Skip to main content

Rais Dk. John Pombe Magufuli Mgeni Rasmi ASDP 11



Rais Dk. John Pombe Magufuli anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika
Uzinduzi wa Programu ya Kuendeleza Sekta ya Kilimo  Awamu ya Pili (ASDP 11) utakaofanyika jijini Dar es Salaam Juni 4 mwaka huu katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu J.k Nyerere.



 Waziri wa Kilimo Dkt.Charles Tizeba akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na Uzinduzi wa ASDP 11wa awamu ya pili utakaofanyika jijini Dar es Salaam.

Uzinduzi huo utahusisha Wizara za kisekta ikiwemo Wizara ya Kilimo, Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Viwanda , Biashara na Uwekezaji na Wizara ya Maji na Umwagiliaji.
Hayo yamesemwa leo jijini Dar es Salaam na Waziri wa Kilimo Dk. Charles Tizeba wakati akizingumza na wanahabari kuhusiana na uzindunzi wa programu hiyo.
Amesema shughuli za uzinduzi zitaanza saa 2:00 asubuhi na kwamba progamu hiyo itatekelezwa  katika mikoa na wilaya zote kwa kuzingatia mazao ya kipaumbele na ikolojia ya kilimo ya kanda 10 kwa vipindi viwili vya miaka mitano ambapo kipindi cha kwanza kitaanza  2018/19 hadi 2023/24.
Amebainisha kuwa lengo la ASPDP ni  kuleta mageuzi katika sekta ya kilimo ili kuongeza uzalishaji tija kwenye kilimo, mifugo na uvuvi, kuongeza pato la taifa la wakulima, wafugaji na wavui pamoja na pato la taifa kuwa  na uhakika wa usalama wa chakula na lishe.
Amesisitiza kuwa program hiyo itatekeleza sera mbalimbali ikiwemo Sera ya kilimo ya Taifa, mifugo, uvuvi, masoko ya mazao ya kilimo, umwagiliaji ya taifa, usalama wa chakula na lishe, ugatuaji madaraka, maendeleo ya ushirika na Sera ya mashirikiano kati ya sekta za umma na sekta binafsi.
Amefafanua kuwa washiriki ni wadau sekta ya kilimo, mifugo, uvuvi ushirika, wizara, taasisi za Serikali na zisizo za kiserikali, washirika wa maendeleo, sekta binafsi na wananchi kwa ujumla.
Ameongeza kuwa endapo ASPDP itasimamiwa kikamilifu hadi kufikia mwaka 2020 nchi itafikia uchumi wa kati.
Ameviomba vyombo vya habari kuishikilia kidete progaramu kupitia makala za magazeti, radio pamoja na vipindi vya televisheni kwa kutoa elimu kwa wananchi kuhusiana na masuala ya kilimo.

Comments