Skip to main content

MBUNGE WA CHAMA TAWALA NCHINI MAREKANI AHAMASISHA UANZISHWAJI WA KAMATI NDOGO (CAUCUS) YA WABUNGE KUISEMEA TANZANIA


Balozi wa Tanzania nchini Marekani na Mexico, Mhe. Mwanaidi Sinare Maajar akiwa na Mhe. Dan Boren, Mbunge wa Bunge la Marekani kutoka Oklahoma,aliyemtembelea ofisini kwakwe.
Mhe.Balozi Maajar akiwa katika picha ya pamoja na Mbunge Dan Boren,Mkurugenzi wa Bunge, Bi.Hilary Moffett,na kushoto na kulia na Bibi Lily Munanka Mkuu wa Utawala Ubalozini na Afisa Ubalozi Bw. Suleiman Saleh.

Balozi wa Tanzania nchini Marekani na Mexico, Mhe. Mwanaidi Sinare Maajar,Jumatano Mei 9, 2012 alimpokea Ubalozini, Mhe. Dan Boren na kufanya naye mazungumzo ya uanzishwaji wa Tanzania Caucus katika Bunge la Marekani ambapo Tanzania itakuwa imepata mtetezi na msemaji bungeni humo kila linapotokea jambo linalohusu Tanzania.

Mhe. Boren ni mbunge wa Bunge la Marekani kutoka Wilaya ya Pili, Jimbo la Oklahoma, amehamasisha na hatimaye kuanzisha kundi la wabunge wenye mapenzi na Tanzania, kamati ndogo (caucus) ya kuisemea Tanzania kwenye Bunge la Marekani.

Mhe. Boren ambaye ni mbunge kutoka Chama Tawala cha Democrat ameasisi Kundi hilo hilo akishirikiana na wabunge wenzake kadhaa wa chama chake na wengine kutoka Chama cha Republican kutokana na kufurahishwa kwao na juhudi za Serikali ya Mhe. Rais Jakaya Mrisho Kikwete katika kuimarisha demokrasia, utawala bora pamoja na juhudi za kimaendeleo katika sekta za uchumi, nishati, kilimo na hifadhi ya mazingira.

Katika ziara yake hapa ubalozini Mhe. Boren aliyeambatana na Bi. Hilary Moffett, Mkurugenzi wa Sheria Bungeni, alimhakikishia Mhe. Balozi Maajar utayari wake wa kuisaidia Tanzania katika juhudi zake hizo.

Aidha alibainisha kwamba Tanzania ina changamoto nyingi sana mbele yake na hivyo kuwepo kwa sauti mpya ya kuisemea katika Bunge la Marekani ni jambo ambalo analiona litakuwa na manufaa makubwa kwa nchi.

Sambamba na hilo, Mhe. Boren alibainisha kwamba Tanzania imekuwa ni moja ya nchi ambazo Serikali ya Marekani inaziangalia kwa umakini kama mfano wa nchi bora na hivyo ameona ni vyema naye akaunga mkono juhudi hizo za Serikali ya Rais Barack Obama.

Kwa upande wake, Mhe.Balozi Mwanaidi Sinare Maajar alifurahishwa na kufarijika na ujio wa Mhe. Boren Ubalozini na kumueleza kwamba atashirikiana naye bega kwa bega na kuahidi kwamba muda wowote atakapohitajika kukutana na kamati hiyo ya Bw. Boren yupo tayari.

Mhe. Maajar alimshukuru Mhe.Boren kwa mwaliko wake kutembelea Jimbo la Oklahoma ili Tanzania ipate kueleweka zaidi na hivyo kufungua pazia la ushirikiano katika sekta mbali mbali za Uchumi, Kilimo, Nishati na Utalii

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.