Skip to main content

Siyo wakati wa Taifa Stars kukata tamaa

JUZI timu yetu ya soka ya taifa,Taifa Stars ilicheza mechi ya kuwania kufuzu kushiriki Fainali za Mataifa ya Afrika CAN dhidi ya Algeria kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.Fainali za 28 za Mataifa ya Afrika zinatarajiwa kufanyika katika nchi za Gabon na Guinea ya Ikweta kuanzia Januari 21 mpaka Februari 12, 2012.

Taifa Stars ambayo ipo katika kundi D pamoja na nchi za Jamhuri ya Afrika ya Kati, Algeria na Morocco ilianza harakati zake za kutaka kufuzu kushiriki katika fainali hizo za mataifa ya Afrika kwa kucheza na Algeria na kutoka nayo sare ya 1-1, kabla ya kucheza na Morocco na kufungwa bao 1-0, Stars iliichapa Jamhuri ya Afrika ya Kati 2-1, pia ilifungwa na Jamhuru ya Afrika ya Kati 2-1 na kutoka sare 1-1 na Algeria.

Hivi sasa Stars imebakisha mechi moja dhidi ya Morocco mechi itakayochezwa mjini Rabat kati ya tarehe 7,8,9 mwezi Oktoba, 2011.

Ni wazi Taifa Stars baada ya kutoka sare ya bao 1-1 na Algeria juzi kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam imejiweka katika mazingira magumu ya kufuzu kushiriki Fainali za Mataifa ya Afrika mwakani.

Lakini, hata hivyo huu siyo wakati wa wachezaji wa Stars, viongozi wa soka, serikali na mashabiki wa soka nchini kukataa tamaa kwa sababu kila timu inayomaliza ikiongoza kundi katika hatua hizi za kufuzu ndiyo inayofuzu kushiriki Fainali za Mataifa ya Afrika, ingawa zipo nafasi mbili kwa ajili ya timu zilizofanya vizuri na kumaliza katika nafasi ya pili.

Ukiangalia msimamo wa kundi D ambalo ipo Taifa Stars utaona Tanzania inashika nafasi ya tatu na ina pointi tano wakati Algeria inashika nafasi ya nne ikiwa na pointi tano.Timu zingine ambazo zipo kwenye kundi hilo ni Morocco inayoongoza ikiwa na pointi saba ikifuatiwa na Jamhuri ya Afrika ya Kati yenye pointi saba pia.

Hata hivyo jana Morocco na Jamhuri ya Afrika ya Kati zilikuwa zikicheza mjini Bangui, ambapo kama timu hizo zimetoka sare basi zitakuwa zimefikisha pointi nane kila moja na kama timu moja imeifunga nyingine basi mojawapo itakuwa imefikisha pointi 10 na nyingine kubaki za pointi saba.

Hivyo nafasi ya kufuzu bado ipo kwa timu zote za Kundi D kwa sababu mechi za mwisho ndizo zitakazoamua timu ipi ifuzu na timu ipi iwanie nafasi mbili kwa ajili ya timu zilizofanya vizuri na kumaliza katika nafasi ya pili katika kila kundi.

Ukiacha mechi ya mwisho ya Stars dhidi ya Morocco mjini Rabat, timu ya Algeria yenyewe itaikaribisha Jamhuri ya Afrika ya Kati na kama Taifa Stars itaifunga Morocco katika mechi yake ya mwisho Stars itakuwa imefikisha pointi nane, lakini kama Jamhuri ya Afrika ya Kati imeifunga Morocco katika mechi ya jana itafikisha pointi 10 na kujiweka katika nafasi nzuri ya kufuzu, pia Morocco ikishinda mechi yake dhidi ya Stars au kama imeshinda mechi yake ya jana itakuwa imefikisha pointi 10 na kuwa na uhakika pia wa kufuzu.

Tunaamini vijana wa Taifa Stars hawatakata tamaa na kuhakikisha wanakamilisha ratiba ya mashindano haya ya kufuzu kwa uwezo wa juu kama walivyocheza katika mechi ya juzi dhidi ya Algeria.

Tunaamini wachezaji wa Stars wanahitaji pongezi na walionyesha kulipigania taifa kwa hali na mali, walicheza kitimu, walijituma, walitengeneza nafasi nyingi za ushindi ila bahati haikuwa yao.

Tunatarajia kuona TFF, wadhamini, mashabiki pamoja na serikali wakiendelea kumpa ushirikiano mzuri kocha Jan Poulsen kwa ajili ya mechi ijayo na tunaamini kocha Poulsen ataweza kuchagua tena wachezaji ambao wataipeperusha vizuri bendera ya Tanzania na kuwaandaa vizuri kwa ajili ya kuhakikisha ushindi unapatikana.

Tunawapongeza pia mashabiki wengi wa soka nchini ambao walijitokeza kuishangilia Taifa Stars na kuacha tabia yao ya kushangilia wachezaji wa timu za Simba na Yanga tu waliopo kwenye kikosi cha Taifa Stars.

Mashabiki wa soka wa Tanzania walichangia kwa kiasi kikubwa kuwaongezea hamasa vijana wa Stars katika mechi dhidi ya Algeria kutokana na moyo wao wa uzalendo wa kuwashangilia ambao watanzania wanatakiwa kundelea nao bila kukata tamaa hata tukifungwa.Habari hii kwa hisani ya Mwanachini .co.tz

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.