Skip to main content

HOSPITALI MLOGANZILA WAJIANDAA KUTIBU SELIMUNDU KWA KUPANDIKIZA UTE WA MIFUPA


MKUU wa Idara ya Hematolojia, Uwekaji wa Damu na Mtafiti Mkuu wa Program ya Selimundu katika Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili(MUHAS) Profesa Jullie Makani amesema wapo katika mchakato wa kutoa huduma ya kutibu Selimundu kwa Kupandikiza ute wa Mifupa

Prof.Makani amesema hayo leo jijini Dar es Salaam wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Selimundu Duniani yaliyofanyika katika Hospitali ya Mlaganzila ambapo amesema kwa sasa wapo katika mchakato wa mazungumzo na yakikamilika wanatarajia kuanza kutibu Selimundu kwa kutumia tiba ya Kupandikiza Ute wa mifupa kwa mgonjwa.

"Zipo njia mbili zinazotumika kutibu Selimundu.Njia ya kwanza ni kwa kutumia Hydroxyurea na ndio ambayo tunaitumia hapa nchini.Njia ya pili ni ya kutibu kwa kupandikiza ute wa mifupa ambayo kitalaam inafahamika Bone Marrow Transplant,"amefafanua.

Alipoulizwa ni lini wataanza kupandikiza ute wa mifupa kwa mgonjwa wa Selimundu katika hospitali hiyo amejibu wanatarajia kuanza mwakani iwapo mchakato utakwenda vizuri hata.Pia amesema haijafahamika gharama ya kutibu kwa kupandikiza ute wa mifupa itakuwa kiasi gani na ndio mazungumzo ambayo wanaendelea nayo kufanya.

Amefafanua nchini India wanatibu Selimundu kwa njia ya kupandikiza ute wa mifupa kwa gharama ya Dola 60,000 na hivyo moja ya jambo ambalo wanalifanya ni kuzungumza na wadau mbalimbali ili watakapoanza kuitoa huduma hiyo gharama iwe yenye unafuu.

Alipoulizwa iwapo mgonjwa wa Selimundu anaweza kutibiwa na kupona kabisa Profesa Makani amejibu inawezekana kwa njia ya kupandikiza ute wa mifuko kwa mgonjwa huku akielezea jitihada mbalimbali zinazofanywa katka kutafiti ugonjwa huo na kutafuta tiba yake.

Kuhusu ugonjwa huo nchini amesema watoto 11000 kila mwaka wanazaliwa wakiwa na Selimundu na nchini kwa takwimu za Dunia zinaonesha watoto 300,000 kwa mwaka.Tanzania inashika nafasi ya nne kwa ugonjwa huo.

Ameeleza kuna tafiti nyingi ambazo zinafanywa na zinaendelea kufanywa na MUHAS katika kutafuta tiba ya ugonjwa huo.Pia wamekuwa wakiendelea kufanya tafiti kwa wanaougua ugonjwa huo.

Profesa Makani alipoulizwa mgonjwa mwenye Selimundu nini ambacho anakabiliana nacho, amejibu kuwa mgonjwa wa Selimundu anakabiliwa na maumivu makali ya mwili na kupungukiwa damu mara kwa mara.

Wakati huohuo Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili(MUHAS)Profesa Appolinary Kamuhabwa amesema pamoja na kufanya tafiti za Selimundu pia wamekuwa wakifanya tafiti mbalimbali huku akieleza kuwa wameamua Hospitali ya Mlongazila kuwa eneo la tafiti za magonjwa.

"Pamoja na kutoa taaluma ya tiba ya afya, tumekuwa tukijikita kufanya tafiti za magonjwa mbalimbali  na sasa Hospitali ya Mloganzila ni eneo ambalo litatumika kufanya tafiti hizo,"amesema.

Amefafanua wamejikita katika kutoa mafunzo, kuhudumia wagonjwa na kufanya tafiti , hivyo wanajivunia kwani wamekuwa wakifanya tafiti nyingi na zimeleta matokeo chanya.

Kwa upande wake Naibu Makamu Mkuu wa Chuo-Huduma za Hospitali Profesa Said Aboud ametumia nafasi hiyo kuwahimiza wananchi kufika kwenye hospitali hiyo kupata huduma bora ambazo zinatolewa na madaktari bingwa na wabobezi.

Amesema wanatoa huduma ya kutibu magonjwa mbalimbali na wanayo maabara ya kisasa pamoja na vifaa tiba vya kutibu magonjwa mbalimbali.
MI3
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MuHAS) Profesa Appolinary Kamuhabwa akizungumza wakati wa maadhimisho ya siku ya Ugonjwa wa Seli Mundu yaliyofanyika kwenye Chuo Kikuu hicho Kampasi ya Mloganzila leo na kushirikisha Madaktari Bingwa, Watafiti wa Magonjwa na Tiba mbalimbali na wauguzi, Profesa Kamuhabwa amesema chuo hicho mpaka sasa ina miradi ya utafiti wa magonjwa mbalimbali pamoja na tiba inayofikia 92.
MI1
Profesa Julie Makani Mkuu wa Idara ya Hematolojia , Uwekaji wa Damu na Mtafiti Mkuu wa Programu ya Seli Mundu (MuHAS)akizungumza katika maadhimisho ya siku ya Seli Mundu yaliyofanyika katika Chuo hicho Kampasi ya Moganzila leo.Profesa Julie Makani Mkuu wa Idara ya Hematolojia , Uwekaji wa Damu na Mtafiti Mkuu wa Programu ya Seli Mundu (MuHAS) akizungumza katika maadhimisho ya siku ya Seli Mundu yaliyofanyika katika Chuo hicho Kampasi ya Moganzila leo.MI2
MI4
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MuHAS) Profesa Appolinary Kamuhabwa katikati ,Profesa Julie Makani Mkuu wa Idara ya Hematolojia , Uwekaji wa Damu na Mtafiti Mkuu wa Programu ya Seli Mundu (MuHAS) kushoto na Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Huduma za Hospitali Profesa Said Aboud wakifuatilia baadhi ya taarifa za tafiti zilizokuwa zikionyeshwa kwenye Projekta. 
MI05
MI5Baadhi ya wataalamu na madaktari mbalimbali wakiwa katika maadhimisho hayo. 
Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Huduma za Hospitali Profesa Said Aboud akitoa shukurani zake wakati wa maadhimisho hayo mara baada ya kutolewa kwa taarifa mbalimbali za kiutafiti katika chuo hicho.
MI8
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MuHAS) Profesa Appolinary Kamuhabwa katikati ,Profesa Julie Makani Mkuu wa Idara ya Hematolojia , Uwekaji wa Damu na Mtafiti Mkuu wa Programu ya Seli Mundu (MuHAS) kushoto na Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Huduma za Hospitali Profesa Said Aboud wa pili kutoka kushoto pamoja na Kaimu Mkurugenzi wa Udahili na Uzamivu (MuHAS) Emmanuel Balondya kushoto wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Madaktari Bingwa, Wataalam na Watafiti wa chuo hicho.
MI7

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.