Skip to main content

KAMATI YA KUDUMU YA MIUNDOMBINU YATOA NENO KWA WIZARA

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu imeishauri Serikali kupitia Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kupeleka fedha kwa mkandarasi anayejenga barabara ya Mtwara - Newala - Masasi (KM 210), sehemu ya Mtwara - Mnivata yenye urefu wa KM 50 ili kuongeza kasi ya ujenzi wa mradi huo.

Kamati hiyo imeonesha kutokuridhishwa na kasi ya mradi huo ambao mpaka sasa ujenzi wake umefikia asilimia 47 kwa sababu changamoto ya fedha kutolipwa kwa wakati.

Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Moshi Selemani Kakoso, amezungumza hayo wakati wa majumuisho ya ziara ya ukaguzi wa miundombinu mkoani Mtwara jana ambapo walitembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa barabara hiyo unaojengwa na mkandarasi Dott Services kwa gharama ya zaidi ya shilingi bilioni 89.

"Kama kamati sijaridhishwa na maendeleo ya mradi huu na sababu kubwa ya kucheleweshwa imesemwa hapa ni kuchelewa kwa malipo ya mradi huu, hali hii itachelewesha maendeleo katika mikoa hii hivyo Wizara mjitahidi fedha zije ili mradi ukamilike na wananchi wapate maendeleo' amesema Mwenyekiti Kakoso.

Aidha kamati imetoa wito kwa Serikali katika kuuendeleza mkoa huo hasa katika uimarishaji wa miundombinu ya barabara ili kuunganisha mkoa huo na mikoa jirani na kurahisisha usafirishaji wa korosho zinazolimwa mkoani humo.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Wizara hiyo anayesimamia masuala ya ujenzi, Mhe. Elias Kwandikwa ameihakikishia kamati hiyo wizara itatenga fedha katika bajeti ya mwaka 2019/20 ili ziweze kulipa madeni yanayodaiwa na mkandarasi huyo na mradi huo ukamilike ili kukuza uchumi wa mkoa na nchi kwa ujumla kupitia barabara hiyo.

Awali akitoa taarifa ya mradi huo kwa kamati, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Barabara na Mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Sekta ya Ujenzi, Mhandisi John Ngowi, ameieleza kamati hiyo kuwa mkandarasi huyo anatakiwa kumaliza mradi mwezi Agosti mwaka huu na ameshaweka tabaka la kwanza la lami KM 8.5 na la tabaka la pili la lami KM 4.

Ameongeza kuwa mkandarasi amemaliza kazi ya ujenzi wa makalvati madogo 31, makalvati makubwa 4 na kazi zinaendelea ili kuhakikisha anakamilisha kwa kipindi cha mkataba.

Katika hatua nyingine, Kamati hiyo imetembelea na kukagua kiwanja cha ndege cha mtwara ambacho kipo katika hatua za awali za uboreshwaji wake ambapo Serikali imepandisha hadhi ya kiwanja hicho kutoka Daraja 3C kwenda Daraja 4E kwa viwango vya Shirika la Kimataifa la Usafiri wa Anga (ICAO).

Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Moshi Kakoso ameiagiza Seikali kumsimamia na kuhakikisha mkandarasi M/S Beijing Construction Engineering Group anaongeza kasi ya ujenzi ili aweze kukamilisha kwa wakati ambapo kazi zote zinatarajiwa kukamilika Mwezi Septemba, 2020.

Kamati pia imeielekeza Mamlaka ya Viwanja vya Ndege (TAA) kuhakiisha wanapata hati miliki ya viwanja vyote hapa nchini ili kuepusha migogoro na wananchi wanaovamia maeneo ya viwanja vya ndege.

Uboreshwaji wa Kiwanja cha Ndege cha Mtwara ukikamilika utaimarisha usafiri wa anga, huduma za kibiashara, na kuchochea shughuli mbalimbali za ukuaji wa kiuchumi na kijamii katika ukanda wa kusini mwa nchi.

Kamati imeipongeza Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) kwa kutekeleza mradi wa upanuzi wa gati ya mtwara na kusisitiza mradi huo usimamiwe kwa kuzingatia kanuni na taratibu za utekelezaji wa mradi.
1
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Barabara na Mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Sekta ya Ujenzi, Mhandisi John Ngowi, akitoa taarifa kwa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu maendeleo ya ujenzi wa barabara ya Mtwara-Mnivata yenye urefu wa KM 50, wakati kamati hiyo ilipotembelea mradi huo, Mkoani Mtwara.
2
Naibu Waziri wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi) Elias Kwandikwa, akifafanua jambo kwa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu hatua za maendeleo ya ujenzi wa barabara ya Mtwara-Mnivata yenye urefu wa KM 50, wakati kamati hiyo ilipotembelea mradi huo, Mkoani Mtwara.
3
Muonekano wa hatua ya ujenzi wa barabara ya Mtwara-Mnivata KM 50 kwa kiwango cha lami. Ujenzi wa barabara hiyo umefikia asilimia 47 na utagharamu zaidi ya shilingi bilioni 89.
4
Meneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS) mkoa wa Mtwara, Eng. Dotto Chacha, akifafanua jambo kwa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, wakati kamati hiyo ilipotembelea mradi wa ujenzi wa barabara ya Mtwara-Mnivata KM 50 kwa kiwango cha lami, mkoani humo. Wa tatu kushoto ni Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Moshi Selemani Kakoso.
5
Mkurugenzi wa Viwanja vya Ndege kutoka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Eng Emmanuel Raphael, akitoa taarifa kwa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu hatua za awali za uboreshwaji wa Kiwanja cha Ndege cha Mtwara kutoka Daraja 3C kwenda Daraja 4E, wakati kamati hiyo ilipotembelea mradi huo, mkoani Mtwara.
6
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Eng. Desusdedit Kakoko, akifafanua jambo kwa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu maendeleo ya upanuzi wa bandari ya Mtwara, wakati kamati hiyo ilipotembelea mradi huo, Mkoani Mtwara.

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...