Skip to main content

MUSSA: WATU WALIKUWA WANAIPA NIGERIA NAFASI YA KUSHINDA LAKINI MAMBO YAMEKUA TOFAUTI



Ahmed Mussa, nahodha wa timu ya Taifa ya Nigeria 'Super Eagles'
Ahmed Mussa, nahodha wa timu ya Taifa ya Nigeria ‘Super Eagles’
Nahodha wa Nigeria Ahmed Mussa amesema, soka la sasa halina timu kubwa wala ndogo. Huku akisema kwamba watu walikuwa wakiipa nafasi kubwa Nigeria ya kushinda kwenye mchezo wao dhdi ya Stars lakini mambo yamekuwa tofauti
“Mchezo wetu umemalizika vizuri na sasa uaweza kuona kwamba hakuna timu ndogo wala kubwa kwenye mchezo wa soka. Watu walikuwa wanasema Nigeria ni taifa kubwa kimpira ukilinganisha na Tanzania huku wakitupa sisi nafasi ya kushinda mchezo wa leo  lakini mambo yamekua tofauti”.
“Kocha bado anatengeneza timu yake naamini baada ya mechi kadhaa tutakuwa vizuri japo nimefurahi kwa jinsi tulivyocheza leo. Kipindi cha kwanza tulishikwa lakini kipindi cha pili tukacheza vizuri”.Inatoka http://shaffihdauda.co.tz

Comments