Skip to main content

Mnyika Ashinda Kesi


Kesi hiyo namba 107 ya 2010, ilifunguliwa na aliyekuwa mgombea wa CCM, Hawa Ngh’umbi dhidi ya Mnyika ambaye ni mdaiwa wa pili katika kesi hiyo akitetewa na Wakili Edson Mbogoro.

Mdaiwa wa kwanza katika kesi hiyo iliyoko mbele ya Jaji Upendo Msuya ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) na aliyekuwa Msimamizi wa Uchaguzi (RO) katika jimbo hilo, (aliyekuwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni) ambao walikuwa wakitetewa na Wakili Mkuu wa Serikali (PSA), Justice Mulokozi.

Katika uchaguzi huo, uliofanyika Oktoba 31, 2010, Msimamizi wa Uchaguzi, Raphael Ndunguru alimtangaza Mnyika kuwa mshindi Novemba 2, 2010 baada ya kupata kura 66,742. Ngh’umbi alipata kura 50,544.

Hata hivyo, Ngh'umbi hakuridhishwa na matokeo hayo akaamua kufungua kesi Mahakama Kuu kuyapinga, akimtumia Wakili Issa Maige.

Katika hati yake ya madai na wakati akitoa ushahidi  mahakamani, Ngh’umbi na mashahidi wake walidai kuwa kulikuwa na ukiukwaji mkubwa wa taratibu na kisheria katika ujumlishaji wa kura na utangazaji wa matokeo ambao umeathiri matokeo hayo.

Hoja za kuzingatia
Katika hukumu ya leo, Jaji Msuya atazingatia hoja tano ambazo zinatokana na madai katika hati ya Ngh’umbi alizozitoa wakati akitoa ushahidi wake mahakamani pamoja na mashahidi wake wawili, kuhusu ukiukwaji huo wa sheria.

Hoja hizo zitakazozingatiwa katika hukumu ya Jaji Msuya ni pamoja na kama mkanganyiko wa takwimu za kura katika Fomu namba 24B (Fomu za matokeo ya jumla ya ubunge), zimeathiri matokeo hayo ya uchaguzi mzima.

Hoja nyingine ni kama mlalamikiwa wa pili (Mnyika), aliingia na kompyuta (laptop) tano katika chumba cha majumuisho ya kura na kama ndizo zilizotumiwa na wasimamizi wa uchaguzi kuhesabu na kujumlishia kura.

Nyingine ni kama marekebisho ya kura katika baadhi ya fomu namba 21B, (Fomu za matokeo ya kura za ubunge vituoni), yalifanyika katika chumba cha majumuisho na mlalamikiwa Mnyika kuingia na kundi la wafuasi wake katika chuma cha majumuisho kinyume cha sheria.

Hoja nyingine ni kama mlalamikiwa wa pili (Mnyika) alitoa kauli za kashfa dhidi ya mlalamikaji (Ngh’umbi) kwa kumuita fisadi, akimtuhumu kuuza jengo la Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT).
Wakati akitoa ushahidi wake mahakamani, Ngh’umbi alidai kuwa matokeo hayo siyo sahihi kwa sababu pamoja na mambo mengine, katika fomu ya matokeo yaliyotangazwa kuna kura 14,854, zisizojulikana mahali zilikotoka ambazo upande wa mashtaka unadai ni kura hewa.

Alisema kwa mujibu wa fomu hiyo, kura halisi zilikuwa ni 119,823, kura halali zilikuwa ni 117,639 huku kura zilizokataliwa (zilizoharibika) zikiwa ni 2,184.
Lakini alidai kuwa ukijumlisha kura zake na za Mnyika wote kwa pamoja kisha zikitolewa kutoka katika kura halali zilizopigwa, zinabaki kura 353 ambazo ndizo zitagawanywa kwa wagombea wengine 14, jambo ambalo alisema si sahihi.

Hata hivyo, wakati akijitetea, Mnyika alikanusha madai hayo yote licha ya kukiri kuwepo kwa mkanganyiko wa usahihi na uwiano wa kura katika Fomu namba 24B.
Lakini, bado alidai kuwa dosari hiyo zinaweza kurekebishwa na kwamba haziathiri matokeo kiasi cha kuyafanya yawe batili.
Shahidi wa kwanza upande wa wadaiwa (DW1), aliyekuwa Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi, Gaudence Kadiarara alikiri kuwa Mnyika aliingiza kompyuta hizo japo alidai kuwa hata hivyo, hawakuzitumia, tofauti na Mnyika ambaye alidai hakuingia na kompyuta yoyote.

Shahidi huyo na mashahidi wengine wa utetezi akiwemo Msimamizi wa Uchaguzi (Mkurugenzi wa Manispaa), pia walikiri kuwepo kwa mkanganyiko katika fomu ya matokeo hayo ya ubunge lakini, wakasisitiza kuwa dosari hizo haziathiri matokeo jumla.

Hoja hizo ndizo ambazo ama zitamshawishi Jaji Msuya katika hukumu yake kutengua matokeo ya ubunge huo au kuthibitisha kwamba matokeo hayo ni halali.

Mawakili wa utetezi, PSA Mulokozi kwa niaba ya AG na RO na Mbogoro kwa niaba ya Mnyika, walidai kuwa mlalamikaji ameshindwa kuthibitisha madai yake na hivyo kuiomba mahakama iyatupilie mbali.

Lakini, Wakili Maige anayemtetea Ngh’umbi alisema wamethibitisha madai yao kwa kiwango kinachohitajika kisheria na kuiomba Mahakama itengue matokeo hayo yaliyompa ushindi Mnyika.

Alisema madai mengine yameungwa mkono na mashahidi wa utetezi hususan DW1 aliyekiri Mnyika kuingia na kompyuta katika chumba cha majumuisho ingawa alikanusha kuzitumia tofauti na Mnyika aliyekana kuingiza kompyuta hizo katika chuma hicho.
Pia Wakili Maige alihoji sababu ya mawakili wa Serikali kutowaita mahakamani baadhi ya mashahidi ambao walitajwa na upande wa madai na wa wadaiwa kuhusika kwa namna moja au nyingine katika mchakato wa uchaguzi huo.

Wakili Maige aliwataja mashahidi hao ambao alidai walikuwa ni muhimu kuitwa mahakamani kujibu madai na kutoa ufafanuzi wa masuala yaliyowagusa kuwa ni pamoja na Mkurugenzi wa Uchaguzi na Mtaalamu wa Teknolojia ya Mawasiliano wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec).

Mkurugenzi huyo alidaiwa kuwa ndiye aliyekagua kompyuta zilizotumika kufanyia majumuisho ya kura ambazo zilidaiwa kuwa zilitoka Manispaa ya Kinondoni, baada ya mfumo wa awali ulioandaliwa na Nec kuonekana kuwa haufai.

Lakini, Wakili Maige alidai kuwa kitendo cha kushindwa kumuita mkurugenzi huyo wa Nec mahakamani kutoa maelezo ya ukaguzi alioufanya na mbinu alizozitumia kuithibitishia mahakama kuwa katika kompyuta hizo zisingewezekana kuingizwa taarifa za kughushi ni kinyume cha sheria.

Akirejea kesi ya Stanbic Bank (T) Ltd dhidi ya Woods (T) Ltd namba 48 ya mwaka 2002, alidai kuwa Mahakama ilishatoa mwongozo kuwa ushahidi wa kitaalamu hauwezi kuthibitishwa kwa maneno matupu mpaka mtaalamu huyo atakapoitwa kuutolea ufafanuzi.

Wakili Maige alidai kuwa upande wa madai umethibitisha kuwa kompyuta zisizostahili kisheria ndizo zilizotumika kufanya majumuisho na kwamba ndizo zilizosababisha kuwepo kwa mkanganyiko uliojitokeza katika fomu ya matokeo wa kura zaidi 14,000, zisizo na maelezo.Inatoka Mjengwa Blogspot.com

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...