Mkuu wa mkoa huyo amewataka watu mbalimbali katika maeneo ya jiji la Dar es salaam kujitokeza ili kushirikiana kwa pamoja na mh Rais Jakaya Mrisho Kikwete ambaye atakuwa mgeni rasmi katika tamasha hilo.
Wasanii mbalimbali ambao wamechaguliwa kuwas mabalozi wa kampeni hiyo wataimba siku hiyo na kushirikisha wasanii wengine pia kwa pamoja ili kutoa ujumbe wenye kuhamasisha jamii kutumia vyandarua ili kujikinga na ugonjwa wa Maralia, na bbaada ya kumaliza Dar wasanii hao wataendelea na kampeni hiyo kwa nchi nzima katika kuhamasisha mapambano dhidi ya Maralia
Kampeni hiyo inaratibiwa na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii ikishirikiana na taasisi ya Malaria No More ya nchini Marekani ili kuhakikisha ugonjwa huo unapungua kwa kiasi kikubwa .
Comments