Skip to main content

Soma AY anavyozidi 'Kutisha' katika anga za Muziki

KATIKA Live Chumba cha Habari Global Publishers, leo tunaye mwanamuziki mahiri anayefanya vizuri ndani na nje ya Tanzania, Ambwene Yessaya ‘AY’ au Mzee wa Commerial ambaye amesema sasa hivi amekuwa wakala wa wasanii wa ndani na nje ya nchi.GPL
Mwanamuziki wa Muziki wa Kizazi Kipya nchini, Ambwene Yessaya 'AY' akipozi katika studio za Global TV Online kabla ya kuhojiwa.
Katika mahojiano na safu hii ambayo huwa inarushwa kupitia Global Tv Online kwenye Kipindi cha Mtu Kati, AY aliweka wazi kuwa anafanya muziki kwa ajili ya watu wote.Mwandishi: Unakumbuka nini kupitia kundi lako la zamani la East Coast Team ambayo sasa hivi haipo tena? 
AY: East Coast Team bado ipo, kitu ambacho nakumbuka sisi tulikuwa marafiki na muziki ulitufanya tukawa kama ndugu, nilitoka mwaka 2006 kwa ajili ya tofauti za kimisimamo na kimtazamo, baadaye MwanaFA naye akaja kutoka.
Baada ya kuachana bado tulikuwa tunawasiliana na kutembeleana lakini kila mtu anafanya kazi katika njia yake na mpaka sasa hivi wenyewe bado wanaendelea kama East Coast Team pia kuna ‘project’ ambayo tutakuja kuifanya pamoja mwakani.
Mwandishi: Inasemekana uko zaidi na MwanaFA kuliko GK kuna nini hapo kati?
AY:  Wakati natoka nilibakia kuwa AY na MwanaFA kama MwanaFA na mimi na MwanaFA ni washikaji kama ‘brothers’, ndiyo maana tumeshirikiana kwenye project nyingi zaidi baada ya kutoka nje. Sisi siyo kundi lakini kila mtu ni mwanamuziki wa kujitegemea.
Mwandishi: Mbali na muziki wewe ni meneja ambaye unamiliki wanamuziki wengi ndani na nje ya Tanzania, kwa sasa una wasanii wangapi?
AY: Sasa hivi nimekuwa wakala, kampuni yangu inafanya kazi ya uwakala na wasanii wengi nje na ndani. Miongoni mwao ambao nimeshawahi kufanya nao kuna Nameless, Stereo, Ommy Dimpoz, Chameleone, P-square na wengine wengi. Kampuni kama hizo zipo katika kila nchi kwa hiyo na mimi nikaona bora nifungue. 
Mwandishi: Changamoto gani unakumbana nazo katika biashara zako?
AY: Biashara yoyote ina changamoto na inakufanya akili yako inakuwa inapanuka zaidi na unaweza kujifunza mbinu nyingi kupitia changamoto uliyoipata. Kiukweli tunajitahidi mimi pamoja na wenzangu tunaona jinsi matunda ya kazi yetu tunayoifanya.
AY akiwa ndani ya studio za Global TV Online na prizenta Pamela Daffa 'Pam D'.
Mwandishi: Unahisi ni sababu gani zinawafanya vijana wengi kushindwa kutoboa kimataifa?
AY: Hii kitu nilikuwa naiangalia tangu zamani ndiyo maana naona nikiendelea kushikilia vitu vya zamani nilivyokuwa navifanya nisingeweza kufikisha vitu ambavyo vinafanyika leo.
Nilivyoingia kwenye muziki nilikuwa nataka siku ambayo naacha muziki watu wanikumbuke kwa kitu fulani, lazima muziki ubadilishe maisha yangu ndiyo maana unaona najitahidi kuwavuta wasanii wenzangu kuwapa chaneli na netiweki zingine kwa ajili ya kwenda mbali zaidi.
Mwandishi: Nini siri ya mafanikio yako?
AY: Vyote hivi ni kuipenda kazi uwe na heshima nayo yaani ujiheshimu na pia uwe na mtandao ujue jinsi ya kufahamiana na watu.
Mwandishi: Ulijisikiaje kufanya kazi na Sean Kingstone?
AY: Nilijisikia vizuri sana kwani mefanya kazi na msanii ambaye zamani nilikuwa namuona kwenye runinga sikuwa na mawazo ya kuja kukutana naye na kufanya naye kazi, kizuri zaidi yeye ndiyo alipendekeza nifanye naye kazi nakumbuka alikuwa amekuja hapa na akaona kazi zangu na alivyokwenda kufanya mahojiano kwenye redio nilikuwa nasikiliza siku hiyo  nikashangaa ananitaja mimi bila kujua.
Mwandishi: Ni hatua gani ambayo unaikumbuka imekupa mafanikio?
AY: Nakumbuka Profesa J wakati anazindua albamu yake ya Machozi, Jasho na Damu, akanipa kolabo katika albamu yake wakati nikiwa na ngoma ya Raha Tu, akaniambia wimbo unaitwa Nawakilisha nataka ‘verse’ kesho yake nikawa tayari basi tukaanza kuzunguka na ndiyo ‘tour’ iliyonifanya nikaanza kufahamika Tanzania nzima, kufahamiana na watu zaidi na mpaka leo tunashirikiana vizuri.
Mwandishi: Sasa hivi umesimama kutoa albamu, unakumbuka una albamu ngapi mpaka sasa?
AY: Nimeacha kutoa albamu tangu mwaka 2006 miaka 8 iliyopita, ya kwanza ilikuwa inaitwa Raha Kamili 2003, Hisia Zangu 2005, Habari Ndiyo Hiyo niliyoifanya na MwanaFA. Nafanya muziki kwa ajili ya watu wote, nafanya kama AY lakini bidii zangu pia hata wasanii  wengine wanafaidika nazo, tusapotiane tuweze kusonga mbele, tuwe na upendo kati yetu, tusipandikiziane chuki kati  ya wasani kwa wasanii ili twende pamoja, tufike mbali zaidi.

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...