Skip to main content

Msome Okwi kuhusu Mbeya City



Na Emmanuel Ndege
MSHAMBULIAJI nyota wa klabu ya Yanga, Emmanuel Okwi, amesema anakunwa na kiwango cha juu cha soka kinachoonyeshwa na timu ya Mbeya City katika michuano ya ligi kuu ya Tanzania Bara.

Akizungumza na Burudani makao makuu ya klabu hiyo, mitaa ya Twiga na Jangwani, Dar es Salaam juzi, Okwi alisema Mbeya City imeleta changamoto mpya katika ligi kuu msimu huu.

Okwi alisema timu hiyo yenye makao makuu yake mjini Mbeya, haijayumba kisoka tangu ligi kuu ilipoanza na wachezaji wake wanacheza kwa kujiamini na bila kukata tamaa.

"Iwapo wataendelea hivi msimu ujao, haitakuwa ajabu kwa Mbeya City kutwaa ubingwa,"alisema mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Uganda.

Okwi amekiri kuwa, ligi ya msimu huu ni ngumu na yenye ushindani mkali na hakuna timu yenye uwezo wa kutangaza ubingwa mapema.

"Nimeichezea Simba kwa miaka zaidi ya miwili. Huko nyuma timu zilikuwa na uwezo wa kutangaza ubingwa zikiwa zimesalia mechi mbili au tatu, lakini msimu huu ni vigumu,"alisema Okwi.

"Yanga, Azam na Mbeya City kila moja ina uwezo wa kutwaa ubingwa, hali hii imesababisha kuwepo kwa ushindani mkali. Ni vigumu kutabiri bingwa mapema,"aliongeza.

Hata hivyo, Okwi alisema licha ya kuzidiwa kwa pointi na Azam, Yanga bado inayo nafasi kubwa ya kutwaa ubingwa wa ligi hiyo, iwapo wachezaji wake wataendelea kucheza kwa kujituma.

Alisema atahakikisha anasaidiana vyema na wachezaji wenzake kuiwakilisha vizuri timu hiyo ili itwae ubingwa na kupata nafasi nyingine ya kushiriki michuano ya klabu bingwa Afrika mwakani.

Akizungumzia jinamizi lililoikumba timu hiyo hivi karibuni la kupoteza penalti katika mechi muhimu, Okwi alisema, adhabu hiyo haina ufundi na kwamba mchezaji yeyote anaweza kupoteza.

"Penalti ni sawa na mchezo wa bahati nasibu, unaweza kupata au kukosa, hazina ufundi,"alisisitiza nyota huyo wa zamani wa Simba.

Wakati huo huo, klabu ya Yanga imesema, itakata rufani kwenye Mahakama ya Rufani Tanzania kupinga hukumu ya Makahama Kuu Divisheni ya Kazi ya kuitaka timu hiyo iwalipe wachezaji Wisdom Ndlovu na Stephen Marashi sh. milioni 106.

Katibu Mkuu wa Yanga, Ben Njovu, alisema mjini Dar es Salaam jana kuwa, wamepokea nakala ya hukumu ya kesi hiyo iliyofungiwa na wachezaji hao ya kupinga kukatishiwa mikataba yao.

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...