Skip to main content

Business Travel laitunuku ETIHAD Tuzo ya Shirika la Ndege la mwaka


Meneja wa Chakula na Vinywaji wa Shirika la Ndege la Etihad.
Etihad Business Studio
Etihad Business Studio.
Shirika la ndege la Etihad limetajwa kuwa Shirika la Ndege la Mwaka wakati wa tuzo za Business Travel 2016. Hafla hii ilifanyika jana usiku katika hoteli ya Grosvenor House iliyopo Jijini London. Tuzo hizi zinatambua makampuni na watu binafsi waliopata mafanikio katika sekta ya biashara ya usafiri na hivyo kuwafanya wastahili kuwania tuzo hizo.
Tuzo hizi zinazoandaliwa na jarida la Uingereza la Buying Business Travel, huwa na jopo la wataalamu wanaojadiliana na kisha kupiga kura kubaini washindi. Hii ni mara ya kwanza kwa Etihad kushinda tuzo hiyo, hii ikija siku chache tu baada ya shirika la ndege la Etihad kupokea “Tuzo ya Uvumbuzi katika Usafiri” kutoka tuzo za jarida la Globe Travel katika hafla nyingine iliyofanyika wiki iliyopita London.
James Harrison, Meneja Mkuu wa shirika la Etihad Uingereza, alisema: “Tuzo hii ni ishara ya kutambulika kwa mchango wa Etihad katika sekta ya usafiri wa anga nchini Uingereza. Tunajisikia fahari kubwa sana kutambuliwa katika jukwaa kubwa hivi.”
“Uingereza ni soko muhimu kwa shirika hili na mwaka huu umekuwa na mafanikio makubwa kwetu kwani tunasherekea miaka kumi tangu tuanze kutoa huduma zetu kati ya jiji la Manchester na Abu Dhabi. Tunategemea kuzindua huduma ya tatu ya kila siku kutoka uwanja wa ndege Heathrow, jijini London, kupitia ndege aina ya A380 ambayo pia ina huduma ya vyumba ya “Makazi”. Zaidi tunalenga kutoa huduma iliyorahisishwa na inayowaunganisha wageni wetu.”
Shirika la Etihad liliibuka kidedea kutokana na huduma zao za hali ya juu, zikiwemo bidhaa (na vyumba) zilizoingia hivi karibuni sokoni na kuleta mapinduzi katika sekta ya usafiri wa anga. Hii ikiwa pamoja na kutumia ndege aina ya Airbus A380 na Boeing 787 Dreamliners, bila kusahau vyumba ambavyo vilishakuwa vikitumika na Airbus A330/A340 na Boeing 777.
Mapinduzi haya yametokana na programu ya utafiti na maendeleo iliyoendeshwa katika Kituo cha Uvumbuzi kilichopo Abu Dhabi na kuongozwa na timu ya ubunifu ya Etihad. Shirika la Etihad linapenda kutoa huduma yenye viwango sawa na hoteli kubwa na sehemu nyingine za kitalii kubwa duniani. Etihad wameajiri wafanyakazi wenye ufundi na uzoefu mkubwa haswa katika safari ndefu kwa mfano wahudumu wakuu walipo katika “Makazi” ya ndege ya A380 kwenda London, Wapishi Wa daraja la Kwanza, meneja wa vyakula na Vinywaji katika “daraja la biashara” na wahudumu wa kutunza watoto wakati wa safari. Wahudumu hawa wamehitimu chuo cha kulea na kutunza watoto Norland huko Uingereza.
Pia shirika la ndege la Etihad lina sehemu ya mapumziko katika viwanja vya ndege wa London Heathrow, Manchester, Frankfurt, Dublin, Paris, Sydney, Washington, D.C. na New York wakati uwanja wa ndege wa Abu Dhabi una sehemu za mapumziko na mapokezi.
Hivi sasa safari za shirika hili zinafika sita kila siku kwenda Uingereza, zikiwa na huduma za moja kwa moja kufika jijini London kupitia uwanja wa ndege wa Heathrow, jijini Manchester na jijini Edinburgh zilizozinduliwa Juni 8 mwaka jana. Uwanja wa ndege wa Heathrow Jijini London ulipata nafasi ya kuwa kituo cha kwanza kwa ajili ya kuzindua huduma ya ndege za jamii aina ya Airbus A380, ikiwemo huduma ya “Makazi”- ikiwa na vyumba vya kipekee duniani kuwekwa kwenye ndege ya kibiashara yenye ukubwa wa vyumba vitatu huku ndege hii pia ikiwa na vyumba 6 vya “daraja la kwanza”, 70 vya “daraja la biashara” na 415 vya “daraja la uchumi”.

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.