Skip to main content

Mrema apewa siku 80 kufanya uchaguzi TLP


Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, imetoa siku 80 kwa uongozi wa Chama cha Tanzania Labour (TLP) kuhakikisha kinafanya uchaguzi wake wa ndani wa kuwapata viongozi wapya.
Kauli hiyo imeitolewa baada ya baadhi ya wanachama wa chama hicho kufikisha malalamiko katika ofisi hiyo wakiiomba itangaze kwamba uongozi wa Mwenyekiti wa chama hicho, Augustine Mrema umefikia kikomo.
Mwenyekiti wa Kamati ya Ukweli na Maridhiano wa TLP Taifa, Joram Kinanda alimtuhumu Mrema kukiuka katiba ya chama hicho, kuongoza chama kidikteta, kuporomosha heshima ya chama na kujilimbikizia madaraka.
Akizungumza ofisini kwake, Dar es Salaam jana, Msaidizi wa Msajili wa Vyama vya Siasa, Sisty Nyahoza alisema baada ya kusikiliza pande zote zinazosigana ofisi hiyo iliwataka viongozi kuandaa uchaguzi.
"Tuliwasikiliza wote upande wa Kinanda na upande wa Mrema ambaye alikuwa na sababu kwamba alishindwa kuitisha uchaguzi kutokana na hali yake ya afya lakini tumewaandikia barua kuwa ifikapo Aprili 26 wawe wamekwisha kufanya uchaguzi na si vinginevyo," alisema Nyahoza na kuongeza: "Vyama hivi ili viweze kujinasua na migogoro ya mara kwa mara lazima vijiendeshe kama taasisi na si chama cha mtu mmoja. Hii itasaidia kukuza demokrasia nchini na siku zote demokrasia inaanzia katika vyama vyetu ndipo inakuja juu. kama vyama havina demokrasia ni ngumu hata huku juu kuwapo."
Malalamiko ya Kinanda yalitolewa pia na aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chama hicho, Jeremiah Shelukindo aliposema jana kuwa aliamua kuandika barua ya kujiuzulu tangu Desemba 15 mwaka jana kutokana na kutoridhishwa na uongozi wa Mrema. Akizungumzia uamuzi huo Mrema alisema: "Kwanza tunaishukuru Ofisi ya Msajili kwani ilielewa sababu tulizozitoa za kutofanya uchaguzi, katiba yetu inaturuhusu kufanya hivyo na tutatekeleza agizo hilo.
"Ofisi ya Msajili ilituhakikishia lazima tufanye uchaguzi kamati kuu yetu imekubaliana kwamba uchaguzi utafanyika Aprili 26 na maandalizi ya uchaguzi huo yanakwenda vizuri."
Mrema ambaye pia ni Mbunge wa Vunjo akizungumzia tuhuma za Shelukindo alisema, "Hazina ukweli wowote na tunaendesha chama kwa kuzingatia Katiba na kanuni za chama na hao wanaosema mimi ni dikteta, hakuna jambo kama hilo.
Vyama vinne vyasajiliwa
Katika hatua nyingine, ikiwa imebaki miezi minane kabla ya kufanyika kwa Uchaguzi Mkuu, vyama vinne vya siasa vimewasilisha barua ya maombi ya usajili katika Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, huku vingine viwili vikipatiwa usajili wa muda.
Vyama vilivyopata usajili wa muda ni; Chama cha Wananchi na Demokrasia (Chawade) kilichoasisiwa na Shabiri Mpaka na Pilly Athuman na Chama cha Maridhiano na Uwiano (CMU) chini ya waasisi Jamali Abdallah na Shaibu Hemed Likwimbi.
Chama cha Kijamii na Uzalendo Tanzania (CKUT), chini ya waasisi wake Ramadhan Semtawa na Noel Antapa kiliwasilisha maombi yake Januari 6. Vingine vilivyowasilisha barua ya maombi tangu mwaka jana ni; Chama cha Demokrasia na Umoja (Dau) ambacho waasisi ni Idd Mwishwa na Lazaro Mwalusamba, Restoration of the National (RNP) chini ya waasisi Atis Jacob Atto na Jenesta Josia na True Conscious for Liberation (TRUCOLI) ambacho kimeasisiwa Leonard Nyongani na Boniface Magesa.CHANZO:MWANANCHI

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...