Skip to main content

BAADA YA SIMBA JANA KUTOLEWA NISHAI NA MBEYA CITY, LEO NI YANGA NA AZAM



KIUNGO Amri Kiemba wa Simba akiwatoka mabeki wa Mbeya City wakati timu hizo zilipomenyana jana kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. (Picha kwa hisani ya Bin Zubeiry Blog)
VIJANA wa Mbeya City jana walidhihirisha kwamba hawakupanda daraja la ligi kuu kwa kubahatisha baada ya kuilazimisha Simba kutoka nayo sare ya mabao 2-2 katika mechi iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Simba itabidi ijilaumu kwa kushindwa kutoka uwanjani na ushindi kwani ilikuwa mbele kwa mabao 2-1 hadi mapumziko, kabla ya vijana wa Mbeya City kuchachamaa na kusawazisha kipindi cha pili.

Kwa matokeo hayo, Simba bado inaongoza ligi hiyo ikiwa na pointi 11 baada ya kucheza mechi tano wakati Mbeya City imefikisha pointi saba.

Mshambuliaji Hamisi Tambwe kutoka Burundi aliendelea kung'ara na kuongoza kwa ufungaji mabao baada ya kuifungia Simba mabao yote mawili. Alifunga mabao hayo dakika ya 29 na 33.

Mbeya City, inayofundishwa na kocha mzoefu, Juma Mwambusi, ilipata bao la kwanza dakika ya 37 kupitia kwa Paul Nonga kabla ya Richard Peter kusawazisha dakika ya 69 na kuwaacha mashabiki wa Simba wakiwa wameduwaa.

Katika mechi hiyo iliyokuwa na ushindani mkali, mabao ya Mbeya City yalionekana kuwa ya ufundi zaidi, hasa bao la pili, ambalo lilifungwa kwa mpira wa adhabu, ambao Richard alitanguliziwa kwa mbele na kuunganisha kwa shuti.

SimbaAbbel Dhaira , William Lucian ‘Gallas’, Issa Rashid ‘Baba Ubaya’, Kaze Gilbert/Hassan Hatibu dk66, Joseph Owino, Jonas Mkude, Twaha Ibrahim/Ramadhani Chombo ‘Redondo’ dk50, Amri Kiemba/Ramadhani Singano ‘Messi’ dk79, Betram Mombeki, Amisi Tambwe na Haroun Chanongo.

Mbeya City:Dvid Burhan, John Kabanda, Hassan Mwasapili, Deogratius Julius, Antony Matogolo, Yohana Morris, Mwagane Yeya/Richard Peter dk59, Steven Mazanda, Paul Nonga, Deus Kaseke na Yussuf Willson.

Katika mechi zingine za ligi hiyo zilizochezwa jana, Mgambo JKT ilitoka sare ya bao 1-1 na Rhino Rangers mjini Tanga, Prisons ilitoka sare ya bao 1-1 na Mtibwa Sugar mjini Mbeya wakati Kagera Sugar iliibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Ashanti.

Ligi hiyo inatarajiwa kuendelea leo wakati Azam itakapomenyana na Yanga kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, JKT Ruvu itacheza na JKT Oljoro kwenye uwanja wa Azam Complex wakati Ruvu Shooting itavaana na Coastal Union kwenye Uwanja wa Mkwakwani mjini Tanga.

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them ...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Mwana muziki Marufu kwa jina la Chuck Brown Afariki Dunia Akiwa na umri wa miaka 75

View Photo Gallery — Chuck Brown dies at 75: The “godfather of go-go” has died By Chris Richards, Updated: Wednesday, May 16, 4:42 PM Chuck Brown, the gravelly voiced bandleader who capitalized on funk’s percussive pulse to create go-go, the genre of music that has soundtracked life in black Washington for more than three decades, died May 16 at the Johns Hopkins University hospital in Baltimore. He was 75. The death, from complications from sepsis, was confirmed by his manager, Tom Goldfogle. Mr. Brown had been hospitalized for pneumonia. Known as the “Godfather of Go-Go,” the performer, singer, guitarist and songwriter developed his commanding brand of funk in the mid-1970s to compete with the dominance of disco. Like a DJ blending records, Mr. Brown used nonstop percussion to stitch songs together and keep the crowd on the dance floor, resulting in marathon performances that went deep into the night. Mr. Brown said the style got its name because “the music j...