Skip to main content

Tanesco Manyara limewatahadharisha wakazi wanaoendelea kufanya shughuli za kibinadamu karibu na miundombinu ya shirika hilo

Manyara%2BManager
Maneja wa Tanesco mkoa wa Manyara Gerson Manase akiongea na waandishi wa habari hawapo kwenye picha hivi karibuni katika kampeni ya kuhamasisha wananchi kuacha kufanya shughuli za kibinadamu karibu na miundombinu ya shirika hilo. 

 Na Mwandishi Wetu,
Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) Mkoa wa Manyara limewatahadharisha wakazi wanaoendelea kufanya shughuli za kibinadamu karibu na miundombinu ya shirika hilo na kusema kuwa hatua kali zitachukuliwa dhidi yao.

Tahadhari hiyo imetolewa na meneja wa Tanesco mkoa huo hivi karibuni, Gerson Manase kupitia kampeni maalumu inayofanywa na Tanesco makao makuu ikiwa na lengo la kuhamasisha juu ya athari za kuhujumu miundombinu ya shirika na kufanya shughuli karibu.

“Kuanzia sasa mkazi yoyote atakaye kiuka sheria na kufanya shughuli za kibinadamu karibu na miundombinu ya umeme, tutafyeka mazao yake yote na hatua nyingine za kisheria zitafuata,” alisema meneja huyo

Kwa sasa Tanesco Manyara inahudumia wilaya tatu ikiwemo Babati, Mbulu na Kateshi ambapo kuna wateja wapatao 28,000 na lengo ni kuongeza idadi zaidi.

Mitambo iliyosimikwa ina uwezo wa kuzalisha megawati 50 ila kwa sasa matumizi ni megawati 15 tu na kukaribisha wawekezaji kwani umeme upo wa kutosha.

Alisema wakazi hao walishalipwa fidia zao na shirika ili kupisha maeneo hayo ambayo ni hatarishi kwa maisha yao lakini kuna baadhi bado wanafanya shughuli za kilimo.

Aidha, alisema katika maeneo hayo kuna vyombo vya moto huwa vinatakiwa kupita kwa ajili ya ukaguzi wa miundombinu sasa wakati mwingine inashindikana kutokana na watu kupanda mazao katika njia hizo, matokeo yake kazi zinashindwa kufanyika kwa wakati.

Meneja alisema, “Tunatoa wito kwa wakazi wote waheshimu sharia kwani tulishaandika barua kwa wenyeviti wa vijiji kuhusiana na amza yetu. Lengo la shirika sio kumkomoa mtu ila na kuhakikisha maisha ya watu yanakuwa salama na umeme unapatikana kwa wakati,”

Katika hatua nyingine meneja huyo aliomba wakazi kuachana na tabia ya kuhujumu miundombinu hiyo na kuongeza mkoa huo umekithiri kwa wizi wa nyaya za umeme.

Alisema wizi huo unarudisha jitihada za shirika nyuma na maendeleo kwa ujumla kwani serikali inatumia gharama kubwa kwa ajili ya marekebisho.

Akitolea mfano hivi karibuni kuna wizi wa transformer ulitokea na kusababisha usumbufu mkubwa kwa wateja na shirika kwa ujumla, “Vitendo hivi vinaweza kuleta maafa makubwa, badala ya kuhujumu tunaomba washirikiane na sisi kukomesha wizi huu,”

Naye Kaimu Meneja Kitengo cha Mawasiliano Tanesco Leila Muhaji alisisitiza kwamba zoezi la uhamasishaji linafanyika nchi nzima lengo ni kutoa elimu ya madhara yanayoweza kupata watu wanaojaribu kuiba vifaa au kufanya shughuli karibu ya miundombinu ya umeme.

“Hili ni shirika lenu tunaomba ushirikiano wenu ili kuhakikisha tunakuwa na umeme wa kutosha na kuvutia wawekezaji wengi nchini, serikali inatumia fedha nyingi kwa ajili ya kufanya marekebisho,” alisema Muhaji.

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...