Skip to main content

Diego Costa kukosa mechi tatu


Costa akimkwaruza Koschielny usoni
Costa akimkwaruza Koscielny usoni
Diego Costa atakosa michezo mitatu baada ya chama cha soka cha England FA kuthibitisha kukutwa na makosa.
Costa alikana mashtaka yaliyokuwa yakimkabili kuhusiana na kumfanyia fujo mlinzi wa Arsenal Laurent Koscielny katika ushindi wa goli 2-0 dhidi ya Arsenal.
Na kisha kumsukuma chini
Na kisha kumsukuma chini
Costa mwenye miaka 26 alionekana kuweka mikono yake juu ya uso wa Koscielny kabla ya kuanza kuzozana na Gabriel Paulista ambaye baadaye alitolewa nje kwa kadi nyekundu.
Mlinzi huyo wa Arsenal alitolewa nje na mwamuzi Mike Dean kwa kumfanyia vurugu mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Hispania.
Costa akikwaruzana na Gabriel ambaye alionyeshwa kadi nyekundu baadae
Costa akikwaruzana na Gabriel ambaye alionyeshwa kadi nyekundu baadae
Costa atakosa mchezo wa kombe la ligi dhidi ya Walsall siku ya jumatano sambamba na ile ya ligi kuu kati ya Newcastle na Southampton.
Baada ya kuthibitisha kuwa mwamuzi wa mchezo hakuona tukio la Costa na Koscielny, chama cha soka England kimesambaza kanda hizo za vidio kwa waamuzi wakongwe watatu wa zamani.
Chanzo: BBC Swahili

Comments