Skip to main content

TIC :YATANGAZA FURSA ZAIDI KWA WAWEKEZAJI WA NDANI NA NJE

KITUO cha Uwekezaji Tanzania (TIC) imesema kwa kushirikiana na Wizara ya mambo ya Nje 
na ushirikiano wa Afrika Mashariki,Taasisi sekta binafsi Tanzania (TPSF) na
Ubalozi wa Tanzania  nchini China iimeandaa kongamano maalum la kuhamasisha  
na kukuza Uwekezaji  na biashara  kati ya Tanzania na China katika kongamano
hilo linatarajiwa kufanyika  Oktoba 16 mwaka huu.



Hayo yamesemwa na Geofrey Mwambe alipo kuwa akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana ambapo  alisema kuwa lengo la mkutano huo ni kutangaza fursa za biashara  na uwekezaji
zilizopo hapa nchini kwa wawekezaji na wafanya biashara wa China fursa ambazo  zipo
katika sekta mbali mbali  kama vile viwanda ,Madini ,Nishati,Usafiri,Mafuta na pamoja
na Miundombinu.

Alisema sekta zingine ni ujenzi ,uvuvi wa kina  kirefu,Kilimo na usindikaji wa 
mazao,Afya,Teknolojia ya habari na mawasiliano,Madawa. mbali na hayo.

 TIC pia kimekanusha taarifa zilizoenea kuwa wawekezaji wanafunga biashara zao huku kikibainisha kuwa taarifa hizo ni za uongo na zinafaa kupuuzwa kwani wawekezaji wanaendelea kuja nchini kwa ajili ya kuwekeza kwenye sekta mbalimabli.

"China mpaka Mei mwaka huu inaongoza kwa uwekezaji nchini kwa thamani ya 
miradi na tunatarajiwa kongamano hili kuhudhuriwa na wawekezaji wa makampuni
makubwa zaidi ya 100 kutoka China,"alisema Geoffrey.

 Geoffrey alisema China itasaidia kuiweka na kuitangaza Tanzania kama miongoni 
mwa maeneo  yenye fursa  na mazingira mazuri ya kibiashara  kwa kampuni za kutoka
China.

Aidha alisema makampuni ya kitanzania yanakaribishwa  kushiriki kwenye kongamano
hilo ili kuweza kuanzisha , kukuza na kuendeleza ushirikiano katika nyanja za biashara
na uwekezaji kwa kushirikiana na kampni za wafanya biashara wa China.

"Tunategemea Tanzania ita ongeza thamani ya mitaji ya uwekezaji kutoka nje yaani
FDI iwapo makampuni ya China yatakayohudhuria kongamano  yata amua kufanya uwekezaji
nchini,"alisema Geoffrey.

Alisema TIC inapenda kutumia fursa hiyo kuitangaza  Tanzania  kwa ujumla kwani
mpaka sasa  mwezi Mei mwaka huu  kituo cha uwekezaji TIC,kimeweza kusajili  miradi
670 ambayo yenye umiliki wa china inayotarajia kuzalisha ajra zipatazo 83,394 yenye
thamani ya mtaji  wa kiasi cha dola za Marekani 5,779 hivyo hiyo ni fursa  muhimu kabisa
kwa watanzania.




Comments