia Ulaya kwenye klabu ya Genk.
Suala la Mbwana kucheza soka Ulaya limefikia tamati kwasababu kitu kikubwa zadi tayari ameshasaini mkataba na klabu ya Genk mkataba wa miaka miwili lakini akiwa na nafasi akitaka kuongeza miaka miwili mingine anaweza kufanya hivyo. Kwahiyo watanzania wawe na amani kwasababu Mbwana ni mchezaji halali wa Genk.
Sasa hii sintofahamu nyingine ya utaratibu wa uhamisho ndiyo unaleta shida, lakini Mbwana amebakiza mkataba wa miezi minne na kwa mujibu wa kanuni za FIFA mchezaji anapobakiza mkataba wa miezi sita na chini ya hapo ana haki ya kujadili mkataba mpya na klabu yoyote au kutaka kujua hatma yake ili mkataba wake unapokwisha asibaki bila timu kwasababu FIFA inataka wakati wote mchezaji awe na timu.
Ukizingatia mwezi April ukimalizika hakuna dirisha la usajili, usajili upo mwezi January na mwezi July, tafsiri yake ni kwamba tulichokifanya kwa Mbwana ni kuhakikisha mwezi Janury anaitumikia Genk lakini ukisema asubiri hadi mwezi wa saba maana yake kunakipindi atabaki akiwa mchezaji ambaye hana timu kwasababu mkataba wake na Mazembe unamalizika mwezi April.
Kwahiyo Mbwana kubaki bila timu kutatoa nafasi ya kumshawishi aendelee kubaki TP Mazembe lakini watanzania wengi wanataka kumuona Samatta akiingia kucheza Ulaya kwasababu ana kila aina ya sifa zaidi ya wachezaji wengi wa Afrika Magharibi, Kaskazini na Kusini mwa Afrika.
Huu utata uliopo unatokana na madai ya kipesa (ada ya uhamisho) TP Mazembe wao wanataka walipwe Euro milioni 2.5 ambayo pesa hii ukizingatia miezi minne au mitatu itakayobaki baada ya mwezi Janury ni pesa nyingi mno ukilinganisha na mkataba halisi wa Mbwana uliobaki. Kwahiyo Genk wakasema hapana, TP Mazembe wakatoa nafasi kwa Genk waseme wao wako tayari kutoa kiasi gani cha pesa.
Genk wakatoa offer ya Euro 350,000 ambayo Moise Katumbi akaona ni pesa ndogo mno akarudisha na kuwaambia waongeze offer, Genk wakapeleka offer nyingine ya Euro 550,000 ambayo pia ilikataliwa na Katumbi ambaye alisema anataka Euro 750,000.
Mimi nikalazimika kwenda Lubumbashi kuzungumza na Katumbi ili amwachie Mbwana, kwasababu wakati Mbwana anasaini mkataba na TP Mazembe kuna vitu ambavyo tuliafikiana. Mimi kama manager wake kwa faida ya mtoto (wakati huo Mbwana alikuwa bado mtoto) tulikubaliana ndani ya miaka miwili au mitatu Mbwana aondoke.
Lakini imefikia kipindi offer nyingi zilizokuwa zinaletwa kwake yeye alikuwa nazitia kapuni, kwahiyo tulizungumza na yeye akatoa masharti kwamba Mbwana aongeze mkataba wake kwa miaka mitatu ambao utamruhusu kuondoka kitu ambacho kwangu kilikuwa ni kigumu.
Tulimwita mwanasheria wetu tukakaa na Frederic Kitengie tukakaa vikao kwa siku mbili lakini havikuzaa matunda kwasababu wao walikuwa wanalazimisha Mbwana asaini mkataba kwao kwa madai ya kumpa thamani.
Sisi pia tukatoa masharti yetu. Mwanasheria wetu akasema, Mbwana anaweza kusaini mkataba ikiwa kutakuwa na kifungu kinachosema ni lazima auzwe mwezi January na siyo kutolewa kwa mkopo kwasababu Katumbi huwa hauzi wachezaji kwenda Ulaya badala yake huwa anawatoa kwa mkopo. Na wao pia wakakataa sharti hilo.
Genk nao wakachua hatua, wameamua kulipeleka suala hili FIFA. Baada ya kutua FIFA, Katumbi alipigiwa simu na watu wa Genk hakupokea lakini baaye aliwapigia simu wakaweza kujadili lakini suala hili bado limekwama. Kwahiyo cha msingi tunataka kuwaambia watanzania wawe na amani Mbwana ni mchezaji halali wa Genk.
Suala lililopo na tunachoshindana ni kwamba Mbwana aondoke January au majira ya joto, sisi tunachotaka aondoke majira haya ya baridi (mwezi Janury).Inatoka http://shaffihdauda.co.tz

Comments