Skip to main content

Posts

Yanga imepanga kukusanya shilingi bilioni 1.5

Klabu ya Yanga imepanga kukusanya shilingi bilioni 1.5 kutoka kwa wanachama na mashabiki wake nchi nzima ikiwa ni awamu ya pili ya kampeni ya uchangiaji kwaajili ya kuiendesha timu hiyo. Mkakati huo umewekwa bayana leo katika kikao cha kwanza cha kamati ya uzinduzi na uhamasishaji rasmi wa kampeni ya kuichangia timu hiyo awamu ya pili chini ya mwenyekiti wake Anthony Mavunde ambaye pia ni Mbunge wa Dodoma Mjini. “Pamoja na mipango na mikakati mipya mizuri iliyowekwa kwenye kikao hicho, Mwenyekiti wa Kamati Mh. Antony Mavunde aliainisha mpango mpya wa kukusanya kiasi cha Tsh 1.5B kutoka kwa wanachama na mashabiki wa Yanga mikoa yote nchini”, imeeleza sehemu ya taarifa iliyotolewa leo na klabu hiyo.

RC Makonda :Awaomba wantanzania kuonesha uzalendo kwa kuishangilia Taifa Stars

BAADA ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kuwa imetaja Kamati maalum ya wajumbe 14 kwa ajili ya kuisaidia timu ya taifa, Taifa Stars ifuzu fainali za kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON)   zitakazofanyika kuanzia Juni 21 hadi Julai 19 mwaka huu nchini Misri. kamati hiyo inayoongozwa na mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda ambaye ni mwenyekiti na katibu ni Mhandisi Hersi Said imesema kuwa jukumu kubwa la kamati hiyo ni kuhakikisha timu hiyo ya taifa inapata ushindi katika mchezo wake wa mwisho wa kundi L kuwania tiketi hiyo ya AFCON dhidi ya timu ya taifa ya Uganda (Uganda Crane) katika mchezo utakaochezwa uwanja wa taifa jijini Dar es Salaam Machi 24. Kikosi cha timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars tayari kimeingia kambini  katika  hoteli ya Bahari Beach iliyopo Kunduchi mjini Dar es Salaam kujiandaa na mchezo wa mwisho wa Kundi Lkufuzu Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika baadaye mwezi huu. Akizungumza na waandishi wa habri jana ...

Walio ibuka na ushindi Jackpot wakabidhiwa million 85 leo

Washindi wawili  wa Jackpot  leo wamekabidhiwa million 85 na Kampuni ya Bahati Nasibu ya Premier Bet Tanzania , imekabidhi hundi hiyo  kwa washindi hao wa Jackpot ya soka kwa Flavian Msigala kutoka Dar es Salaam na Robert Daniel kutoka Mpanda huku kila mmoja atajinyakulia mill 42.5. Akizungumza na waandishi wa jijini Dar es Salaam,Afisa rasilimali watu na Meneja utawala Amanda Reuben Kombe amesema kuwa kampuni hiyo pamoja na Michezo mingine wamekua wakiendesha mchezo wa Jackpot ya soka kupitia vituo vya mawakala wao na maduka kote nchini Tanzania. Aidha amesema ikampuni hiyo, imekua ikiendesha shughuli zake kwa kufuata misingi yote ya kubashiri timu ambayo imewekwa, hivyo amewataka wananchi kuendelea kubashiri michezo mbalimbali kupitia premier bet ili kuboresha maisha yao endapo wataibuka washindi na kuachana na propaganda kuwa washindi hupangwa. “Kampuni yetu ya Premier Bet huendeshwa kwa kufuata kanuni na sheria ya...

Patrick Aussems Nyoni yuko fiti kuimaliza AS Vita Kesho

Kocha Mkuu wa Simba, Patrick Aussems amesema beki kiraka wa Simba, Erasto Nyoni atakuwepo kwenye mchezo wa kesho lakini atamkosa Juuko Murshid. Nyoni ameanza kufanya mazoezi baada ya kupona jeraha la kwenye mguu alilopata mwezi Januari kwenye michuano ya Mapinduzi. Aussems amesema Nyoni alifanya mazoezi tangu wiki iliyopita ingawa hakukusafiri kwenda Algeria ila bado ana nafasi ya kuwa ndani ya kikosi chake kesho. "Nyoni tulianza naye mazoezi hivyo imani yetu tutakuwa naye kwenye kikosi cha kesho kitakachowavaa AS Vita. "Kuhusu Juuko bado anahitaji mapumziko mpaka Jumatatu kwa hiyo kwa uhakika Juuko hatakuwepo katika timu," amesema Aussems.

Hatua ya robo fainali klabu bingwa itaanza kutimua vumbi mapema mwezi Aprirl

Hatua ya robo fainali itaanza kutimua vumbi mapema mwezi Aprirl mwaka huu  na makundi hayo yapo kama ifuatavyo:- Ajax atamenyana na Juventus. Liverpool dhidi ya FC Porto. Totthenhum dhidi ya Manchester City. Manchester United dhidi ya Barcelona. Mshindi kati ya Liverpool na FC Porto atamenyana na mshindi kati ya Manchester United na Barcelona kwenye hatua ya nusu fainali huku mshindi kati ya Ajax na Juventus atamenyana na mshindi kati ya Totthenham na Manchester City.

Kambi:kongamano na maonesho ya Saba Afya Jumuiya ya Afrika Mashariki Kufanyika Dar Machi 27

 Kongamano la Maonesho ya Awamu ya Saba ya afya, sayansi na Biashara Jumuiya ya Afrika Mashariki pamoja na maonyesho ya kimataifa limepangwa kuanza Machi 27 hadi 29 mwaka huu Jijini Dar es Salaam. Hayo yamesemwa leo jijini Dar es Salaam leo   na Mganga Mkuu wa Serikali, Profesa Muhamad Kambi wakati akitoa taarifa ya kongamano na maonesho hayo yatayofanyika kwa siku tatu. Amesema kuwa kongamano hilo ni la saba na kwamba lengo ni kubadilishana mawazo kati ya washiriki ya namna ya kutumia Tekolojia ya Habari na Mawasiliano (Tehama) katika uendeshaji wa huduma za afya katika nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki (EAC). “ Maandalizi yameshafanyika kikao cha mwisho kilifanyika Burundi baada ya miaka kitafanyika Kenya tunatarajia Samia atalifungua Ukumbi wa Mikutano wa Mwalimu Julis Nyerere” amesema Profesa Kambi. Amebainisha kuwa kongamano hilo litakwenda sambamba na maonesho ya Tehama huku akiwasisitiza wananchi kushiriki kupata fursa zitakazowasilis...

Rais mpya wa DR Congo waamua kuunda Serikali ya muungano

Kiongozi mpya katika Jamhuri ya Kidmeokrasi ya Congo, Felix Tshisekedi na mtangulizi wake Joseph Kabila wamesema wameamua kuunda serikali ya muungano kufuatia mazungumzo, shirika la habari la AFP linaripoti. Share via Email Kwa mujibu wa Shirika la habari la BBC, Licha ya ushindi wa rais Tshisekedi — kiongozi huyo amejikuta akilazimika kugawanya uongozi tangu uchaguzi huo wa urais. Mpaka sasa hajafanikiwa kumteua waziri mkuu kutokana na kwamba muungano wa Kabila – Common Front for Congo (FCC) una uwingi katika bunge la taifa. Mkwamo huo umeweka kizuizi kwa maazimio ya Tshisekedi kuigeuza nchi hiyo inayogubikwa kwa rushwa na tuhuma za ukiukaji wa haki za binaadamu. Katika taarifa ya pamoja hapo jana Jumatano, Tshisekedi na Kabila wamesema kwamba licha ya “FCC kuwa na uwingi mkubwa bungeni” katika kuidhinisha matakwa yalioelezewa na wapiga kura, FCC na CACH wanaonesha uwajibikaji “wa malengo yao ya pamoja kuongoza pamoja kama sehemu ya serikali ya muungano” lina...