Skip to main content

Magufuli: Nikishinda sina deni la fadhila


Mgombea urais wa CCM Dkt. John Magufuli
Mgombea urais wa CCM Dkt. John Magufuli
Mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. John Magufuli, amesema hana deni la kulipa kwa mtu yeyote akichaguliwa kushika wadhifa huo kwa kuwa hakutoa rushwa wakati wa uteuzi ndani ya chama hicho.
Magufuli alitoa kauli hiyo jana wakati akijinadi yeye na wagombea udiwani na ubunge wa CCM mkoani hapa ili wachaguliwe katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 25, mwaka huu.
Dk. Magufuli alikuwa akijinadi na wagombea hao kwa nyakati tofauti katika mji wa Mbalizi na wilayani Songwe eneo la Mkwajuni, Makongolosi wilaya ya Chunya.
Magufuli ambaye jana alikuwa katika  siku ya nne ya kujinadi kwa wananchi na kuomba kura tangu kufunguliwa kwa pazia la kampeni mikoani, alisema tangu kuanza kwa mchakato wa kumpata mgombea wa CCM wa urais ndani ya chama hicho, hakutumia fedha bali alikwenda kimya kimya makao yao makuu kuchukua fomu na kuzirejesha.
Alisema kwa mantiki hiyo,  hana cha kulipa kwa sababu hadaiwi na mtu yeyote.
Magufuli alisisitiza kuwa anachofahamu ni kwamba deni kubwa alilonalo ni kuwatumikia Watazania na kuwaletea maendeleo ili wazidi kuwa na maisha bora.
“Nilichukua fomu kimya kimya na kurudisha kimya kimya, natembea na barabara ili shida zenu ziwe shida zangu, ili nikiingia Ikulu nizishughulikie kwa haraka,” alisema.
Magufuli alisema anaamini kuwa kuteuliwa kwake na CCM kupeperusha bendera ya chama hicho katika kinyang’anyiro hicho kuna makusudi ya Mwenyezi  Mungu ili afanye kazi.
“Sikutoa rushwa kwa kuwa ni dhambi na adui wa haki… niliacha mchakato huo wa kumpata rais ndani ya CCM ufanywe na Mungu,” alisema.
AOMBA POWER
Dk. Magufuli alisema wale wanaosalimia kwa kutumia salamu na kauli mbiu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Peoples Power, wampe ‘power’ aende Ikulu kuharakisha maendeleo ya watanzania.
“Nipeni wabunge na madiwani wa CCM nikafanye kazi, tutafanyakazi bila kinyongo, hatutawabagua, hapa ni kazi tu,” aliahidi.
Alisema maendeleo hayana chama, kabila wala rangi, hivyo amepanga kufanya kazi na makundi yote bila kubagua na kuomba kura kwa wananchi wote bila ya kujali vyama vyao vya siasa.
“Hakuna anayezaliwa kutoka tumboni mwa mama yake akiwa na kadi ya chama fulani, bali wanavikuta, hivyo msidangaywe na vyama, kinachotakiwa ni maendeleo,” alisema.
WALIMU VUMILIENI
Akizungumzia kuhusu madai ya walimu nchini, alisema kada hiyo siyo wito bali ni kazi, fedha na kuwafundisha wanafunzi kwenye shule walizopangiwa na serikali.
Alisema baada ya kuingia Ikulu, kazi yake ya kwanza itakuwa ni kuwalipa madeni wanaoyoidai serikali.
Magufuli aliwataka walimu kuwa wavumilivu na kuwaomba kumchagua kwa kura nyingi katika uchaguzi huo.
“Sitawaangusha, nitamtanguliza Mungu na kila mmoja katika sala zake aniombee nisijeanza kwa kiburi, kujiona, kusahau ahadi, niwe mtumishi wa watu, nikapendwe kwa utumishi na siyo bora utumishi,” alisema.
AWATANGAZIA KIAMA MAJANGILI
Aidha, Magufuli alitangaza kiama dhidi ya majangili wanaoshirikiana na askari wanyamapori kupora rasilimali za meno ya tembo na pembe za ndovu huku akishangazwa na kitendo cha askari wanyapori kulipwa mishahara vizuri na wenye silaha kwa kushindwa kuwalinda tembo kwenye hifadhi za wanyamapori nchini na kuuawa na meno yao kukatwa na kusafirishwa nchi za nje.
Alionya kuwa serikali yake haitakubali vitendo hivyo viendelee.
WAKURUGENZI
Pia, Magufuli alisema serikali yake itapiga marufuku wakurugenzi wa halmashauri nchini kutembelea magari ya kifahari na kukaa kwenye majengo mazuri wakati wanafunzi wakisoma wakiwa wamekaa chini madarasani.
Alitangaza kuwa elimu itakuwa ikitolewa bure kwenye shule za serikali na kuboresha mazingira ya kusomea.
Magufuli alionya kuwa watakaoshindwa kwenda na kasi yake katika kutumikia wananchi, watakazimika kuachia madaraka.
MAADHIMISHO MARUFUKU
Kadhalika, alisema katika serikali yake itakuwa ni marufuku kufanyika maadhimisho ya Wiki ya Maji kwa kuwa yana lengo la waandaji kulipana posho na kuvaa sare za fulana na kofia huku wananchi wakiteseka kwa kukosa maji safi na salama.
AWALIPUA WAPINZANI
Katika hatua nyingine, awalirushia kombora wapinzani, akiwataka wananchi wasiwachague kwa madai kuwa watasababishia mateso.
Alisema kwa sasa Tanzania inaelekea kwenye neema ya maliasili kama ya gesi, madini na wanyamapori, ndipo wapinzani wanajitokeza kuwalaghai watanzania kuwa wataleta mabadiliko makubwa.
AIAGIZA TANROADS
Katika hatua nyingine, Magufuli ameendelea kutumia wadhifa wake wa uwaziri wa Ujenzi kwa kumwagiza Wakala wa Barabara nchini (Tanroads) mkoa wa Mbeya, kujenga barabara ya kilomita moja mjini Mbalizi na kutangaza zabuni ya kilomita nne za barabara mjini Makongolosi ndani ya wiki moja.
Pia, amemwagiza Mtendaji Mkuu wa Tanroads, kupeleka fedha za ujenzi na upanuzi wa barabara hizo ndani ya wiki moja.
Akihutubia mikutano ya hadhara mjini Mbalizi na Makongolisi, alimpandisha jukwani Mwenyekiti wa Bodi ya Barabara ambaye ni Mkuu wa mkoa wa Mbeya, Abass Kandoro na kumtaka ampelekee maagizo hayo Meneja wa Tanroads wa mkoa huo aliyemtaja kwa jina la Lyakurwa.
“Mimi bado ni Waziri wa barabara, ukifika ofisini mweleze Lyakurwa barabara hii ianze kujengwa, leo (jana) nampigia Chief Executive (Mtendaji Mkuu) wa Tanroads alete fedha haraka, wiki hii nataka kuona kazi inaanza…natamani ningekuwa rais nianze kazi leo niguse na sekta nyingine,” aliagiza.
Akiwa katika katika mji wa Makongolosi, alimuita jukwaani Kandoro na iagiza Tanroads kutangaza zabuni ya kilomita nne za barabara za mjini Makongolosi.
“Mimi napenda mambo yaende harakaharaka, uwaziri wa ujenzi bado ninao, tukitoka hapa RC mwambie Meneja wa Tanroads atangaze zabuni ya kilomita nne mjini Masongolosi zianze kujegwa na fedha nitatoa, nataka muone kuwa nasema na kutekeleza,” alisema.
Chanzo: NIPASHE

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them ...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Mwana muziki Marufu kwa jina la Chuck Brown Afariki Dunia Akiwa na umri wa miaka 75

View Photo Gallery — Chuck Brown dies at 75: The “godfather of go-go” has died By Chris Richards, Updated: Wednesday, May 16, 4:42 PM Chuck Brown, the gravelly voiced bandleader who capitalized on funk’s percussive pulse to create go-go, the genre of music that has soundtracked life in black Washington for more than three decades, died May 16 at the Johns Hopkins University hospital in Baltimore. He was 75. The death, from complications from sepsis, was confirmed by his manager, Tom Goldfogle. Mr. Brown had been hospitalized for pneumonia. Known as the “Godfather of Go-Go,” the performer, singer, guitarist and songwriter developed his commanding brand of funk in the mid-1970s to compete with the dominance of disco. Like a DJ blending records, Mr. Brown used nonstop percussion to stitch songs together and keep the crowd on the dance floor, resulting in marathon performances that went deep into the night. Mr. Brown said the style got its name because “the music j...