Skip to main content

Konstebo Noel Paul Jenga Amejiua




Waziri wa mambo ya ndani Lawrence Masha

Mohammed Mhina, wa Jeshi la Polisi

Askari polisi mmoja ambaye ni Mkufunzi wa Tanzania police Academy, Konstebo Noel Paul Jenga33), amejiua leo kwa kujipiga risasi moja kichwani akiwa kwenye chumba cha kutunzia silaha kwenye Chuo hicho Jijini Dar es Salaam.

Mkuu wa Tanzania Police Academy SACP Alice Mapunda, amesema kuwa Kostebo Noel Jenga, amejiua majira ya saa moja asubuhi baada ya kupokea zamu ya ulinzi katika kituo kidogo cha Polisi cha Mfano, kilichopo Chuoni hapo.

SACP Mapunda amesema kuwa mara baada ya kupokea zamu ya ulinzi askari huyo aliwaruhusu wenzake waliokesha kwa ulinzi katika kituo hicho kisha kuandika taarifa ya kusudio lake la kujiua kwenye kitabu maalum cha shughuli za zamu maafufu kama OB.

Katika taarifa hiyo, iliyoandikwa saa 12.45 asubuhi, Konstebo Noel Jenga, alisema kuwa ameamua kujiua mwenyewe kwa hiyari yake bila ya kulazimishwa na mtu yoyote na ameomba asisumbuliwe mtu yeyote kutokana na tukio hilo.

Amesema baada ya kuandika taarifa hiyo, Konsetebo Noel Jenga, alianza kuwapigia simu baadhi ya nduguzake kuwaaga buriani na baada ya kumaliza kufanya hivyo alizima simu na kisha kuweka mtutu wa bunduki mdomoni na kujifyatulia risasi ambayo imesababisha kifo chake.

Marehemu Noeli alizaliwa Desemba 25, 1977 huko mjini Morogoro na baadaye kupata elimu ya msingi katika sule moja mjini Morogoro tangu mwaka 1986 hadi 1992 na kujiunga na masomo ya Sekonda kwenye Shule ya Sekondari ya Center mjini Dodoma kati Ya mwaka 1993 na 1996 kabla ya kujiunga na kidato cha tano na cha sita katika shule ya Sekondari ya Forest mjini Morogoro kati ya mwaka 1998 na 2000.

Alijiunga na Jeshi la Polisi katika Chuo cha polisi cha Kimataifa cha CCP cha Mjini Moshi mkoani Kilimanjaro mnamo Septemba 25, 2000 na kuhitimu mafunzo ya awali ya uaskari Polisi Mei 25, 2001.

Mara baada ya kumaliza mafunzo hayo alipangiwa mkoa wa Iringa ambapo alipelekwa katika kituo cha Polisi Ludewa kabla ya kuhamishiwa CCP Moshi mkoani kama Mkufunzi mwaka 2006 na kutokana na juhudi yake ya ukufunzi alihamishiwa katika Chuo Kikuu cha Polisi Jijini Dar es Saam ambacho sasa ni Tanzania Police Academy.

Kamanda Mapunda amesema kuwa Polisi wameanza uchunguzi wa chanzo cha kifo cha marehemu na kwamba mipango ya kusafirisha mwili wa marehemu kwenda kwao Morogoro inafanywa.

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.