Skip to main content

IS wavamia ngome ya Marekani


iraq usa 

Kati ya wapiganaji 20 au 25 wa kikundi cha IS hapo jana walijaribu kuingia kwenye kambi ya mafunzo ya vikosi 400 vya Iraq na marekani huku wakiwa wamevaa sare za jeshi la Iraq.
Wapiganaji hao waliuawa kwa shambulizi lililofanywa na wanajeshi wa Iraq na hakuna ofisa yeyote wa Marekani ambaye aliathirika na shambulizi hilo.
Taarifa iliyotolewa na muungano huo imethibitisha kutokea kwa shambulizi hilo.
Taarifa iliyotolewa ilikuwa inasema hivi ” kundi dogo la wapiganaji wa ISIS waliokuwa wamevalia sare za jeshi la Iraq walivamia ngome yetu ya Al Asad Air Base jimboni Anbar muda wa saa 7:20 asubuhi”.

Comments