Skip to main content

Ngeleja Tena Kuhusu Mgawo wa Umeme


MATUMAINI yaliyotolewa na Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja kwamba makali ya mgawo wa umeme yangepungua kwa kiasi kikubwa kuanzia Septemba 7, mwaka huu yamekuwa kinyume chake kutokana na adha ya upatikanaji wa nishati hiyo kuongezeka.

Maeneo mengi ya Jiji la Dar es Salaam hayana umeme yapata siku tatu sasa, huku mengine yakipata nishati hiyo mara moja katika muda wa saa 36 na 48.
Ngeleja alitoa ahadi kwamba kungekuwa na nafuu ya mgawo baada ya kuwashwa kwa mitambo ya umeme ya Kampuni ya Symbion na ile ya Aggreko ambayo kwa ujumla wake, ilitarajiwa kuzalisha megawati 137.5.
Hata hivyo, hadi jana jioni mitambo hiyo haikuwa imewashwa hivyo kusababisha maeneo mengi ya Dar es Salaam kuendelea kuwa gizani.

Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili jana umebaini kuwa baadhi ya maeneo ya yakiwamo Ubungo, Mwenge, Kimara, Temeke, Keko na Sinza makali ya mgawo wa umeme yamezidi huku Tabata kukiwa hakuna umeme kwa siku tatu mfululizo.
Mtendaji Mkuu wa Symbion, Stanley Munai alisema bado hawajaanza uzalishaji licha ua mafuta ya kuwashia mitambo kufika akisema kwanza wameyapeleka kuyapima ili kujua kama yanafaa ama la... “Tunasubiri majibu ili kuona kama yanafaa au hayafai.”

Alisema uamuzi wa kuyapima mafuta hayo umezingatia kwamba mtambo wao utakuwa ukiyatumia kwa mara ya kwanza, hivyo ni lazima yapimwe ili yasije kusababisha tatizo jingine.
“Ukiwasha bila kupima mafuta unaweza kuua mtambo, mafuta huwa tunachukulia katika kampuni ya kuuza mafuta ya BP,” alisema Munai.

Alipoulizwa ni lini mitambo hiyo itawashwa, Munai alisema: “ Muda wowote tu tukishapata majibu, mafuta huwa yanapimwa na kampuni ya SGS au Intertake.”

Alichoahidi Ngeleja Septemba 4
Septemba 4, mwaka huu alipotembelea mitambo hiyo iliyopo Ubungo, Ngeleja alisema makali ya umeme yangepungua kwa kiasi kikubwa akirejea ahadi aliyopewa na Symbion kwamba mitambo yao ingewashwa katika muda huo.
Ngeleja kwa kauli ya kujiamini alikwenda mbali zaidi huku akisisitiza kwamba mpaka kufikia Desemba mwaka huu, uzalishaji wa umeme utafikia megawati 572, hivyo kutamaliza kabisa mgawo wa umeme.

“Mitambo ya Symbion ina uwezo wa kuzalisha megawati 112 ambayo inatumia gesi na mafuta mepesi, mpaka sasa inazalisha megawati 75 tu, megawati nyingine 35.7 za mtambo huu zitaanza kuzalishwa kesho (Septemba 6) au keshokutwa (Septemba 7) baada ya kuwasili kwa mafuta mepesi” alisema Ngeleja.

Alisema kuwa mitambo ya Aggreko ambayo inazalisha megawati 100 utawashwa baada ya kukamilika kwa ufungaji wa baadhi ya vifaa zikiwemo transfoma.
Hii si mara ya kwanza kwa Ngeleja kutoa kauli kama hiyo kwani amekuwa akifanya hivyo na kutoa ahadi ambazo utekelezaji wake umekuwa mgumu.

Mapema mwaka huu, wakati akiapishwa kushika nafasi yake ya Waziri wa Nishati na Madini kwa kipindi kingine, aliutangazia umma kwamba mgawo wa umeme ungekuwa historia lakini wiki hiyo ya kwanza tangu kuapishwa kwake nchi ikatikiswa na mgawo mkubwa.

Alipotafutwa kwa ajili ya kuzungumzia ongezeko la makali ya mgawo, Meneja Uhusiano wa Shirika la Ugavi wa Umeme Tanzania (Tanesco), Badra Masoud hakupatikana kwani simu yake ilikuwa ikiita bila majibu ya kupokewa.

Hata hivyo, mmoja wa wafanyakazi wa kampuni hiyo ambaye hakutaka kutajwa jina lake kwa kuwa si msemaji wa alisema Badra alikuwa msibani na kwamba hayupo ofisini mpaka Jumatatu ijayo.

“Badra amefiwa hayupo kwa sasa, ila kuhusu suala la mtambo wa Symbion ungekwenda kuzungumza na haohao Symbion kwa sababu wao wanawauzia umeme Tanesco,” alisema mfanyakazi huyo.

Kuhusu mitambo ya Aggreko alisema mitambo hiyo itawashwa mwezi huu baada ya kukamilika ufundi.
“Unajua kuna upungufu wa megawati 300 katika Gridi ya Taifa kwa hiyo hata zikiwashwa hizo megawati 37.5 za Symbion na megawati 100 za Aggreko bado kutakuwa na mgawo, Waziri Ngeleja alifafanua kuwa mpaka Desemba mwaka huu ndipo mgawo utakwisha kabisa,” alisema mtumishi huyo.

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.