Skip to main content

Wanajeshi 800 wastaafishwa nchini Rwanda



Baadhi ya wanajeshi wa Rwanda waliokuwa CAR wakiabiri ndege January 16, 2014Haki miliki ya pichaAFP
Image captionWanajeshi wa Rwanda hulinda amani katika nchi kadha Afrika
Askari jeshi zaidi ya 800 wakiwemo baadhi ya maafisa wakuu katika jeshi la Rwanda wamestaafishwa.
Miongoni mwa waliostaafishwa ni majenerali wawili waliowahi kuongoza idara za upelelezi za nchi hiyo, Jenerali Karenzi Karake na Jenerali Jack Nziza.
Mwaka uliopita majenerali hao walibadilishiwa nyadhifa walizokuwa nazo jeshini, hatua ambayo kwa baadhi waliifasiri kuwa kama kushushwa ngazi.
Kulingana na wizara ya ulinzi ya Rwanda baadhi ya waliostaafishwa wamekamilisha mikataba yao jeshini na wengine ni kutokana na sababu za ugonjwa.
Mwandishi wa BBC aliyepo Kigali Yves Bucyana anasema kwa jumla maafisa waliostaafishwa ni 817.
Luteni jenerali Karenzi Karake kwa muda mrefu aliongoza idara ya upelelezi ya Rwanda na nje ya mipaka ya nchi hii akawa naibu kamanda wa kikosi cha umoja wa mataifa cha kulinda amani katika jimbo la Darfur nchini Sudan.
Naye Brigedia jenerali Jacques Nziza alishika nyadhifa mbali mbali katika wizara ya ulinzi ukiwemo wadhifa wa mkuu wa vitengo vya upelelezi.
Mwaka 2015 akiwa mkuu wa upelelezi, jenerali Karenzi alikamatwa mjini London kufuatia waranti ya kimataifa iliyotolewa na nchi ya Uhispania ikimhusisha yeye na maafisa wengine wa jeshi la Rwanda kwa makosa ya uhalifu wa kivita nchini Rwanda na jamuhuri ya kidemokrasia ya Congo.
Hata hivyo, baada ya pilka pilka za kidiplomasia Uingereza ilimwachia huru kwa kile ambachoJaji alisema sheria za nchi hizo mbili hazilingani.
Pamoja na hayo, mageuzi ya mwaka uliopita ndani ya jeshi ambapo majenerali hao walibadilishiwa nyadhifa, kwa baadhi yalitafsiriwa kama kushushwa ngazi.
Jenerali Karenzi aliachishwa kazi ya mkuu wa upelelezi na kutangazwa kama mshauri wa rais wa masuala ya kijeshi huku Jacques Nziza akapewa wadhifa wa kuongoza kitengo cha kuratibu shughuli za jeshi na wananchi.
Tangazo la wizara ya ulinzi ya Rwanda, pamoja na kuonyesha picha za karamu iliyoandaliwa kwa ajili ya waliostaafishwa, limeelezea tu kwamba miongoni mwa askari hao, zaidi ya 300 walikuwa mchanganyiko wa maafisa wakuu na maafisa wa dogo, na kwamba baadhi walihitimisha mikataba yao na jeshi la RDF huku wengine 70 wakistaafishwa kwa sababu ya ugonjwa.Source BBC.

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.