Skip to main content

Nyange alwataka Watanzania kujiwekea mazoea ya kutembelea hifadhi mbalimbali za Taifa

HIFADHI ya  Ngorongoro  pamoja na Hifadhi ya Taifa ya Serengeti ni moja ya
maajabu mapya nane ya Dinia,Mwaka 2010,kamati ya masuala ya Urithi wa Dunia 
ilitaja kuwa Hifadhi ya Norongoro kuwa Eneo la Utamaduni la urithi wa Dunia.
Afisa Uhusiano wa Hifadhi ya Ngorongoro Nickson Nyange wakati akizungumza na kuhusiana na maonyesho ya wiki ya mazingira

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi Dar es Salaam katika viwanja vya mnazi mmoja
katika muendelezo wa maonyesho ya wiki ya mazingira Afisa Uhusiano idara ya 
ya Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro Nickson Nyange aliwataka Watanzania kujiwekea 
mazoea ya kutembelea hifadhi mbalimbali za Taifa zilizopo hapa nchini 
ikiwemo Hifadhi ya Taifa ya Ngorongoro.

Alisema Tanzania imebarikiwa na Mungu kwa kuwa na vivutio vingi 
ambavyo vimesheheni maajabu lakini pia wanyama pori wa aina tofauti 
tofauti hivyo ni vyema wananchi wanaonyesha muamko wakwenda kutalii.

“Tumekuja kwenye viwanja nvya mnazi mmoja kwa lengo la kuwapatia elimu watanzania
 namna ambavyo wanapaswa kutembelea mbuga zetu za wanyama ili kushuhudia uumbaji 
wa Mungu”alisema Nyange

Katika suala la utunzaji wa mazingira alisema wanashiriki kwenye kampeni ya 
kuhakikisha wanayatunza na kuyahifadhi mazingiza ya hifadhi ikiwa ni pamoja 
na upandaji wa miti ili kuacha mazingira mazuri kwa vizazi vijanvyo.

Inaelezwa kuwa Hifazi ya Ngorongoro inasimamiwa na Mamlaka ya Hifadhi ya 
Ngorongoro ambayo kisheria inatekeleza majukumu yake makuu kama kuifadhi 
maliasili zilizo ndani ya Eneona pili inasimamia kukuza na kuendeleza 
utalii katika eneo la Hifadhi ya Ngorongoro.

“Miti mikubwa ambayo munaiona sasa hivi haikuoteshwa jana wala juzi wala mwaka 
jana bali ilioteshwa miaka mingi iliyopita hivyo tunapaswa kuyatunza na kuyahifadhi
 mazingira.”alimaliziea kusema Nyange.

Ngorongoro  ni eneo la kasoko kubwa nchini Tanzania, lenye umbali wa takriban
kilomita180 kutoka Arusha; pia ni hifadhi ya taifa inayojulikana kote duniani
 ambapo inasemekana Kuna jumla ya wanyamapori wakubwa takriban 25,000, wakiwa 
pamoja na  vifaru, viboko, nyumbu, pundamilia, nyati, simba, fisi na chui.

Comments