Skip to main content

Wanajeshi 800 wastaafishwa nchini Rwanda



Baadhi ya wanajeshi wa Rwanda waliokuwa CAR wakiabiri ndege January 16, 2014Haki miliki ya pichaAFP
Image captionWanajeshi wa Rwanda hulinda amani katika nchi kadha Afrika
Askari jeshi zaidi ya 800 wakiwemo baadhi ya maafisa wakuu katika jeshi la Rwanda wamestaafishwa.
Miongoni mwa waliostaafishwa ni majenerali wawili waliowahi kuongoza idara za upelelezi za nchi hiyo, Jenerali Karenzi Karake na Jenerali Jack Nziza.
Mwaka uliopita majenerali hao walibadilishiwa nyadhifa walizokuwa nazo jeshini, hatua ambayo kwa baadhi waliifasiri kuwa kama kushushwa ngazi.
Kulingana na wizara ya ulinzi ya Rwanda baadhi ya waliostaafishwa wamekamilisha mikataba yao jeshini na wengine ni kutokana na sababu za ugonjwa.
Mwandishi wa BBC aliyepo Kigali Yves Bucyana anasema kwa jumla maafisa waliostaafishwa ni 817.
Luteni jenerali Karenzi Karake kwa muda mrefu aliongoza idara ya upelelezi ya Rwanda na nje ya mipaka ya nchi hii akawa naibu kamanda wa kikosi cha umoja wa mataifa cha kulinda amani katika jimbo la Darfur nchini Sudan.
Naye Brigedia jenerali Jacques Nziza alishika nyadhifa mbali mbali katika wizara ya ulinzi ukiwemo wadhifa wa mkuu wa vitengo vya upelelezi.
Mwaka 2015 akiwa mkuu wa upelelezi, jenerali Karenzi alikamatwa mjini London kufuatia waranti ya kimataifa iliyotolewa na nchi ya Uhispania ikimhusisha yeye na maafisa wengine wa jeshi la Rwanda kwa makosa ya uhalifu wa kivita nchini Rwanda na jamuhuri ya kidemokrasia ya Congo.
Hata hivyo, baada ya pilka pilka za kidiplomasia Uingereza ilimwachia huru kwa kile ambachoJaji alisema sheria za nchi hizo mbili hazilingani.
Pamoja na hayo, mageuzi ya mwaka uliopita ndani ya jeshi ambapo majenerali hao walibadilishiwa nyadhifa, kwa baadhi yalitafsiriwa kama kushushwa ngazi.
Jenerali Karenzi aliachishwa kazi ya mkuu wa upelelezi na kutangazwa kama mshauri wa rais wa masuala ya kijeshi huku Jacques Nziza akapewa wadhifa wa kuongoza kitengo cha kuratibu shughuli za jeshi na wananchi.
Tangazo la wizara ya ulinzi ya Rwanda, pamoja na kuonyesha picha za karamu iliyoandaliwa kwa ajili ya waliostaafishwa, limeelezea tu kwamba miongoni mwa askari hao, zaidi ya 300 walikuwa mchanganyiko wa maafisa wakuu na maafisa wa dogo, na kwamba baadhi walihitimisha mikataba yao na jeshi la RDF huku wengine 70 wakistaafishwa kwa sababu ya ugonjwa.Source BBC.

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them ...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Mwana muziki Marufu kwa jina la Chuck Brown Afariki Dunia Akiwa na umri wa miaka 75

View Photo Gallery — Chuck Brown dies at 75: The “godfather of go-go” has died By Chris Richards, Updated: Wednesday, May 16, 4:42 PM Chuck Brown, the gravelly voiced bandleader who capitalized on funk’s percussive pulse to create go-go, the genre of music that has soundtracked life in black Washington for more than three decades, died May 16 at the Johns Hopkins University hospital in Baltimore. He was 75. The death, from complications from sepsis, was confirmed by his manager, Tom Goldfogle. Mr. Brown had been hospitalized for pneumonia. Known as the “Godfather of Go-Go,” the performer, singer, guitarist and songwriter developed his commanding brand of funk in the mid-1970s to compete with the dominance of disco. Like a DJ blending records, Mr. Brown used nonstop percussion to stitch songs together and keep the crowd on the dance floor, resulting in marathon performances that went deep into the night. Mr. Brown said the style got its name because “the music j...