Skip to main content

Watanzania wataka nchi ikumbukwe duniani

as_03af5.jpg
Washington. Ujumbe wa Tanzania katika mikutano muhimu inayofanyika Marekani wameipigia debe nchi yao wakitaka ikumbukwe.
Katika mkutano wa 45 wa Kamisheni ya Takwimu ya Umoja wa Mataifa (UN) na mkutano wa wazi wa tisa wa kikosi kazi kuhusu mapendekezo ya ajenda za malengo mpya ya maendeleo endelevu baada ya 2015 (SDGs), wamekuwa wakitetea masilahi ya nchi kwa kushiriki na kuchangia majadiliano ya mada mbalimbali zinazohusiana na mikutano hiyo
.
Akichangia katika mada iliyohusu Technolojia ya Habari na Mawasiliano (ICT), Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu, Dk. Albina Chuwa alisema mwaka hadi mwaka Tanzania na Afrika imeendelea kupiga hatua katika teknolojia ya habari na mawasiliano licha ya changamoto mbalimbali.
Alizitaja baadhi ya changamoto hizo kuwa ni kutokuwapo kwa uratibu kati ya wazalishaji wa takwimu za ICT na watumiaji na kati ya wazalishaji na watoaji wa takwimu ambao ni chanzo muhimu cha taarifa.
Alisema tatizo hili kama halitarekebishwa, linaweza kusababisha uchapishaji usio sahihi wa takwimu kuhusu ICT, jambo ambalo linaweza kusababisha utoaji uamuzi wenye makosa.
Alisema uboreshaji na uratibu kati ya wazalishaji, wauzaji na watumiaji wa takwimu, utaepusha kujirudia kwa makosa yakiwamo ya matumizi ya rasilimali fedha na watu, rasilimali ambazo ni haba katika Afrika.
''Kipengele cha takwimu za ICT kinapaswa kuingizwa katika mikakati ya kitaifa kwa ajili ya maendeleo ya takwimu na katika mipango ya kazi ya kikanda, '' alisema.
Dk. Chuwa alisema ukusanywaji wa takwimu katika ngazi za kitaifa lazima uimarishwe kwa kuweka utaratibu kati ya taasisi husika pamoja na Ofisi za Taifa za Takwimu.
Kuhusu uwezeshaji, alisema Afrika inahitaji kuimarisha uwezo wake wa kutafuta rasilimali ndani ya Afrika ili hatimaye Afrika ijijengee uwezo wa kuboresha ukusanyaji, uchambuzi na usambazaji wa viashiria vya msingi vya ICT katika Afrika.
Alisema Tanzania ingependa kuona wataalamu walioandaa mfumo huo, wanakuja na mkakati wa utoaji mafunzo na uwezeshaji kwa nchi zinazoendelea ikiwamo Tanzania(E.L).source http://www.mjengwablog.com/

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them ...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Mwana muziki Marufu kwa jina la Chuck Brown Afariki Dunia Akiwa na umri wa miaka 75

View Photo Gallery — Chuck Brown dies at 75: The “godfather of go-go” has died By Chris Richards, Updated: Wednesday, May 16, 4:42 PM Chuck Brown, the gravelly voiced bandleader who capitalized on funk’s percussive pulse to create go-go, the genre of music that has soundtracked life in black Washington for more than three decades, died May 16 at the Johns Hopkins University hospital in Baltimore. He was 75. The death, from complications from sepsis, was confirmed by his manager, Tom Goldfogle. Mr. Brown had been hospitalized for pneumonia. Known as the “Godfather of Go-Go,” the performer, singer, guitarist and songwriter developed his commanding brand of funk in the mid-1970s to compete with the dominance of disco. Like a DJ blending records, Mr. Brown used nonstop percussion to stitch songs together and keep the crowd on the dance floor, resulting in marathon performances that went deep into the night. Mr. Brown said the style got its name because “the music j...