Skip to main content

Simba matumaini kibao : yasaka ushindi sasa.

Kocha mkuu wa timu ya Simba, Mzambia Patrick Phiri, amesema kikosi chake kina ari ya juu ya ushindi na kitashuka uwanjani kuwakabili wapinzani wao Prisons katika mechi ya Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara Jumamosi kwa tahadhari ili waweze kupata pointi tatu muhimu.
Simba iliondoka jijini Dar es Salaam jana asubuhi na jioni iliwasili salama Mbeya tayari kwa mchezo huo utakaofanyika kwenye Uwanja wa Sokoine.
Phiri aliliambia gazeti hili kwamba kila timu inapokuwa kwenye Uwanja wa nyumbani hujiamini zaidi lakini wao wamejipanga kukabiliana na ushindani kutoka kwa wenyeji wao Prisons.
Kocha huyo alisema ligi ya Bara msimu huu ni ngumu na ushindi unaweza kupatikana ugenini au nyumbani.
"Ligi ina ushindani na changamoto, lakini pia hakuna mwenye uhakika wa kushinda nyumbani, hata ugenini timu inaweza kushinda, hicho ndicho ninachokiamini mimi, soka limebadilika," alisema Phiri.
Aliongeza kuwa, kikosi chake kinatarajia kuanza mazoezi leo asubuhi na jioni wataendelea kujinoa ili kujiweka tayari kuwakabili wenyeji.
Naye Rais wa Simba, Evans Aveva, alisema wameamua kwenda mapema Mbeya ili kutoa nafasi ya wachezaji kupumzika na hatimaye kuendelea na mazoezi kwa muda wa siku mbili.
Aveva alisema kuwa wanaamini mazoezi waliyofanya katika kambi ya Afrika Kusini itawasaidia
kuendelea kuonyesha kiwango cha juu na hatimaye 'kuzoa' pointi tatu za kwanza msimu huu."Timu imeshaenda Mbeya, tunaamini mambo yatakuwa mazuri huko ingawa hakuna timu ya kuidharau kwenye ligi hii," alisema Aveva.
Rais huyo aliongeza kuwa huenda timu hiyo ikacheza mechi ya 'ndondo' mkoani Iringa mara baada ya kumaliza mchezo huo Jumamosi.
Baada ya mechi ya Jumamosi, Simba itacheza mechi nyingine ugenini dhidi ya Mtibwa Sugar itakayofanyika Novemba Mosi kwenye Uwanja wa Jamhuri mkoani Morogoro.
Wekundu wa Msimbazi wamecheza mechi nne na wana pointi nne mkononi wakati vinara wa ligi hiyo ni mabingwa watetezi, Azam ambao wana pointi 10 sawa na Mtibwa Sugar.
Kipa chipukizi, Peter Manyika 'Junior' anatarajiwa kusimama tena langoni katika mechi hiyo kutokana na makipa wengine, Ivo Mapunda na Hussein 'Casillas' kuwa majeruhi.
CHANZO: NIPASHE

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Uganda Police issue fresh terror alert

  By Chris Kiwawulo, The Police have issued a fresh terror alert against a possible attack on Uganda by four terrorists from Kazakhstan. Police spokesperson Judith Nabakooba “We have received a security notification in form of an orange notice of four terrorists originating from Kazakhstan who are planning to travel to foreign countries in order to commit attacks and participate in hostile acts,” Police spokesperson Judith Nabakooba said in a statement on Monday. Nabakooba named the four active members of radical organizations as; Nassiruauly Kairat, Umurzakov Marat Eskendirovich, Kovtun Denis Valerevich and Mazhibayen Alimzhan Akhlazhanovich. By press time, a search on the international web has not yielded anything on the named persons.Last evening, police said that in collaboration with other security agencies vigilance has been stepped up to avert the terrorists’ evil plans. Police have in the past issu...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...