Skip to main content

Serikali yafuta Mafunzo ya Ualimu ngazi ya Cheti


Serikali imefuta mafunzo ya ualimu ngazi ya cheti kuanzia mwaka huu ili kuboresha kiwango cha elimu nchini.
Tamko hilo limetolewa jana na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dkt.Shukuru Kawambwa wakati akizungumza na wanafunzi wa Chuo cha Ualimu Tabora, kilichoko Manispaa ya Tabora.
Alisema kuanzia mwaka huu, Serikali imeyafuta mafunzo hayo ikiwa ni mkakati maalumu wa kuboresha kiwango cha elimu ambapo walimu ambao wataajiri wakufundisha shule za msingi na sekondari, watatakiwa kuwa na elimu ya kiwango cha diploma na kuendelea.
Aliongeza kuwa, kuanzia sasa Wizara yake inataka kusimamia ubora wa elimu na walimu ambao kuanzia mwaka huu, wale ambao wataajiriwa kufundisha katika shule za msingi na sekondari, lazima wawe na elimu ya kiwango cha diploma na wasiofikia kiwango hicho, watapewa fursa ya kujiendeleza bila tatizo.
“Walimu wa shule za msingi na sekondari na wahitimu wa kidato cha sita waliopata daraja la 1-3 na kuchaguliwa kujiunga na kozi maalumu ya ualimu ngazi ya cheti, watapelekwa vyuoni kupata masomo ya diploma katika vyuo maalumu vilivyoandaliwa.
“Ili kuhakikisha mpango huu unatekelezwa, Wizara inaandaa waraka maalumu wamaelekezo ambao utatumwa kwa Wakurugenzi wa Halmashauri zote nchini,” alisema Dkt. Kawambwa.
Awali, akijibu swali la mwanafunzi wa chuo hicho aliyetaka kujua kwanini muda wakufanya mazoezi kwa vitendo (BTP) umepunguzwa na kuwa wiki tatu badala ya siku 60, Dkt. Kawambwa alisema utaratibu huo ni wa dharura kutokana na uhaba wa fedha.
Alisema Serikali itajitahidi kurekebisha hali hiyo kadri hali ya kifedha itakavyoruhusu ambapo akizungumzia ombi la kuongezwa posho kutoka sh. 4,500 wanazolipwa sasa hadi sh.7,500 ambazo wanalipwa wanafunzi wa ngazi ya Shahada, aliahidi kulifanyia kazi suala hilo katika Bajeti ya Wizara.
“Nawaomba wanafunzi wote wa vyuo vya ualimu, kuhakikisha mnafaulu masomo yote mnayofundishwa chuoni ili muweze kuajiriwa serikalini vinginevyo mtakaa benchi,” alisema.
Dkt.Kawambwa alisema wakati anaingia katika Wizara hiyo, alisema hataajiri walimu waliofeli, hivyo ataendelea na msimamo huo kwa nia njema, hivyo wanafunzi waliopo shuleni wanapaswa kufaulu masomo yao na ya ziada ili waweze kuajiriwa.
Chanzo: Majira.

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.