Skip to main content

NEC yabaini kasoro 300 katika Daftari


Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji Mstaafu Damian Lubuva
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji Mstaafu Damian Lubuva
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec), imesema uchakataji wa Daftari la Kudumu la Wapigakura umekamilika na wamebaini kasoro ndogo ndogo takriban 300 ambazo zimeondolewa.
Mkurugenzi wa Daftari na Tehama wa Nec, Dk. Modest Kipilimba, alisema walianza na kasoro 17 zilizobainishwa na Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).
Ukawa walibainisha kasoro hizo katika kituo cha mpigakura cha Ofisi ya Kitongoji Azimio 1, chenye namba 10101010102, kilichopo mtaa wa Mahoma/Makulu, Kata ya Chahwa, jimbo la Dodoma Mjini.
Ukawa walibainisha vivuli, mabati, hoteli, watu waliojipiga picha wenyewe, Wazungu, Wachina na vivuli vikiwa vimepewa namba ya mpigakura na majina yasiyoeleweka.
“Tumeondoa kasoro nyingi sana na kituo cha Azimio kwa sasa hakuna kasoro yoyote, mbali na kasoro hizo, kasoro nyingi ni za jinsia, kujirudia, jina kutokuonekana, majina kukosewa kulingana na wananchi wanavyopiga simu katika kituo chetu kilichopo Nec,” alisema.
Aidha, alisema ni vugumu kueleza kasoro hizo zilibainika katika vituo vingapi, lakini kwa sasa vyama husika vimekabidhiwa Daftari ambalo halina kasoro zozote.
“Daftari limeshapelekwa katika vituo mbalimbali na limebandikwa, wananchi wanapokwenda kwenye vituo kuangalia taarifa zao wanapoona hazipo wanaruhusiwa kuwasiliana nasi moja kwa moja kupitia ‘Calling center’ yetu, apige namba 0800782100 ili kupata msaada, nasi tunarekebisha taarifa zake,” alifafanua Dk. Kipilimba.
Alisema marekebisho yataendelea kwa kadiri wananchi wanavyopiga simu kwa kuwa ni jambo la kawaida kuchanganya majina ambayo siyo rahisi kuyabaini kama ni ya kike au kiume kwa kuwapa jinsia halisi.
Dk. Kipilimba alisema kasoro nyingine ni za waliojiandikisha zaidi ya mara moja kwa kuwa wapo ambao wamejiandikisha mara nane, lakini Daftari la mwisho linapaswa kumtambua mtu mmoja.
Mkurugenzi huyo alisema vyama vyote vimeshapewa Daftari lingine ambalo limekamilika na vinaruhusiwa kuwasilisha kasoro watakazoziona kwa kuwa kasoro nyingi ni za kawaida na za kibinadamu zaidi.
Alisema kuwa kasoro hizo hazitabadili idadi ya wapigakura kwa kiasi kikubwa na kwamba haitazidi 100 kwani hadi sasa wenye sifa ya kupiga kura ni 22, 751,292.
Awali baada ya kukamilika uandikishaji wapigakura Nec ilisema watu wenye sifa ya kupiga kura ni zaidi ya milioni 23.78, na baada ya uchakataji ilibainika watu milioni 22.75 ndiyo wapiga kura halali.
Chanzo: NIPASHE

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.