Skip to main content

Soma AY anavyozidi 'Kutisha' katika anga za Muziki

KATIKA Live Chumba cha Habari Global Publishers, leo tunaye mwanamuziki mahiri anayefanya vizuri ndani na nje ya Tanzania, Ambwene Yessaya ‘AY’ au Mzee wa Commerial ambaye amesema sasa hivi amekuwa wakala wa wasanii wa ndani na nje ya nchi.GPL
Mwanamuziki wa Muziki wa Kizazi Kipya nchini, Ambwene Yessaya 'AY' akipozi katika studio za Global TV Online kabla ya kuhojiwa.
Katika mahojiano na safu hii ambayo huwa inarushwa kupitia Global Tv Online kwenye Kipindi cha Mtu Kati, AY aliweka wazi kuwa anafanya muziki kwa ajili ya watu wote.Mwandishi: Unakumbuka nini kupitia kundi lako la zamani la East Coast Team ambayo sasa hivi haipo tena? 
AY: East Coast Team bado ipo, kitu ambacho nakumbuka sisi tulikuwa marafiki na muziki ulitufanya tukawa kama ndugu, nilitoka mwaka 2006 kwa ajili ya tofauti za kimisimamo na kimtazamo, baadaye MwanaFA naye akaja kutoka.
Baada ya kuachana bado tulikuwa tunawasiliana na kutembeleana lakini kila mtu anafanya kazi katika njia yake na mpaka sasa hivi wenyewe bado wanaendelea kama East Coast Team pia kuna ‘project’ ambayo tutakuja kuifanya pamoja mwakani.
Mwandishi: Inasemekana uko zaidi na MwanaFA kuliko GK kuna nini hapo kati?
AY:  Wakati natoka nilibakia kuwa AY na MwanaFA kama MwanaFA na mimi na MwanaFA ni washikaji kama ‘brothers’, ndiyo maana tumeshirikiana kwenye project nyingi zaidi baada ya kutoka nje. Sisi siyo kundi lakini kila mtu ni mwanamuziki wa kujitegemea.
Mwandishi: Mbali na muziki wewe ni meneja ambaye unamiliki wanamuziki wengi ndani na nje ya Tanzania, kwa sasa una wasanii wangapi?
AY: Sasa hivi nimekuwa wakala, kampuni yangu inafanya kazi ya uwakala na wasanii wengi nje na ndani. Miongoni mwao ambao nimeshawahi kufanya nao kuna Nameless, Stereo, Ommy Dimpoz, Chameleone, P-square na wengine wengi. Kampuni kama hizo zipo katika kila nchi kwa hiyo na mimi nikaona bora nifungue. 
Mwandishi: Changamoto gani unakumbana nazo katika biashara zako?
AY: Biashara yoyote ina changamoto na inakufanya akili yako inakuwa inapanuka zaidi na unaweza kujifunza mbinu nyingi kupitia changamoto uliyoipata. Kiukweli tunajitahidi mimi pamoja na wenzangu tunaona jinsi matunda ya kazi yetu tunayoifanya.
AY akiwa ndani ya studio za Global TV Online na prizenta Pamela Daffa 'Pam D'.
Mwandishi: Unahisi ni sababu gani zinawafanya vijana wengi kushindwa kutoboa kimataifa?
AY: Hii kitu nilikuwa naiangalia tangu zamani ndiyo maana naona nikiendelea kushikilia vitu vya zamani nilivyokuwa navifanya nisingeweza kufikisha vitu ambavyo vinafanyika leo.
Nilivyoingia kwenye muziki nilikuwa nataka siku ambayo naacha muziki watu wanikumbuke kwa kitu fulani, lazima muziki ubadilishe maisha yangu ndiyo maana unaona najitahidi kuwavuta wasanii wenzangu kuwapa chaneli na netiweki zingine kwa ajili ya kwenda mbali zaidi.
Mwandishi: Nini siri ya mafanikio yako?
AY: Vyote hivi ni kuipenda kazi uwe na heshima nayo yaani ujiheshimu na pia uwe na mtandao ujue jinsi ya kufahamiana na watu.
Mwandishi: Ulijisikiaje kufanya kazi na Sean Kingstone?
AY: Nilijisikia vizuri sana kwani mefanya kazi na msanii ambaye zamani nilikuwa namuona kwenye runinga sikuwa na mawazo ya kuja kukutana naye na kufanya naye kazi, kizuri zaidi yeye ndiyo alipendekeza nifanye naye kazi nakumbuka alikuwa amekuja hapa na akaona kazi zangu na alivyokwenda kufanya mahojiano kwenye redio nilikuwa nasikiliza siku hiyo  nikashangaa ananitaja mimi bila kujua.
Mwandishi: Ni hatua gani ambayo unaikumbuka imekupa mafanikio?
AY: Nakumbuka Profesa J wakati anazindua albamu yake ya Machozi, Jasho na Damu, akanipa kolabo katika albamu yake wakati nikiwa na ngoma ya Raha Tu, akaniambia wimbo unaitwa Nawakilisha nataka ‘verse’ kesho yake nikawa tayari basi tukaanza kuzunguka na ndiyo ‘tour’ iliyonifanya nikaanza kufahamika Tanzania nzima, kufahamiana na watu zaidi na mpaka leo tunashirikiana vizuri.
Mwandishi: Sasa hivi umesimama kutoa albamu, unakumbuka una albamu ngapi mpaka sasa?
AY: Nimeacha kutoa albamu tangu mwaka 2006 miaka 8 iliyopita, ya kwanza ilikuwa inaitwa Raha Kamili 2003, Hisia Zangu 2005, Habari Ndiyo Hiyo niliyoifanya na MwanaFA. Nafanya muziki kwa ajili ya watu wote, nafanya kama AY lakini bidii zangu pia hata wasanii  wengine wanafaidika nazo, tusapotiane tuweze kusonga mbele, tuwe na upendo kati yetu, tusipandikiziane chuki kati  ya wasani kwa wasanii ili twende pamoja, tufike mbali zaidi.

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.