Skip to main content

Gwajima, Flora Mbasha wafunguka


Mchungaji Josephat Gwajima
Mchungaji Josephat Gwajima
Siku chache baada ya picha za mtoto mchanga kusambazwa katika mitandao ya kijamii na kudai kuwa ni za mtoto wa mwimbaji wa nyimbo za Injili nchini, Flora Mbasha kuwa amezaa na Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima hatimaye wawili hao wamefunguka.
Hatua hiyo imekuja miezi saba tangu wawili hao walipoingia katika mgogoro wa ndoa yao hali iliyosababisha mume wa Flora, Emmanuel Mbasha kufikishwa mahakamani kwa kosa la ubakaji.
Akizungumza na MTANZANIA jijini Dar es Salaam jana ili kupata ukweli kuhusu taarifa za picha za mtoto huyo ambaye anadaiwa kuwa amezaa na Flora, Mchungaji Gwajima, alisema taarifa hizo ni za uzushi na huenda zinasambazwa na mume wa Flora.
Mchungaji Gwajima alikwenda mbali na kusema pamoja na uzushi huo unaosambazwa dhidi yake kwa kuhusishwa katika uhusiano na Flora anamwachia Mungu kila kitu.
“Hahaha… si unajua hiyo issue (suala, jambo) ya Mbasha ni ya muda mrefu tu… wakati mwingine mimi huwa sijibu ujinga,” alisema Gwajima huku akicheka.
“Awali niliwaza kuwashitaki (alipoanza kuhusishwa kwamba ana uhusiano na Flora) wanaoeneza uzushi huo lakini nikaona ‘It doesn’t hold water’ (haina mashiko), najua shutuma hizo zinatoka wapi,” alisema Mchungaji Gwajima.
Alipoulizwa kuhusu mtu anayemshuku kueneza uvumi huo alisema: “Probably’ (nadhani) atakuwa Emmanuel Mbasha mwenyewe. Tangu mwanzo alipotuhumiwa kumbaka shemeji yake na kutoroka kwake akihofia kukamatwa na polisi, mkewe alikuja kanisani kwetu na mimi nilimwagiza mwenyekiti wa kusaidia jamii amsaidie,” alisema Gwajima na kuongeza:
“Sasa Mbasha alipotoka huko alikokimbilia na kusikia kuwa mkewe yuko hapa kanisani, ndipo alipoanza kueneza uzushi,” alisema.
Gwajima alisisitiza kuwa Flora hakufikia kwake kwa jambo lolote bali aliendelea kuishi katika nyumba aliyopanga.
Alipoulizwa kwa nini hamshitaki Mbasha ili kulinda heshima yake, Gwajima alisema ameshawaita ndugu zake akiwemo baba yake mzazi lakini nao wakaonekana kutommudu Emmanuel.
“Nilishawaita wazazi wake, baba na mama yake, ndugu zake kina Mbasha na tukazungumza. Lakini baba yake alisema hata yeye amemshindwa. Yaani anawadharau hata ndugu zake,” alisema.
Akisimulia jinsi alivyokutana na Emmanuel na Flora Mbasha, Mchungaji Gwajima alisema awali walikuwa wakiimba kwenye mikutano aliyokuwa akihubiri.
“Hawa hawakuwa washirika wetu, ila walikuwa wakija kuimba kwenye mikutano yetu ya Injili. Walikuja Arusha, Moshi na Tanga, kwa hiyo tulikuwa tukiwatumia sana. Baadaye ndiyo yakatokea hayo hadi Flora akakimbilia kanisani kwetu,” alisema.
Hata hivyo Gwajima alisema hakujua kama Flora ni mjamzito wakati anakuja kuomba msaada kanisani kwake.
“Mimi sikujua kama alikuwa mjamzito, hata taarifa kwamba amejifungua ndiyo nazisikia kwako. Hapa nimetoka ‘airport’, sikuwepo Dar es Salaam,” alisema na kuongeza:
“Sasa kama mtu una wasiwasi na mtoto si ukapime DNA ili upate uhakika? Hii ni habari ya kutaka tu kulichafua kanisa na huduma,” alisisitiza.
FlORA ANENA
Gazeti hili lilimtafuta Flora kwa njia ya simu ili kuzungumzia suala hilo ambapo alisema “Siko tayari kuzungumza lolote kuhusu Mbasha kwa sasa. Yeye anajeuri ya pesa ndo maana anafanya haya yote lakini mimi ninasimama na Mungu wangu na ninajua Mungu atanipigania,” alisema Flora.
Alipoulizwa kuhusu hali ya mtoto wake mchanga, alisema “Mtoto hajambo, lakini mtoto anayesambazwa kwenye mitandao siyo wangu, na hizo picha nyingine nafikiri ni za kutengeneza tu,” alisema Flora.
EMMANUEL MBASHA
Kutokana na hali hiyo MTANZANIA ilimtafuta mume wa Flora, Emmanuel Mbasha, ili kuzungumzia suala hilo, licha ya kupokea simu yake ya kiganjani, aliishia kusema yuko njiani hivyo apigiwe baadaye.
Hata alipopigiwa baadaye, aliendelea kusema kuwa atafutwe baadaye na wala hakujibu ujumbe wa simu (sms).
Alipotafutwa kwa njia ya ujumbe mfupi wa WhatsApp, ujumbe huo ulionekana kufika na kusomwa na baada ya muda alituma ujumbe wa sauti uliokuwa na wimbo na kuandika maneno mafupi yaliyosomeka ‘wimbo wangu mpya’.
Pamoja na mambo mengine, wimbo huo unamaneno yasemajo “Haribu mipango ya shetani, haribu…, Binadamu wengine mashetani mfano wa Cobra, wanawaza mabaya, kuna siku watakufa kabisa,” ulisikika ujumbe wa wimbo huo
Sehemu nyingine ya wimbo huo ulioimbwa kwa mwelekeo wa mipasho, inasema “Wanakesha kwa waganga kuliloga, darubini ya bwana imewamulika, ukiwaona utadhani ni wema,”
Kwa mujibu wa taarifa zilizopo katika tovuti ya kituo cha televisheni ya East Africa (EATV), Agosti 27, mwaka jana Flora alihojiwa na kituo hicho kupitia kipindi cha Kikaangoni Live, kinachoendeshwa kwa njia ya mtandao wa kijamii wa Facebook, alisema ujauzito aliokuwa nao ni wa mumewe Mbasha na si Mchungaji Gwajima.
Flora alisema kuwa hawezi kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Mchungaji Gwajima kwa kuwa ni mjomba wake na kwamba watu wamekuwa wakizusha kwa lengo la kumchafua na kumshushia hadhi.
“Hayo ni maneno tu ya watu mtaani ila Mchungaji Gwajima ni mtumishi wa Mungu na ni ‘Uncle’ wangu ninawezaje kuwa na uhusiano na uncle wangu..? ” alihoji Flora.
Kuhusu kuachana na Mbasha, Flora alisema hakuachana naye kwa sababu ya Gwajima na amedai kuwa bado anampenda, lakini anampenda Mungu zaidi.
“Sijamwacha mume wangu sababu ya Gwajima na kweli bado napenda sana Mbasha lakini nampenda zaidi Mungu,” alisema Flora.
Chanzo: MTANZANIA

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.