Skip to main content

SOMA JINSI NYOTA WA ARSENAL TESEKA KATIKA UHUSIANO WA Celia Kay

MWANAMITINDO AMPASUA KICHWA 



LONDON, England
HATIMAYE mshambuliaji, Olivier Giroud wa klabu ya Arsenal ameamua kuvunja ukimya kwa kujibu tuhuma za kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwanamitindo, Celia Kay.

Giroud anatuhumiwa kumpeleka Kay kwenye hoteli ya Four Seasons iliyoko Canary Wharf siku moja kabla ya Arsenal kuichapa Crystal Palace katika mechi ya ligi kuu ya England iliyochezwa Februari 2 mwaka huu.

Kocha Mkuu wa Arsenal, Arsene Wenger, hadi sasa hajaamua kuweka wazi kuhusu hatua zitakazochukuliwa kwa Giroud baada ya kukiri kufanya mapenzi na binti huyo wakati akiwa katika majukumu ya kuitumikia timu yake.

Wenger alikaririwa hivi karibuni akisema kuwa, suala la mchezaji huyo ni la ndani na litashughulikiwa na uongozi wa klabu.

"Hili ni suala la ndani, sitaki kulizungumza hadharani kwa sababu naheshimu maisha yake binafsi,"alisema Wenger.

Kay alimpiga picha Giroud alipokuwa kwenye chumba cha hoteli hiyo, akiwa amevaa chupi ya ndani na kuisambaza kwenye mitandao, ukiwemo mtandao wa MailOnline.

Awali Giroud, ambaye aliifungia Arsenal mabao mawili ilipoichapa Everton mabao 4-1 katika mechi ya Kombe la FA iliyochezwa wiki iliyopita, alitoa taarifa ya kuomba msamaha kwa mkewe, Jennifer na Wenger.

"Naomba radhi kwa mke wangu, familia yangu, marafiki, kocha, wachezaji wenzangu na mashabiki,"alisema Giroud.

"Napaswa kuipigania familia na klabu yangu na kuomba radhi kwao," alisema mshambuliaji huyo.

"Kuna mambo yaliyokuwa na ukweli, lakini mengine yalikuwa ya uongo. Lakini hayo yamepita kwa sasa,"alisema nyota huyo wa Arsenal, ambaye Juni mwaka jana mkewe alijifungua mtoto wa kiume.

"Kitu ambacho hakiwezi kuniua, kinanifanya niwe jasiri. Nashawishika kuamini kwamba, kina kinachotokea kwangu, kitanifanya niwe na nguvu zaidi,"aliongeza.

Giroud alisema anachopaswa kukifanya kwa sasa ni kuelekeza nguvu na akili yake uwanjani kwa kuitumikia vyema klabu yake na kutunza familia yake.

"Kilikuwa kipindi kigumu. Unapaswa kuwa na ujasiri kichwani kwako. Nilitumia mchezo wa soka kupambana na hili. Mchango wa Kocha Arsene Wenger ulikuwa muhimu. Nilizungumza naye.

"Nataka kusahau kuhusu hili kwa sasa na kuendelea na mambo mengine na kuanza upya,"alisisitiza.
Arsenal ilipanga kumtoza faini ya pauni 230,000 mchezaji huyo, lakini baadaye iliamua kumuunga mkono baada ya kukanusha tuhuma hizo. Wanasheria wa mchezaji huyo nao wameliandikia barua gazeti la Daily Mail kulilaumu kwa kuandika habari hizo.

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...