Skip to main content

TWIGA STARS KUJIPIMA KWA ZIMBABWE

Release No. 069
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Mei 8, 2012
 
TWIGA STARS KUJIPIMA KWA ZIMBABWE
Timu ya Taifa ya wanawake (Twiga Stars) itacheza na Zimbabwe katika mchezo wa kirafiki utakaofanyika Mei 12 mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
 
Twiga Stars hivi iko katika ziara ya mechi za kirafiki katika mikoa ya Dodoma na Mwanza. Leo (Mei 8 mwaka huu) itacheza na kombaini ya Mkoa wa Dodoma ya vijana wenye umri chini ya miaka 17 katika mchezo utakaofanyika Uwanja wa Jamhuri, mjini Dodoma.
 
Kesho (Mei 9 mwaka huu) itaondoka kwenda jijini Mwanza ambapo pia itacheza mechi moja ya kirafiki Mei 10 mwaka huu kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, na kurejea Dar es Salaam tayari kwa ajili ya mechi dhidi ya Zimbabwe.
 
Zimbabwe inatarajia kuwasili kesho (Mei 9 mwaka huu) jioni kwa ndege ya South African Airways (SAA) ikiwa na msafara wa 25 na wataondoka Mei 14 mwaka huu alfajiri.
 
KAMATI YA MASHINDANO KUPANGA VITUO LIGI YA TAIFA
Kamati ya Mashindano ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) inatarajia kukutana leo (Mei 8 mwaka huu) ambapo pamoja na mambo mengine itapanga vituo vya Ligi ya Taifa na tarehe ya kuanza ligi hiyo.
 
Mikoa nane imeomba kuwa wenyeji wa ligi hiyo itakayochezwa katika vituo vitatu. Mikoa hiyo kupitia kwenye vyama vyao vya mpira wa miguu ni  
Mikoa iliyoomba vituo ni Dar es Salaam, Kigoma, Kilimanjaro, Lindi, Mara, Mbeya, Shinyanga na Singida.
 
Timu zinazoshiriki ligi hiyo ni mabingwa wa mikoa. Timu hizo ni Ashanti United ya Ilala (Dar es Salaam), Aston Villa (Singida), Bandari FC (Kagera), CDA (Dodoma), Flamingo SC (Arusha), Forest FC ya Siha (Kilimanjaro), JKT Kanembwa (Kigoma), Korogwe United ya Korogwe (Tanga), Kurugenzi ya Mafinga (Iringa), Lindi SC (Lindi) na Majimaji (Tabora).
 
Mighty Elephant (Ruvuma), Mkamba Rangers ya Kilombero (Morogoro), Mpanda Stars ya Mpanda (Rukwa), Mwadui FC (Shinyanga), Nangwa VTC (Manyara), Ndanda FC (Mtwara), Pamba SC (Mwanza), Polisi Mara (Mara), Red Coast ya Kinondoni (Dar es Salaam), Super Star ya Bagamoyo (Pwani), Tenende SC (Mbeya) na Tessema FC ya Temeke (Dar es Salaam).
 
KILA LA KHERI SIMBA, PONGEZI
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linaitakia kila la kheri timu ya Simba kwenye mechi yake ya marudiano ya Kombe la Shirikisho dhidi ya Al Ahly Shandy ya Sudan itakayochezwa Jumapili (Mei 13 mwaka huu).
 
Mechi hiyo itachezwa katika mji wa Shandy kuanzia saa 2 kamili usiku kwa saa za Afrika Mashariki. Simba inaondoka kesho kwenda huko kwa ndege ya Kenya Airways.
 
Msafara wa timu hiyo utaongozwa na Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya TFF, Hussein Mwamba, na unatarajia kurejea nyumbani Mei 15 mwaka huu.
 
Pia TFF inaipongeza Simba kwa kufanikiwa kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) ambayo Mei 6 mwaka huu ilifunga msimu wa 2011/2012.
 
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
 

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.