Skip to main content

SAKATA LA JERRY MURO BADO LATIKISA

Kamanda Kova akiwatambulisha watuhumiwa  Emanuel Kapamo na Deogratius Ngassa kwa waandishi wa habari siku chache sasa , leo sakata hilo katika maswali ya Papo kwa hapo Mbunge na kiongozi wa kambi ya Upinzani aliingiza
Hamad Rashid Hamad aliuliza swali kuwa nikwanini waandishi wa si Tanzania pekee bali hata dunia nzima wanaoibua tuhuma mbalimbali hupatwa na misukosuko.

Hamad amesema huwa haoni sababu ya kuibuka kwa malumbano chini kutokana  na kitendo chamwandishi huyo kukamatwa.

Waziri pinda amesema kuwa mwandishi  ni binadamu wa kawaida  na mwenye mapungufu kama walivyo watu wengine na hakuna binadamu aliyekamili .

Pinda amesema kuwa amepata taarifa kuhusiana na kukamatwa  kwa mwandishi huyo na tayari uchunguzi wa kina unafanywa  ilikubaini ukweli wa tatizo hilo. Waziri amesema hapendi suala hilo liendelee kwa kipindi kirefu kwani linaweza kureta kasorombali mbali  hivyo  amewasiliana na  Mkuu wa Jeshi la Poloisi nchini ilikupata ukweli wa tukio.

Comments