Skip to main content

SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR YAILILIA AMREF


Na Carlos Nichombe

Waziri wa Afya wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mahmoud Thabit Kombo ameliombaShirika la Utafiti wa Tiba na Afya barani Afrika (AMREF) kujenga ofisi Visiwani Zanzibar ili kuisaidia Serikali katika kupambana na tatizo la vifo vya mama na mtoto.
Kombo aliyasema hayo jana Jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na wadau mbambali wa Masuala ya Afya waliojitokeza katika maadhimisho ya miaka 60 ya uanzishwaji wa Shirika la AMREF.
Alisema AMREF wamekuwa na mchango mkubwa nchini Tanzania hususani katika ukomeshaji vitendo vya ukeketaji kwa wanawake katika maeneo mbalimbali hivyo kuwaomba waigeukie na Zanzibar kwa ajili ya utatuzi wa masuala mbalimbali yanayowasumbua.
Alieleza kuwa jukumu la kutokomeza vifo vya mama na mtoto ni la jamii yote hivyo kama shirika hilo litajenga ofisi zao visiwani Zanzibar litaongeza nguvu kwa Serikali ambayo 
imekuwa ikitafuta wadau mbalimbali katika kutatua matatizo hayo.

“Najua mmefanya juhudi nyingi ambazo kila mwenye macho ameziona na mie naomba niwaeleze kilio chetu kama Wazanzibar mje mjenge ofisi na kule kwetu kwa sababu 
tunatambua mtakuwa mnaanzisha program mbalimbali ambazo zitasaidia kuondoa tatizo hili linalosumbua sana visiwa vya Zanzibar,” alidai Kombo.

Akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu Kombo alisema AMREF imekuwa ni msaada mkubwa kwa Taifa la Tanzania kwani imekuwa ikiendesha na kuanzisha program mbalimbali ambazo zimesaidia kupunguza uhaba wa wataalamu wa afya.
“Nataka niwaambie kwamba Serikali inatambua mchango wenu na tupo tayari kushirikiana nanyi kwa lolote lile ili mradi mboreshe zaidi huduma za afya ambazo mnazitoa kwa watanzania”
“Lakini pia naomba watanzania watambue kwamba hili Shirika limekuwa msaada mkubwa sana kwetu kwenye masuala ya afya kwani wametusaidia kuingia katika maeneo ya pembezoni zaidi mwa nchi yetu hususani vijijini ambako kulikuwa kumesahaulika kwa kipindi kirefu,” alisema
Kombo.

Kwa upande wake Mkurugenzi mkazi wa shirika hilo,dkt. florence Temu alisema wataendelea kutoa huuduma mbalimbali za Afya nchini ikiwemo utoaji wa elimu ya madhara ya ukeketaji kwa jamii hususani Mangariba, wazee wa vijiji pamoja na wanawake wanaoishi katika maeneo 
ambayo yamekithiri zaidi kwa vitendo hivyo.

Alidai kuwa wamepata mafanikio makubwa ya kupambana na tatizo la ukeketaji pamoja na kupambana na ugonjwa wa Fistula kwani watu wengi wamekuwa na uelewa wa masuala 
hayo ambayo yalikuwa yanaisumbua zaidi Serikali.

“Ili kufanikiwa katika suala hili ni lazima tuishirikishe sana jamii ,kwani tusipofanya hivi tutakua tunakaribisha matatizoyanayowapata wasichana wanaofanyiwa ukeketeji ikiwemo kumwaga damu pamoja na kupewa ndoa za mapema”alisema Florence

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.