Skip to main content

Uganda kuitisha tena mazungumzo ya Burundi

Burundi Armee findet Waffen in der Hauptstadt Bujumbura
Uganda imesema itaitisha tena mazungumzo ya upatanishi ya Burundi, kufuatia machafuko yaliyoipeleka nchi hiyo ndogo kwenye kingo za vita na kuulazimu Umoja wa Afrika kujitayarisha kutuma kikosi cha kuwalinda raia.
Serikali ya Burundi na pia kundi kubwa zaidi la upinzani wamekaribisha hatua ya kuanzisha tena mazungumzo hayo. Siku ya Ijumaa, (18.12.2015) Umoja wa Afrika ulisema unajiandaa kutuma kikosi cha wanajeshi 5,000 nchini Burundi kuwalinda raia, ukitumia nguvu kwa mara ya kwanza kutuma wanajeshi katika nchi mwanachama dhidi ya matakwa ya nchi hiyo.
Hali ya wasiwasi umekuwa ikiongezeka nchini Burundi hasa tangu watu wenye silaha walipovamia kambi za kijeshi katika mji mkuu Bujumbura wiki iliyopita, na kuzusha hofu katika kanda hiyo ambako kumbukumbu za mauaji ya kimbari ya mwaka 1994 katika nchi jirani ya Rwanda zingalipo.
Burundi ilitumbukia katika mgogoro mwezi Aprili baada ya Rais Pierre Nkurunziza kutangaza mipango ya kuwania muhula wa tatu madarakani. Umoja wa Mataifa unasema watu wasiopungua 400 wameuawa tangu mwezi Aprili, wakati uamuzi huo wa Nkurunziza ulipozusha maandamano na baadae jaribio la mapinduzi lililoshindwa.
Serikali yasema iko tayari
Waziri wa ulinzi wa Uganda Chrispus Kiyonga, aliuambia mkutano wa wandishi wa habari mjini Kampala siku ya Jumamosi, kwamba hali ya usalama nchini Burundi imekuwa ikidorora kila kukicha. "Tunadhani sasa ni wakati muafaka na muhimu kuanzisha tena majadiliano," alisema Kiyonga.(P.T)
Kiyonga alisema karibu makundi 14 yanayowakilisha matabaka mbalimbali ya jamii ya Burundi, kikiwemo chama tawala, vyama vya upinzani na mashirika ya kiraia yatahudhuria mazungumzo hayo.
Msemaji wa serikali ya Burundi Philippe Nzobonariba alisema serikali imekuwa tayari wakati wote kufanya mazungumzo na ilikuwa inasubiri mwaliko. "Ni mazungumzo ya Warundi na ni Warundi tu watakaoamua nini cha kujadiliana," aliliambia shirika la habari la Reuters.
Nzobonariba hata hivyo aliondoa uwezekano wa kuzungumza na yeyote ambaye serikali inamchukulia kuwa mhusika katika jaribio la mapinduzi lililofeli. "Linaweza kuwa tukio la kutuwezesha kuwakamata kwa sababu wanatafutwa na vyombo vya sheria vya Burundi," alisema.
Mazungumzo kuanza Desemba 28
Pancrace Cimpaye, msemaji wa muungano mkubwa zaidi wa upinzani nchini Burundi unaojulikana kama CNARED, alikaribisha hatua ya Uganda kuitisha upya mazungumzo ya amani, inagwa alisema mungano wake ulikuwa bado haujapatiwa mwaliko.
"Kwetu mazungumzo ni kati ya pande mbili kwenye mgogoro, na pande hizo mbili zinazozozana ni Nkurunziza na serikali yake kwa upande mmoja, na CNARED kwa upande mwingine," aliliambia shirika la Reuters.
Mazungumzo hayo yataanza tena nchini Uganda Desemba 28, na baadae yatahamishiwa mjini Arusha nchini Tanzania, yaliko makao makuu ya jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), ambayo Burundi ni mwanachama wake.
Mwezi Julai jumuiya ya Afrika Mashariki ilimeteua Rais wa Uganda Yoweri Kaguta Museveni kuwa mpatanishi wa mgogoro huo na mikutano ya awali ilifanyika katika mji mkuu wa Burundi katika mwezi huo.
Hali yazidi kuwa mbaya
Katika mapigano mabaya zaidi tangu jaribio la mapinduzi lililoshindwa mwezi Mei, waasi walizishambulia kambi za kijeshi katika mji mkuu wa Burundi; Bujumbura wiki iliyopita, ambapo karibu watu 90 waliuawa.
Mashirika ya kuteteta haki za binaadamu yameripoti kuwepo na makabiliano mabaya kati ya waandamanaji na vikosi vya serikali, mashambulizi ya silaha na kuwekwa vizuwizini wakosoaji wa serikali. Lakini serikali imepuuza ripoti za ukiukaji wa haki za binaadamu.
Mamia ya maelfu ya Warundi wameikimbia nchi hiyo kunusuru maisha yao tangu ulipoibuka mgogoro huo mbaya zaidi kuikumba Burundi tangu ilipotoka kwenye vita vya wenyewe kwa wenyewe vilivyokuwa na mwelekeo wa kikabila mwaka 2005.
Mwandishi: Iddi Ssessanga/rtre.
Mhariri. Caro Robi
Chanzo:DW

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...

Uganda Police issue fresh terror alert

  By Chris Kiwawulo, The Police have issued a fresh terror alert against a possible attack on Uganda by four terrorists from Kazakhstan. Police spokesperson Judith Nabakooba “We have received a security notification in form of an orange notice of four terrorists originating from Kazakhstan who are planning to travel to foreign countries in order to commit attacks and participate in hostile acts,” Police spokesperson Judith Nabakooba said in a statement on Monday. Nabakooba named the four active members of radical organizations as; Nassiruauly Kairat, Umurzakov Marat Eskendirovich, Kovtun Denis Valerevich and Mazhibayen Alimzhan Akhlazhanovich. By press time, a search on the international web has not yielded anything on the named persons.Last evening, police said that in collaboration with other security agencies vigilance has been stepped up to avert the terrorists’ evil plans. Police have in the past issu...