Skip to main content

'WANA LAMBALAMBA'AZAM FC YATEKELEZA AGIZO LA DR. MAGUFULI KWA VITENDO





1
Viongozi wa benchi la ufundi la Azam Academy wakishiriki shughuli za usafi kwenye Zahanati ya Chamazi
Kikosi cha Azam FC leo kimetekeleza agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Mgufuli alilolitoa majuma machache kabla ya kuadhimisha siku ya Uhuru wa Tanganyika kwamba, siku ya kuadhimisha Uhuru wa Tanganyika December 9 wananchi wote wafanye usafi kwenye maeneo yanayowazguka ili kuzuia magonjwa mbalimbali yasababishwayo na uchafu.
Katika kutekeleza agizo hilo la Rais Magufuli, kikosi cha Azam FC kwa kushirikiana na wananchi leo kimefanya usafi kwenye Zahanati ya Chamazi iliyopo eneo la Chamazi-Mbande, Manispaa ya Temeke kwa kusafisha mazingira yanayoizunguka zahanati hiyo.

7
Wachezaji wakimwaga taka baada ya kusafisha mazingira yanayozunguka eneo la Zahanati ya Chamazi
Asilimia kubwa ya wachezaji, makocha na viongozi wengine walikuwa wanatoka katika kikosi B kutokana na kikosi cha kwanza kuwa kwenye maandalizi ya mchezo wa ligi kuu dhidi ya Simba SC unaotarajiwa kuchezwa siku ya Jumamosi December 12.
Mganga mfawidhi wa zahanati hiyo Bi Eduiga Mroso ameushukuru uongozi wa Azam FC pamoja na wachezaji wote walioshiriki kwenye usafi wa maeneo yanayoizunguka zahanati hiyo na kuiomba timu hiyo kuendeleza ushirikiano na ujarani mwema uliopo kati yao.

6
Bi. Eduiga Mroso, Mganga Mfawidhi wa Zahanati ya Chamazi
“Tunaishukuru timu ya Azam FC kuamua kuja kwetu kushirikiana na sisi kuunga mkono kauli ya Rais wetu Magufuli ya kuadhimisha siku ya Uhuru kwa kufanya usafi kwenye maeneo yanayotuzunguka. Lakini ushirikiano wetu usiishie hapa bali uende mbali zaidi kwasababu sisi pia ni majirani na tunawashukuru sana Azam kwa hilo kwasababu wengeweza kwenda sehemu nyingine lakini waliamua kuja kwetu”, amsesema Bi Mroso.
Kwa upande wa mtendaji mkuu wa kikosi hicho Saad Kawemba amesema wameamua kufanya usafi kwenye zahanati hiyo ikiwa ni sehemu ya kudumisha ushirikiano wao na jamii hasa sehemu zenye uhitaji kama zahanati, shule na sehemu nyingine nyingi.

5
Saad Kawemba, Mtendaji mkuu wa Azam FC
Pia akaongeza kuwa, zahanati hiyo ipo eneo la jirani na wao hivyo hata ikitokea mchezaji au mtu yeyote amepatwa na maradhi atapelekwa kwenye zahanati hiyo kwa ajili ya matibabu na hicho ndio kitu kilichowasukuma kushirikiana na wakazi wa eneo la Chamazi kufanya usafi kwenye zahanati hiyo.
“Sisi kama Azam tumeamua kuja kushiriki shughuli ya usafi hapa kwasababu kwanza tunataka kudumisha ushirikiano wetu na jamii inayotuzunguka lakini pia kutekeleza agizo la Rais alilolitoa juu ya maadhimisho ya siku ya leo kwamba itakuwa ni siku ya kufanya usafi na si sherehe kubwa ya kitaifa”, amesema Kawemba wakati wa zoezi la usafi kwenye zahanati ya Chamazi.
4
“Lakini hawa ni majirani zetu, ikitokea mchezaji au kiongozi wa Azam FC akapatwa na maradhi ataletwa hapa, kwahiyo tukaona ni vyema tuje kushirikiana na majirani zetu kufanya usafi kwenye eneo la hii zahanati.

3
Wachezaji wa Azam wakisafisha mfereji (mtaro) pembeni ya zahanati ya Chamazi
Mh. Dr. Magufuli alipiga marufuku kufanyika sherehe kubwa za maadhidimisho ya siku ya Uhuru ambazo zimekuwa zikigharimu pesa nyingi na badala yake akaagiza pesa hizo zifanye kazi nyingine za maendeleo ya jamii na siku hiyo wananchi wote wafanye usafi kwenye maeneo yanayowanunguka.

2
Viongozi wa kikosi cha Azam wakishiriki zoezi la usafi lililofanyika kwenye zahanati ya Chamazi

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.