Skip to main content

Bei ya umeme kushuka Machi


Mkurugenzi mkuu wa mamlaka ya udhibiti wa nishati, maji nchini Felix Ngalamgosi akizungumza na waandishi wa habari
Mkurugenzi mkuu wa mamlaka ya udhibiti wa nishati, maji nchini Felix Ngamlagosi akizungumza na waandishi wa habari
Serikali imeshusha bei ya umeme nchini kwa asilimia 2.21 kuanzia mwezi Machi mwaka huu.
Bei hiyo itatumika katika kipindi cha miezi mitatu wakati mapitio mapya yakiwa yanafanyika kulingana na mfumuko wa bei.
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Udhibiti wa huduma za Nishati na Maji (Ewura), Felix Ngamlagosi, alisema hatua hiyo imekuja baada ya kupitia gharama ya uzalishaji wa umeme kwa kuzingatia mabadiliko ya bei ya mafuta, thamani ya shilingi ya Tanzania na mfumuko wa bei.
Alisema  kufuatia bei hiyo mpya watumiaji wa majumbani  wamepunguziwa kwa shilingi nane kutoka Sh. 306 hadi Sh. 298.
Watumiaji wa kati wanaotumia umeme wa Volti 400, bei itashuka kutoka Sh. 205 hadi Sh. 200 kwa uniti moja, sawa na punguzo la Shilingi tano kwa uniti.
Wateja wakubwa walionganishwa katika msongo wa kati wa umeme, watapunguziwa kwa Shilingi nne, ambapo watanunua Sh. 159 badala ya Sh. 163 ya awali.
Kwa wateja waliounganisha katika msongo mkubwa wa umeme kama migodi na Shirika la Umeme Zanzibar, watapunguziwa Shilingi tatu, wamepunguziwa gharama kutoka Sh. 159 hadi Sh. 156 kwa uniti moja.
“Kwa wateja wa majumbani wenye matumizi madogo ya wastani wa uniti 75 kwa mwezi, bei ya umeme haitabadilika kutokana na kundi hilo kuchangiwa gharama na wateja wakubwa wa majumbani,” alisema.
Ngamlagosi alisema wateja hao wadogo wa majumbani wataendelea kulipia Sh. 100 kwa uniti moja.
Aidha akizungumzia namna walivyokokotoa gharama hizo, alisema katika kupindi hicho Tanesco iliokoa Sh. Bilioni 57 baada ya uzalishaji kuwa wa chini kwa mitambo ya uzalishaji inayotumia mafuta mazito na ya ndege..
Alisema katika kipindi hicho thamani ya shilingi ilishuka kwa wastani wa asilimia 7.28, wakati mfumuko wa bei uliongeza mahitaji ya pato la Tanesco kwa Sh. Bilioni 17.
Ngamlagosi gharama halisi ya pato la Tanesco kwa mwaka huo ulikuwa Sh. Bilioni 33.
Hata hivyo, alisema bei hiyo  itadumu kwa muda wa miezi mitatu baada ya kuwepo kwa kifungu cha kanuni kinachotaka bei elekezi katika huduma hiyo kubadilika kila mara.
Alisisitiza yapo matumaini ya kushuka zaidi kwa bei ya umeme baada ya kuanza kwa uzalishaji wa nishati hiyo kupitia mitambo ya Kinyerezi pamoja na kufanya marekebisho kwa mitambo iliyopo kutoka kuendeshwa kwa kutumia mafuta badala yake kutumia gesi.
Chanzo: NIPASHE

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.