Skip to main content

Matokeo CCM yazidi kuwa mwimba kwa Wabunge



Matokeo ya kura za maoni kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi kwa wagombea wa nafasi za udiwani na ubunge yameendelea kuwa mwiba mkali kwa waliokuwa wakitetea nafasi hizo.
Mbunge wa Kilombero Abdu Mteketa
Wilayani kilombero aliyekua mbunge wa jimbo hilo Abdul Mteketa amelazimika kuyakimbia matokeo baada ya kubaini ameangushwa katika kutetea nafasi hiyo.
Hali hiyo imejitokeza wakati wa kutangazwa kwa matokeo ya uchaguzi ndani ya CCM, wa kuwatafuta wawakilishi wa ubunge na udiwani watakaopeperusha bendera ya CCM, katika uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu,
Mbunge wa Kilombero Abdu Mteketa alilazimika kususia zoezi hilo baada ya kubaini nafasi aliyokuwa akiwania kuitetea, kuchukuliwa na kijana mdogo, Abubakar Asenga aliyetumia nafasi hiyo kuwaomba wana ccm kuvunja makundi yaliyojitokeza wakati wa kura za maoni na kuwa wamoja ili kufanikisha ushindi na maendeleo ya chama hicho na taifa kwa ujumla
Abubakar Asenga ameshinda kura hizo za maoni za kuwania ubunge kilombero kwa kupata kura 9629,dhidi ya mpinzani wake wa karibu Abdalah Lyana aliyepata kura 3999 huku mteketa aliyekuwa akiwania nafasi hiyo akishika nafasi ya tatu kwa kuambulia kura 2646 na alipotafutwa kwa simu yake ya mkononi iliita bila majibu,
Katibu wa CCM, wilaya ya kilombero Bakari Mfaume pamoja na kushukuru zoezi hilo kumalizika salama,amesema ofisi yake ipo tayari kupokea malalamiko ya wanaodhani wameonewa katika uchaguzi huo ili wafanyie kazi.
Katika maeneo mengine ya uchaguzi ndani ya ccm mkoani Morogoro,baadhi ya waliokuwa wabunge wamefañikiwa kutetea nafasi zao kwa kushinda kura za maoni,akiwemo aliyewahi kuwa Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dkt. Haji Mponda aliyeshinda jimbo la ulanga magharibi,Waziri wa nchi ofisi ya Raisi Menejimenti ya Utumishi wa umma,Celina Kombani akishinda ulanga mashariki,Ahmed Shabiby akishinda jimbo la Gairo na Abdulaziz Abood akishinda Morogoro mjini,huku jimbo wazi la kilosa ambalo awali lilishikiliwa na Mustafa Mkulo ambaye hakugombea tena akishinda Mbaraka Bawaziri.
Walioangushwa ni pamoja na naibu waziri wa maji na mbunge wa mvomero amos makala na nafasi hiyo kuchukuliwa na aliyewahi kuwa mbunge wa jimbo hilo suleiman Sadiq Murrad,aliyewàhi kuwa Naibu Waziri wa afya Dkt. Lucy Nkya akianguka jimbo la Morogoro kusini Mashariki na nafasi yake kuchukuliwa na Mgumba,
Mwenyekiti wa CCM, mkoa wa Morogoro Innocent Kalogores akiangushwa jimbo la Morogoro kusini na nafasi yake kuchukuliwa na Mbena na aliyekuwa mbunge wa mikumi Abdusalam Ameir akiangushwa jimbo la Mikumi na nafasi hiyo kuchukuliwa na Jonas Estomih nkya.Chanzo http://www.eatv.tv/news

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them ...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Mwana muziki Marufu kwa jina la Chuck Brown Afariki Dunia Akiwa na umri wa miaka 75

View Photo Gallery — Chuck Brown dies at 75: The “godfather of go-go” has died By Chris Richards, Updated: Wednesday, May 16, 4:42 PM Chuck Brown, the gravelly voiced bandleader who capitalized on funk’s percussive pulse to create go-go, the genre of music that has soundtracked life in black Washington for more than three decades, died May 16 at the Johns Hopkins University hospital in Baltimore. He was 75. The death, from complications from sepsis, was confirmed by his manager, Tom Goldfogle. Mr. Brown had been hospitalized for pneumonia. Known as the “Godfather of Go-Go,” the performer, singer, guitarist and songwriter developed his commanding brand of funk in the mid-1970s to compete with the dominance of disco. Like a DJ blending records, Mr. Brown used nonstop percussion to stitch songs together and keep the crowd on the dance floor, resulting in marathon performances that went deep into the night. Mr. Brown said the style got its name because “the music j...