Skip to main content

Simba matumaini kibao : yasaka ushindi sasa.

Kocha mkuu wa timu ya Simba, Mzambia Patrick Phiri, amesema kikosi chake kina ari ya juu ya ushindi na kitashuka uwanjani kuwakabili wapinzani wao Prisons katika mechi ya Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara Jumamosi kwa tahadhari ili waweze kupata pointi tatu muhimu.
Simba iliondoka jijini Dar es Salaam jana asubuhi na jioni iliwasili salama Mbeya tayari kwa mchezo huo utakaofanyika kwenye Uwanja wa Sokoine.
Phiri aliliambia gazeti hili kwamba kila timu inapokuwa kwenye Uwanja wa nyumbani hujiamini zaidi lakini wao wamejipanga kukabiliana na ushindani kutoka kwa wenyeji wao Prisons.
Kocha huyo alisema ligi ya Bara msimu huu ni ngumu na ushindi unaweza kupatikana ugenini au nyumbani.
"Ligi ina ushindani na changamoto, lakini pia hakuna mwenye uhakika wa kushinda nyumbani, hata ugenini timu inaweza kushinda, hicho ndicho ninachokiamini mimi, soka limebadilika," alisema Phiri.
Aliongeza kuwa, kikosi chake kinatarajia kuanza mazoezi leo asubuhi na jioni wataendelea kujinoa ili kujiweka tayari kuwakabili wenyeji.
Naye Rais wa Simba, Evans Aveva, alisema wameamua kwenda mapema Mbeya ili kutoa nafasi ya wachezaji kupumzika na hatimaye kuendelea na mazoezi kwa muda wa siku mbili.
Aveva alisema kuwa wanaamini mazoezi waliyofanya katika kambi ya Afrika Kusini itawasaidia
kuendelea kuonyesha kiwango cha juu na hatimaye 'kuzoa' pointi tatu za kwanza msimu huu."Timu imeshaenda Mbeya, tunaamini mambo yatakuwa mazuri huko ingawa hakuna timu ya kuidharau kwenye ligi hii," alisema Aveva.
Rais huyo aliongeza kuwa huenda timu hiyo ikacheza mechi ya 'ndondo' mkoani Iringa mara baada ya kumaliza mchezo huo Jumamosi.
Baada ya mechi ya Jumamosi, Simba itacheza mechi nyingine ugenini dhidi ya Mtibwa Sugar itakayofanyika Novemba Mosi kwenye Uwanja wa Jamhuri mkoani Morogoro.
Wekundu wa Msimbazi wamecheza mechi nne na wana pointi nne mkononi wakati vinara wa ligi hiyo ni mabingwa watetezi, Azam ambao wana pointi 10 sawa na Mtibwa Sugar.
Kipa chipukizi, Peter Manyika 'Junior' anatarajiwa kusimama tena langoni katika mechi hiyo kutokana na makipa wengine, Ivo Mapunda na Hussein 'Casillas' kuwa majeruhi.
CHANZO: NIPASHE

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.