Skip to main content

Mrema apewa siku 80 kufanya uchaguzi TLP


Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, imetoa siku 80 kwa uongozi wa Chama cha Tanzania Labour (TLP) kuhakikisha kinafanya uchaguzi wake wa ndani wa kuwapata viongozi wapya.
Kauli hiyo imeitolewa baada ya baadhi ya wanachama wa chama hicho kufikisha malalamiko katika ofisi hiyo wakiiomba itangaze kwamba uongozi wa Mwenyekiti wa chama hicho, Augustine Mrema umefikia kikomo.
Mwenyekiti wa Kamati ya Ukweli na Maridhiano wa TLP Taifa, Joram Kinanda alimtuhumu Mrema kukiuka katiba ya chama hicho, kuongoza chama kidikteta, kuporomosha heshima ya chama na kujilimbikizia madaraka.
Akizungumza ofisini kwake, Dar es Salaam jana, Msaidizi wa Msajili wa Vyama vya Siasa, Sisty Nyahoza alisema baada ya kusikiliza pande zote zinazosigana ofisi hiyo iliwataka viongozi kuandaa uchaguzi.
"Tuliwasikiliza wote upande wa Kinanda na upande wa Mrema ambaye alikuwa na sababu kwamba alishindwa kuitisha uchaguzi kutokana na hali yake ya afya lakini tumewaandikia barua kuwa ifikapo Aprili 26 wawe wamekwisha kufanya uchaguzi na si vinginevyo," alisema Nyahoza na kuongeza: "Vyama hivi ili viweze kujinasua na migogoro ya mara kwa mara lazima vijiendeshe kama taasisi na si chama cha mtu mmoja. Hii itasaidia kukuza demokrasia nchini na siku zote demokrasia inaanzia katika vyama vyetu ndipo inakuja juu. kama vyama havina demokrasia ni ngumu hata huku juu kuwapo."
Malalamiko ya Kinanda yalitolewa pia na aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chama hicho, Jeremiah Shelukindo aliposema jana kuwa aliamua kuandika barua ya kujiuzulu tangu Desemba 15 mwaka jana kutokana na kutoridhishwa na uongozi wa Mrema. Akizungumzia uamuzi huo Mrema alisema: "Kwanza tunaishukuru Ofisi ya Msajili kwani ilielewa sababu tulizozitoa za kutofanya uchaguzi, katiba yetu inaturuhusu kufanya hivyo na tutatekeleza agizo hilo.
"Ofisi ya Msajili ilituhakikishia lazima tufanye uchaguzi kamati kuu yetu imekubaliana kwamba uchaguzi utafanyika Aprili 26 na maandalizi ya uchaguzi huo yanakwenda vizuri."
Mrema ambaye pia ni Mbunge wa Vunjo akizungumzia tuhuma za Shelukindo alisema, "Hazina ukweli wowote na tunaendesha chama kwa kuzingatia Katiba na kanuni za chama na hao wanaosema mimi ni dikteta, hakuna jambo kama hilo.
Vyama vinne vyasajiliwa
Katika hatua nyingine, ikiwa imebaki miezi minane kabla ya kufanyika kwa Uchaguzi Mkuu, vyama vinne vya siasa vimewasilisha barua ya maombi ya usajili katika Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, huku vingine viwili vikipatiwa usajili wa muda.
Vyama vilivyopata usajili wa muda ni; Chama cha Wananchi na Demokrasia (Chawade) kilichoasisiwa na Shabiri Mpaka na Pilly Athuman na Chama cha Maridhiano na Uwiano (CMU) chini ya waasisi Jamali Abdallah na Shaibu Hemed Likwimbi.
Chama cha Kijamii na Uzalendo Tanzania (CKUT), chini ya waasisi wake Ramadhan Semtawa na Noel Antapa kiliwasilisha maombi yake Januari 6. Vingine vilivyowasilisha barua ya maombi tangu mwaka jana ni; Chama cha Demokrasia na Umoja (Dau) ambacho waasisi ni Idd Mwishwa na Lazaro Mwalusamba, Restoration of the National (RNP) chini ya waasisi Atis Jacob Atto na Jenesta Josia na True Conscious for Liberation (TRUCOLI) ambacho kimeasisiwa Leonard Nyongani na Boniface Magesa.CHANZO:MWANANCHI

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.