Skip to main content

Siyo wakati wa Taifa Stars kukata tamaa

JUZI timu yetu ya soka ya taifa,Taifa Stars ilicheza mechi ya kuwania kufuzu kushiriki Fainali za Mataifa ya Afrika CAN dhidi ya Algeria kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.Fainali za 28 za Mataifa ya Afrika zinatarajiwa kufanyika katika nchi za Gabon na Guinea ya Ikweta kuanzia Januari 21 mpaka Februari 12, 2012.

Taifa Stars ambayo ipo katika kundi D pamoja na nchi za Jamhuri ya Afrika ya Kati, Algeria na Morocco ilianza harakati zake za kutaka kufuzu kushiriki katika fainali hizo za mataifa ya Afrika kwa kucheza na Algeria na kutoka nayo sare ya 1-1, kabla ya kucheza na Morocco na kufungwa bao 1-0, Stars iliichapa Jamhuri ya Afrika ya Kati 2-1, pia ilifungwa na Jamhuru ya Afrika ya Kati 2-1 na kutoka sare 1-1 na Algeria.

Hivi sasa Stars imebakisha mechi moja dhidi ya Morocco mechi itakayochezwa mjini Rabat kati ya tarehe 7,8,9 mwezi Oktoba, 2011.

Ni wazi Taifa Stars baada ya kutoka sare ya bao 1-1 na Algeria juzi kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam imejiweka katika mazingira magumu ya kufuzu kushiriki Fainali za Mataifa ya Afrika mwakani.

Lakini, hata hivyo huu siyo wakati wa wachezaji wa Stars, viongozi wa soka, serikali na mashabiki wa soka nchini kukataa tamaa kwa sababu kila timu inayomaliza ikiongoza kundi katika hatua hizi za kufuzu ndiyo inayofuzu kushiriki Fainali za Mataifa ya Afrika, ingawa zipo nafasi mbili kwa ajili ya timu zilizofanya vizuri na kumaliza katika nafasi ya pili.

Ukiangalia msimamo wa kundi D ambalo ipo Taifa Stars utaona Tanzania inashika nafasi ya tatu na ina pointi tano wakati Algeria inashika nafasi ya nne ikiwa na pointi tano.Timu zingine ambazo zipo kwenye kundi hilo ni Morocco inayoongoza ikiwa na pointi saba ikifuatiwa na Jamhuri ya Afrika ya Kati yenye pointi saba pia.

Hata hivyo jana Morocco na Jamhuri ya Afrika ya Kati zilikuwa zikicheza mjini Bangui, ambapo kama timu hizo zimetoka sare basi zitakuwa zimefikisha pointi nane kila moja na kama timu moja imeifunga nyingine basi mojawapo itakuwa imefikisha pointi 10 na nyingine kubaki za pointi saba.

Hivyo nafasi ya kufuzu bado ipo kwa timu zote za Kundi D kwa sababu mechi za mwisho ndizo zitakazoamua timu ipi ifuzu na timu ipi iwanie nafasi mbili kwa ajili ya timu zilizofanya vizuri na kumaliza katika nafasi ya pili katika kila kundi.

Ukiacha mechi ya mwisho ya Stars dhidi ya Morocco mjini Rabat, timu ya Algeria yenyewe itaikaribisha Jamhuri ya Afrika ya Kati na kama Taifa Stars itaifunga Morocco katika mechi yake ya mwisho Stars itakuwa imefikisha pointi nane, lakini kama Jamhuri ya Afrika ya Kati imeifunga Morocco katika mechi ya jana itafikisha pointi 10 na kujiweka katika nafasi nzuri ya kufuzu, pia Morocco ikishinda mechi yake dhidi ya Stars au kama imeshinda mechi yake ya jana itakuwa imefikisha pointi 10 na kuwa na uhakika pia wa kufuzu.

Tunaamini vijana wa Taifa Stars hawatakata tamaa na kuhakikisha wanakamilisha ratiba ya mashindano haya ya kufuzu kwa uwezo wa juu kama walivyocheza katika mechi ya juzi dhidi ya Algeria.

Tunaamini wachezaji wa Stars wanahitaji pongezi na walionyesha kulipigania taifa kwa hali na mali, walicheza kitimu, walijituma, walitengeneza nafasi nyingi za ushindi ila bahati haikuwa yao.

Tunatarajia kuona TFF, wadhamini, mashabiki pamoja na serikali wakiendelea kumpa ushirikiano mzuri kocha Jan Poulsen kwa ajili ya mechi ijayo na tunaamini kocha Poulsen ataweza kuchagua tena wachezaji ambao wataipeperusha vizuri bendera ya Tanzania na kuwaandaa vizuri kwa ajili ya kuhakikisha ushindi unapatikana.

Tunawapongeza pia mashabiki wengi wa soka nchini ambao walijitokeza kuishangilia Taifa Stars na kuacha tabia yao ya kushangilia wachezaji wa timu za Simba na Yanga tu waliopo kwenye kikosi cha Taifa Stars.

Mashabiki wa soka wa Tanzania walichangia kwa kiasi kikubwa kuwaongezea hamasa vijana wa Stars katika mechi dhidi ya Algeria kutokana na moyo wao wa uzalendo wa kuwashangilia ambao watanzania wanatakiwa kundelea nao bila kukata tamaa hata tukifungwa.Habari hii kwa hisani ya Mwanachini .co.tz

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...