Skip to main content

SOMA JINSI NYOTA WA ARSENAL TESEKA KATIKA UHUSIANO WA Celia Kay

MWANAMITINDO AMPASUA KICHWA 



LONDON, England
HATIMAYE mshambuliaji, Olivier Giroud wa klabu ya Arsenal ameamua kuvunja ukimya kwa kujibu tuhuma za kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwanamitindo, Celia Kay.

Giroud anatuhumiwa kumpeleka Kay kwenye hoteli ya Four Seasons iliyoko Canary Wharf siku moja kabla ya Arsenal kuichapa Crystal Palace katika mechi ya ligi kuu ya England iliyochezwa Februari 2 mwaka huu.

Kocha Mkuu wa Arsenal, Arsene Wenger, hadi sasa hajaamua kuweka wazi kuhusu hatua zitakazochukuliwa kwa Giroud baada ya kukiri kufanya mapenzi na binti huyo wakati akiwa katika majukumu ya kuitumikia timu yake.

Wenger alikaririwa hivi karibuni akisema kuwa, suala la mchezaji huyo ni la ndani na litashughulikiwa na uongozi wa klabu.

"Hili ni suala la ndani, sitaki kulizungumza hadharani kwa sababu naheshimu maisha yake binafsi,"alisema Wenger.

Kay alimpiga picha Giroud alipokuwa kwenye chumba cha hoteli hiyo, akiwa amevaa chupi ya ndani na kuisambaza kwenye mitandao, ukiwemo mtandao wa MailOnline.

Awali Giroud, ambaye aliifungia Arsenal mabao mawili ilipoichapa Everton mabao 4-1 katika mechi ya Kombe la FA iliyochezwa wiki iliyopita, alitoa taarifa ya kuomba msamaha kwa mkewe, Jennifer na Wenger.

"Naomba radhi kwa mke wangu, familia yangu, marafiki, kocha, wachezaji wenzangu na mashabiki,"alisema Giroud.

"Napaswa kuipigania familia na klabu yangu na kuomba radhi kwao," alisema mshambuliaji huyo.

"Kuna mambo yaliyokuwa na ukweli, lakini mengine yalikuwa ya uongo. Lakini hayo yamepita kwa sasa,"alisema nyota huyo wa Arsenal, ambaye Juni mwaka jana mkewe alijifungua mtoto wa kiume.

"Kitu ambacho hakiwezi kuniua, kinanifanya niwe jasiri. Nashawishika kuamini kwamba, kina kinachotokea kwangu, kitanifanya niwe na nguvu zaidi,"aliongeza.

Giroud alisema anachopaswa kukifanya kwa sasa ni kuelekeza nguvu na akili yake uwanjani kwa kuitumikia vyema klabu yake na kutunza familia yake.

"Kilikuwa kipindi kigumu. Unapaswa kuwa na ujasiri kichwani kwako. Nilitumia mchezo wa soka kupambana na hili. Mchango wa Kocha Arsene Wenger ulikuwa muhimu. Nilizungumza naye.

"Nataka kusahau kuhusu hili kwa sasa na kuendelea na mambo mengine na kuanza upya,"alisisitiza.
Arsenal ilipanga kumtoza faini ya pauni 230,000 mchezaji huyo, lakini baadaye iliamua kumuunga mkono baada ya kukanusha tuhuma hizo. Wanasheria wa mchezaji huyo nao wameliandikia barua gazeti la Daily Mail kulilaumu kwa kuandika habari hizo.

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.