Skip to main content

‘Umushyikirano’: Somo murua kwa JK kutoka kwa Kagame!


KATIKA toleo Na. 215 la Raia Mwema, Jenerali Ulimwengu alitaja moja ya mapungufu ya watawala wetu Tanzania kwamba ni ile hulka yao ya kutotaka kujifunza na kuiga kutoka kwa wenzetu wa nje (Ughaibuni) wanaofanya vizuri. Aliandika hivi:
“Watawala wetu ni watu wanaosafiri mno, hadi wamesababisha malalamiko kwamba hawatulii nyumbani jinsi walivyo ‘kiguru na njia’. Inashangaza kwamba wanakwenda Ughaibuni kila uchao lakini hawana wanachojifunza huko kuhusu jinsi wenzao walivyopiga hatua za haraka kujiletea maendeleo na kuzikwamua nchi zao kutoka kwenye mateso ya umasikini.
“Wanakwenda Ughaibuni kushangaa maendeleo ya wenzetu na kufanya ‘shopping’ za upuuzi wakati nchi yao inadidimia. Hawana uwezo hata wa kutazama, kuona, kuelewa na kutaka kuiga kilicho kizuri.”
Hivyo ndivyo alivyoandika Jenerali katika toleo hilo. Napenda kuuendeleza kidogo mjadala huo, na nianze kwa kuongeza kwamba; hata kile ambacho kipo chini ya uwezo wa nchi yetu kukitekeleza wenyewe wanachokiona huko Ughaibuni, hawawezi kukiiga. 
Kwa mfano, watawala wetu kadhaa wametembelea miji ya wenzetu kama New Delji (Green Delhi) wa India na Durban wa Afrika Kusini na wamejionea wenyewe jinsi ilivyo misafi na ya kijani lakini wameshindwa kuiga. Wameshindwa kuligeuza jiji letu la Dar es Salaam lifanane angalu kidogo na miji hiyo kwa usafi na u-kijani.
Je; hivi kweli hata usafi wa jiji letu la Dar es Salaam na kuligeuza kuwa la kijani, ni kitu kinachopaswa kusubiri ufadhili wa Wazungu? Kama hivyo ndivyo, ni nini basi tunachoweza kumudu kukifanya sisi wenyewe kwa pesa zetu wenyewe na kwa mikono yetu wenyewe?
Lakini kinachokatisha tamaa zaidi kutoka kwa watawala wetu hawa wa zama hizi, ni kwamba wanashindwa kuiga hata kile chema kinachofanywa na majirani zetu. Mfano mzuri ni hiki kinachofanywa kila mwaka na wenzetu wa Rwanda kinachoitwa Umushyikirano.
Kwa miaka tisa mfululizo, Rais Paul Kagame amekuwa akiitisha, kila mwaka,  mkutano wa kitaifa wa kujadili Muafaka wa Taifa (National Dialogue) – mkutano ambao umepachikwa jina la Umushyikirano.
Kila mwishoni mwa mwaka (Desemba 14 na 15) viongozi wa serikali kuu, viongozi wa serikali za mitaa, wawakilishi wa vikundi vya jumuiya za kiraia (NGOs), viongozi wa dini, wabunge, wanadiplomasia, wafanyabiashara, Wanyarwanda wanaoishi Ughaibuni na wananchi wa kawaida, hukutana kwa siku mbili kwenye ukumbi wa bunge kujadiliana utendaji kazi wa serikali ulivyokuwa kwa mwaka huo na kupeana mikakati kwa mwaka mpya unaofuata.
Ni katika mikutano hiyo ya Umushyikirano ambako miafaka ya kitaifa hufikiwa katika masuala mbalimbali nyeti yanayoigusa nchi. Kwa ufupi, Umushyikirano ni mikutano ya kila mwaka inayojadili mustakabali wa taifa la Rwanda.
Nimekuwa nikiifuatilia mikutano hii kwa miaka mitatu iliyopita ukiwemo wa wiki iliyopita, na lazima nikiri kwamba imenisisimua. Kwangu mimi, ni moja ya vitu vyema vilivyobuniwa na Rais Paul Kagame ambavyo kama vitaendelezwa, vitaiwezesha nchi hiyo kupiga kasi ya maendeleo kuliko tunayoishuhudia sasa.
Kinachonisisimua zaidi kuhusu Umushyikirano ni namna mikutano hiyo inavyoendeshwa. Inaendeshwa kwa uwazi mkubwa. Mbali ya mikutano hiyo kuwa live kwenye televisheni na redio, mijadala yake pia huwekwa kwenye tovuti.
Isitoshe, hata wale Wanyarwanda ambao hawakubahatika kuhudhuria wenyewe mikutano hiyo mjini Kigali, hupewa fursa ya kuchangia maoni yao au hata kuuliza maswali kupitia njia za simu za moja kwa moja na hata kwa njia za sms na twitter.
Kwa uelewa wangu (naomba kusahihishwa kama nakosea), hakuna nchi yoyote ya Kiafrika yenye mkutano wa kila mwaka wa National Dialogue wenye ushiriki mpana na unaoendeshwa kwa uwazi kama huo wa Rwanda.
Na bado wako watu wanaomwita Rais Kagame “dikteta mkubwa” (mimi nasema kama ni dikteta, basi, ni ‘dikteta poa’ – benevolent dictator).
Japo wanakiri kwamba Kagame ameiletea Rwanda maendeleo ya kasi, haraka haraka wanaongeza:“lakini anabana uhuru wa kujieleza na ni mvunjaji mkubwa wa haki za binadamu.”
Mimi sidhani kama kuna dikteta mkubwa popote pale duniani anayeitisha mikutano ya mijadala ya kitaifa mithili ya huu wa kila mwishoni mwa mwaka wa Rais Kagame unaoitwa Umushyikirano ambao kila mwananchi ana haki ya kutema cheche zake, kuuliza lolote au kuchangia lolote! Kama yupo dikteta wa namna hiyo, niambieni ni nani na ni wa nchi gani.
Kwa sababu ya uwazi huo wa mikutano hiyo ya Kagame ya Umushyikirano, hata mimi niliye Dar es Salaam (na ambaye si Mnyarwanda) nimeweza kuifuatilia kwa miaka mitatu iliyopita, na naweza kuwa shuhuda wa baadhi ya matunda ya mikutano hiyo.
Kwa mfano, katika mkutano wa Desemba mwaka jana, washiriki wengi ukumbini na hata waliopiga simu, waliishutumu Serikali ya Rais Kagame kwa kushindwa kuifanikisha haraka kampeni ya ujenzi wa nyumba bora za kuishi kote nchini.
Kwa hakika, mjadala wa mwaka jana ulitawaliwa na utekelezaji wa programu hiyo ya serikali ya kujenga nyumba bora kwa wananchi na kutokomeza nyumba za udongo (nyakatsi) kote nchini Rwanda.
Viongozi wa ngazi za chini walilaumiwa sana kwa kuvurunda programu hiyo. Baada ya majadiliano makubwa, mkutano huo wa Umushyikirano ulikubaliana kwamba watakaozembea kwenye programu hiyo kwa mwaka 2011 watawajibishwa.
Matokeo yake ni kwamba
katika mkutano wa mwaka huu, uliofanyika wiki iliyopita, shutuma zilikuwa chache. Washiriki wengi walieleza kuridhishwa na programu hiyo ya kuteketeza nyumba za udongo nchini humo kwa kujenga za kisasa. Wenyewe wanakiri kwamba programu hiyo sasa imefanikiwa kwa asilimia 98!
Hiyo maana yake ni nini? Hiyo maana yake ni kwamba muda si mrefu nyumba za udongo katika Rwanda zitakuwa ni historia.
Hebu tulitafakari jambo hili kwa undani kidogo. Ni hivi;  wenzetu Rwanda, kwa kupitia mkutano huo wa Umushyikirano, walifikia mwafaka wa kitaifa kwamba nyumba za udongo (nyakatsi) katika Rwanda ziwe historia ndani ya miaka mitano.
Baada ya mwafaka huo wa kitaifa, wote wakaanza kuchapakazi kwa pamoja kuitimiza ndoto hiyo, na kila mwaka wamekuwa wakikutana (kupitia Umushyikirano) kufanya tathmini. Wamesutana na kunyoosheana vidole kwa wale waliovurunda lakini pia wamepongezana na kutiana moyo kwa wale waliofanya vizuri.
Matokeo yake ni kwamba mafanikio kwa mwaka huu wa 2011 unaoelekea ukingoni, yamekuwa asilimia 98! Hiyo maana yake ni kwamba, muda si mrefu nyumba za udongo za nyakatsi zitakuwa historia katika Rwanda.
 Je; ni lini nasi nyumba za udongo katika Tanzania zitakuwa historia? Si tu kwamba hatuna programu ya kuzitokomeza hapa nchini, lakini hata wazo tu la kuwanayo programu ya namna hiyo halipo!
Najua wapo watakaodai kwamba Rwanda ni ka-nchi kadogo kenye watu wachache, na hivyo ni rahisi kutekeleza programu ya namna hiyo. Hiyo ni kweli – Rwanda ni ka-nchi kadogo kenye watu wachache ikilinganishwa na Tanzania, lakini pia ni kweli kwamba ka-nchi hako kadogo hakana utajiri mkubwa wa maliasili ambao Tanzania imejaliwa nao.
Kwa maneno mengine; kama tungekuwa na viongozi wa aina ya Kagame, hakika tungeweza kuutumia utajiri huo mkubwa wa maliasili tulionao kutokomeza zile tembe za Wagogo kule Dodoma au za Wasukuma kule Shinyanga au hata zile nyumba za msonge kule Upareni!
Ndugu zangu, nimetoa mfano mmoja tu wa kutokomezwa nyumba za nyakatsi kama moja ya matunda ya mikutano hiyo ya Umushyikirano ya mijadala ya kitaifa yenye lengo la kufikia miafaka ya kitaifa katika masuala mbalimbali yanayohusu mustakabali wa Taifa la Rwanda, lakini naamini ipo mifano mingi tu mingine ya mafanikio.
Tukirejea hapa nyumbani kwetu,  je; hatuwezi nasi kuiga jambo hilo jema la Rwanda? Kama Umishyikirano imeisaidia Rwanda kuharakisha maendeleo yao, kwanini isitusaidie pia sisi?
Kwanini tusiianzishe mikutano ya namna hiyo na kuitafutia jina letu ili nasi ituwezeshe kufikia miafaka ya kitaifa kuhusu masuala mbalimbali ya maendeleo yetu?
Nauliza hivyo; maana, kwa hali ilivyo sasa hapa nchini mwetu, hatuna National Dialogue. Siku zote tunasikiliza tu kutoka kwa watawala wetu na si kujadiliana nao. Ni lini nasi watatusikiliza na kujadiliana nasi kuhusu mustakabali wa Taifa letu?
Afadhali zama za Nyerere; kwani mara moja moja alikuwa akienda pale UDSM,  ukumbi wa Nkrumah, kukutana na wasomi wetu na kujadiliana nao kuhusu masuala mbalimbali ya kitaifa na kimataifa. Siku hizi si tu kwamba watawala wetu wanakwepa majadiliano ya moja kwa moja na wasomi, lakini hata mikutano tu na waandishi wa habari wanaikwepa?
Siku hizi wakubwa wetu wakiwa na jambo zito la kitaifa, hawataki mjadala au ushauri wa mtu yeyote nje ya dola. Watawaita wazee (wa CCM) pale Diamond Jubilee au ukumbi wa PTA na kuwahutubia au kuwaeleza msimamo wao (wa serikali yao) kuhusu jambo hilo.
Wazee hao wa CCM ‘wakishahutubiwa’, watapiga makofi na kushangilia; hata kama hawakukielewa vyema hicho alichozungumza bwana mkubwa kinachohusu mustakabali wa taifa letu sote.
Staili hii hovyo ya uongozi ni ile wanayoiita kwa kimombo “top down”; yaani kila kitu kinatoka juu kwa wakubwa kwenda chini kwa wananchi. Kwa maneno mengine, wa chini ni wapokeaji tu wa amri na maelekezo!
Nihitimishe safu yangu hivi: Watawala wetu wanajigamba kwamba katika miaka 50 ya Uhuru, wamethubutu. Kama kweli wanathubutu, nawasihi basi wathubutu pia kujifunza somo la Umushyikirano kutoka kwa jirani yetu, Rais Paul Kagame wa Rwanda. Binafsi, naamini ni somo maridadi linaloweza kutusaidia.
Kwangu mimi; mikutano ya kila mwaka kama hiyo ya Rwanda yenye ushiriki mpana, na yenye kujadili na kufikia miafaka ya kitaifa kuhusu masuala mbalimbali, ni matumizi mazuri ya fedha za walipakodi kuliko mikutano ile ya Rais Kikwete kama ule wa Sullivan.Cnazo ni Raiamwema.

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Uganda Police issue fresh terror alert

  By Chris Kiwawulo, The Police have issued a fresh terror alert against a possible attack on Uganda by four terrorists from Kazakhstan. Police spokesperson Judith Nabakooba “We have received a security notification in form of an orange notice of four terrorists originating from Kazakhstan who are planning to travel to foreign countries in order to commit attacks and participate in hostile acts,” Police spokesperson Judith Nabakooba said in a statement on Monday. Nabakooba named the four active members of radical organizations as; Nassiruauly Kairat, Umurzakov Marat Eskendirovich, Kovtun Denis Valerevich and Mazhibayen Alimzhan Akhlazhanovich. By press time, a search on the international web has not yielded anything on the named persons.Last evening, police said that in collaboration with other security agencies vigilance has been stepped up to avert the terrorists’ evil plans. Police have in the past issu...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...