Skip to main content

Bei ya umeme kushuka Machi


Mkurugenzi mkuu wa mamlaka ya udhibiti wa nishati, maji nchini Felix Ngalamgosi akizungumza na waandishi wa habari
Mkurugenzi mkuu wa mamlaka ya udhibiti wa nishati, maji nchini Felix Ngamlagosi akizungumza na waandishi wa habari
Serikali imeshusha bei ya umeme nchini kwa asilimia 2.21 kuanzia mwezi Machi mwaka huu.
Bei hiyo itatumika katika kipindi cha miezi mitatu wakati mapitio mapya yakiwa yanafanyika kulingana na mfumuko wa bei.
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Udhibiti wa huduma za Nishati na Maji (Ewura), Felix Ngamlagosi, alisema hatua hiyo imekuja baada ya kupitia gharama ya uzalishaji wa umeme kwa kuzingatia mabadiliko ya bei ya mafuta, thamani ya shilingi ya Tanzania na mfumuko wa bei.
Alisema  kufuatia bei hiyo mpya watumiaji wa majumbani  wamepunguziwa kwa shilingi nane kutoka Sh. 306 hadi Sh. 298.
Watumiaji wa kati wanaotumia umeme wa Volti 400, bei itashuka kutoka Sh. 205 hadi Sh. 200 kwa uniti moja, sawa na punguzo la Shilingi tano kwa uniti.
Wateja wakubwa walionganishwa katika msongo wa kati wa umeme, watapunguziwa kwa Shilingi nne, ambapo watanunua Sh. 159 badala ya Sh. 163 ya awali.
Kwa wateja waliounganisha katika msongo mkubwa wa umeme kama migodi na Shirika la Umeme Zanzibar, watapunguziwa Shilingi tatu, wamepunguziwa gharama kutoka Sh. 159 hadi Sh. 156 kwa uniti moja.
“Kwa wateja wa majumbani wenye matumizi madogo ya wastani wa uniti 75 kwa mwezi, bei ya umeme haitabadilika kutokana na kundi hilo kuchangiwa gharama na wateja wakubwa wa majumbani,” alisema.
Ngamlagosi alisema wateja hao wadogo wa majumbani wataendelea kulipia Sh. 100 kwa uniti moja.
Aidha akizungumzia namna walivyokokotoa gharama hizo, alisema katika kupindi hicho Tanesco iliokoa Sh. Bilioni 57 baada ya uzalishaji kuwa wa chini kwa mitambo ya uzalishaji inayotumia mafuta mazito na ya ndege..
Alisema katika kipindi hicho thamani ya shilingi ilishuka kwa wastani wa asilimia 7.28, wakati mfumuko wa bei uliongeza mahitaji ya pato la Tanesco kwa Sh. Bilioni 17.
Ngamlagosi gharama halisi ya pato la Tanesco kwa mwaka huo ulikuwa Sh. Bilioni 33.
Hata hivyo, alisema bei hiyo  itadumu kwa muda wa miezi mitatu baada ya kuwepo kwa kifungu cha kanuni kinachotaka bei elekezi katika huduma hiyo kubadilika kila mara.
Alisisitiza yapo matumaini ya kushuka zaidi kwa bei ya umeme baada ya kuanza kwa uzalishaji wa nishati hiyo kupitia mitambo ya Kinyerezi pamoja na kufanya marekebisho kwa mitambo iliyopo kutoka kuendeshwa kwa kutumia mafuta badala yake kutumia gesi.
Chanzo: NIPASHE

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Uganda Police issue fresh terror alert

  By Chris Kiwawulo, The Police have issued a fresh terror alert against a possible attack on Uganda by four terrorists from Kazakhstan. Police spokesperson Judith Nabakooba “We have received a security notification in form of an orange notice of four terrorists originating from Kazakhstan who are planning to travel to foreign countries in order to commit attacks and participate in hostile acts,” Police spokesperson Judith Nabakooba said in a statement on Monday. Nabakooba named the four active members of radical organizations as; Nassiruauly Kairat, Umurzakov Marat Eskendirovich, Kovtun Denis Valerevich and Mazhibayen Alimzhan Akhlazhanovich. By press time, a search on the international web has not yielded anything on the named persons.Last evening, police said that in collaboration with other security agencies vigilance has been stepped up to avert the terrorists’ evil plans. Police have in the past issu...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...