Skip to main content

Katibu Mkuu Wizara ya Maji na Umwagiliaji Profesa Kitila amezitaka Asasi zisizo za Kiserikali kuchangia katika uwekezaji


KATIBU MKUU Wizara ya Maji na Umwagiliaji Profesa Kitila Mkumbo ,ameyataka Mashirika ya maendeleo ya kimataifa,Taasis binafsi na Asasi zisizo za Kiserikali kuchangia katika uwekezaji wa miradi ya maji nchini.

Prof Mkumbo aliyasema hayo jana katika hoteli ya New Africa wakati wa majadiliano baina ya wadau wa sekta binafsi na Wizara ya Maji ,nakusema kuwa Serikali peke yake haiwezi kutatua kero ya maji nchini nakuyataka mashirika hayo kuunga mkono jitihada za serikali.

“Serikali inatekeleza maendeleo ya sekta ya maji kwakushirikisha halmashauri zote nchini, katika vipaumbele vya miaka mitano ambapo sekta ya maji ni miongoni mwao na ni sekta ambayo hupata pesa nyingi.

Alisema zipo jitihada    nyingi zinazofanywa na serikali katika kuhakikisha tatizo la maji linakwisha nakufikia malengo  ya Dunia namba sita lakini pia serikali ina malengo ya miaka mitano ambapo hadi sasa 58%-60 ya watu wa vijijini wanapata maji safi na salama.

Aidha Prof Mkumbo alisema kuwa sekta ya maji inawekeza katika matumizi yake katika maeneo makuu matatu yakiwemo umwagiliaji, majumbani, na umeme.
“Tumekutana na wenzetu hawa wadau wa maji nakuwataka wawekeze katika ushiriki wa viwanda kwakuwa  maji yapo yakutosha, kikubwa ni teknolojia na fedha kwa ajili ya kuvuna maji hayo na serikali pekee haiwezi."Alisema.

Naye Ofisa Mkuu Mtendaji wa mfuko wa UTT alisema kuwa serikali imewekeza vya kutosha katika sekta ya maji lakini mahitaji katika sekta hiyo ni makubwa hivyo sekta binafsi haina budi kuunga mkono serikali katika jitihada za kutatua tatizo la maji.

“Sekta binafsi inatakiwa nayo kufanya kwa nafasi yake kusaidia nakuna haja ya kushirikiana na halimashauri na watekelezaji wa miradi ya maji kwakuwapatia vitendea kazi mbalimbali.Alisema.

Hata hivyo Washima alisema kuwa wao kama UTT wamekuwa wakichangia miradi mbalimbali ya maji nchini inayotekelezwa katika halmashauri mbalimbali.

Comments