Skip to main content

CCM: Hatushangai

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimeeleza kutoshangazwa na matokeo ya utafiti wa taasisi huru ya Twaweza yaliyotoa ushindi wa asilimia 65 kwa Mgombea Urais wao, Dk John Magufuli, huku kikiahidi kuongeza kasi, nguvu na mikakati zaidi katika nusu ya pili ya kampeni.
Hata hivyo, kimeshangazwa na taharuki hasa kutoka miongoni mwa wasomi na wanaharakati, kuhusu matokeo ya utafiti huo na kusema kilitegemea wasomi na wanaharakati hao wangefurahia utamaduni wa tafiti za kisiasa ulioanza kujitokeza nchini kwa vile unajenga.
Pia kimesisitiza kuwa kimethibitisha kushiriki mdahalo wa wagombea urais ulioandaliwa na Baraza la Habari Tanzania (MCT), lakini kikisitiza uwashirikishe wagombea wenyewe na si wawakilishi wao, na pia wagombea wote, hasa wa vyama vikuu wawepo na washiriki.
Juzi, Taasisi ya Twaweza ilitoa matokeo ya utafiti wake kuhusu ‘Sauti za Wananchi’ kwenye siasa na kuonesha kuwa, kama uchaguzi huo ungefanyika juzi, Dk Magufuli angeibuka mshindi wa asilimia 65 na Mgombea wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Edward Lowassa ambaye ana asilimia 25.
Pia Twaweza katika utafiti huo, ilisema wahojiwa hao walipoulizwa wanajisikia kuwa karibu zaidi na chama gani, asilimia 62 walisema wako karibu na CCM huku Chadema ikipata asilimia 25 na vyama vingine vikiambulia asilimia zilizobaki.
Katika utafiti huo uliofanywa mapema Agosti hadi Septemba mwanzoni mwaka huu, wahojiwa waliulizwa swali ni mgombea yupi watampigia kura na kwa nini, na majibu yalikuwa asilimia 26 walisema watampigia Magufuli kwa sababu ni mchapakazi huku asilimia 12, walisema watampigia Lowassa kwa sababu ya kutaka mabadiliko.
CCM haikushangazwa
Akizungumzia matokeo hayo, Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (NEC) ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati ya Kampeni ya CCM, January Makamba alisema CCM haikushangazwa na matokeo ya utafiti huo ambao umeibua mjadala mkubwa miongoni mwa jamii wakiwamo wasomi na wanaharakati.
“Hatukushangazwa na matokeo ya utafiti huu kwa sababu tano; moja; siku Ukawa walipomteua Lowassa kuwa mgombea wao ndio siku CCM ilipohakikishiwa ushindi katika uchaguzi wa mwaka huu.
CCM hatukumteua kwa sababu tuliamini hakuna namna ambapo Watanzania wengi watamchagua,” January aliwaambia waandishi wa habari jana Dar es Salaam. Aliitaja sababu ya pili kuwa CCM inafanya utafiti wa ndani wa kisayansi kila wiki kujua mwenendo na mwelekeo wa kampeni na maeneo yanayohitaji nguvu mahsusi na kwamba tangu utafiti huo uanze mwishoni mwa Agosti, karibu kila wiki asilimia za ushindi wa CCM hazijawahi kushuka chini ya asilimia 60 na zimekuwa zikipanda.
Tatu; alisema kazi kubwa anayofanya mgombea wa CCM, Magufuli na Mgombea Mwenza Samia Suluhu Hassan, kuzunguka nchi nzima kwa barabara na kuzungumza moja kwa moja na wapiga kura inazaa matunda kutokana na kuwafikia wapiga kura wengi, hasa wa vijijini, na wapiga kura wanawaelewa.
Aliitaja sababu ya nne kuwa ni kutokana na kampeni kubwa zinazofanywa na wagombea ubunge na udiwani wa CCM na makada na viongozi wa chama hicho katika ngazi zote za nchi nzima kila siku kumuombea kura Magufuli, na kampeni hizo kuzaa matunda.
Kuhusu sababu ya tano, January alisema “Tunaamini pia migogoro ndani ya Ukawa katika kipindi hiki cha uchaguzi iliyopelekea mitafaruku katika kuachiana majimbo na baadaye, kutokana na uteuzi wa Mgombea Urais wa Ukawa, kusababisha kujiuzulu kwa Profesa Ibrahim Lipumba na Dk Willbrod Slaa, na migongano ndani ya NCCR- Mageuzi, ambayo yote yamepunguza imani ya wananchi kwa vyama hivyo.”
Taharuki ya wasomi Akizungumzia wasomi, January ambaye pia ni Mgombea Ubunge Jimbo la Bumbuli mkoani Tanga, alisema CCM imeshangazwa na taharuki hasa kutoka miongoni mwa wasomi na wanaharakati kuhusu matokeo ya utafiti huo.
“CCM ilitegemea kwamba jamii ya wasomi na wanaharakati ingefurahia utamaduni wa tafiti za kisiasa unaoanza kujitokeza hapa nchini ili siku zijazo tujikite katika kurekebishana kwenye kanuni za utafiti na ithibati na uhakiki wa ubora,” alieleza January na kutoa mfano wa utafiti wa Sinovate mwaka 2010 ambao ulionesha kuwa Rais Jakaya Kikwete angeshinda kwa asilimia 61, na kweli akapata asilimia 61.17 kushinda muhula wa pili na wa mwisho.
“Tunasikitika kwamba yanawekwa mazingira ya kutisha na kukatisha tamaa kwa watu wanaotaka kufanya tafiti za kisiasa nchini. Utafiti ni sayansi, na matokeo ya utafiti hupingwa kwa matokeo ya utafiti mwingine, si kwa kuponda tu au kwa matusi na vitisho.
Ni vyema tukajifunza kupokea habari ambayo haikufurahishi bila taharuki.” Kasi, mikakati kuongezeka Akizungumzia mwenendo wa kampeni, January alisema CCM inaridhika na mwenendo wa kampeni, na katika nusu ya pili ya kampeni itaongeza kasi na msukumo wa kuwafikia wananchi wengi zaidi kwa mbinu na mikakati mipya.
“Kwa kifupi, mgombea Urais Magufuli na mgombea mwenza Samia, wanaendelea vizuri na kampeni. Kila mmoja anafanya mikutano na wananchi kati ya minane na 11 kwa siku na kukutana na maelfu kwa maelfu ya wananchi.
“Tunawashukuru pia makada wa CCM wanaojitolea kwa hali na mali kukipigania Chama Cha Mapinduzi na kumtafutia kura Ndugu Magufuli,” alisema. Midahalo ya wagombea Kwa upande wa midahalo ya wagombea, alisema CCM imeshangazwa na kauli ya Baraza la Habari Tanzania (MCT) kupitia kwa Katibu Mtendaji wake, Kajubi Mukajanga kwamba CCM haijathibitisha kushiriki mdahalo.
Akifafanua kilichotokea, January alisema; “CCM ilipokea mwaliko wa MCT na kuijibu kwa barua ya tarehe 13 Septemba 2015 yenye kumbukumbu CCM/ OND/M/190/132 iliyosainiwa na Stephen Msami ambaye ni Msaidizi wa Katibu Mkuu, ikithibitisha kushiriki mdahalo.”
Alisema mbali ya hatua hiyo; CCM ilithibitisha kushiriki mdahalo huo kupitia vikao mbalimbali na kwamba kauli ya Mukajanga inalenga kuwasaidia kisiasa wale ambao hawajathibitisha au hawana nia ya kuthibitisha kushiriki.
“Kwa msingi huu, tunaamini ni vyema mdahalo huu ukaandaliwa na ushirika wa taasisi mbalimbali zilizokuwa na nia ya kuandaa midahalo kama vile UDASA, Twaweza na nyinginezo ili kuiondolea uwezo taasisi moja au kikundi cha watu wachache, kuhodhi na kuwa na ukiritimba kwenye jambo hili kubwa na muhimu.
“CCM inapenda kusisitiza kwamba Magufuli amekubali kushiriki mdahalo wa wagombea Urais, mdahalo uwashirikishe wagombea wenyewe na si wawakilishi wao na wagombea wote, hasa wa vyama vikuu, wawepo na washiriki,” alisema January.
ACT yafarijika Kwa upande wake, Chama cha ACTWazalendo kimesema mbali ya kuchelewa kutangaza wagombea wa nafasi mbalimbali za uongozi, lakini kinafarijika kuwa chama pekee nje ya vyama vingine vya siasa kutajwa na wapiga kura zaidi ya asilimia moja katika matokeo ya utafiti wa Twaweza.
Kimesema kupitia utafiti huo, chama hicho kimeonekana kuwa cha nne katika kukubalika kwa wapiga kura nyuma ya CCM, Chadema na CUF. Kadhalika kimesema hadi sasa kimekusanya fedha Sh milioni 365 na kutumia Sh milioni 363 huku kikiri kuwa na upinzani mkubwa katika majimbo 89 wakihitaji nguvu ya ziada.
Akizungumza jana Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi na Kampeni Taifa, Nixon Tugara alisema katika utafiti wa Twaweza unaonesha kuwa chama hicho hakikufanya vizuri na kwamba bado wana kazi kubwa ya kuwafikia wapiga kura katika muda uliobakia wa kampeni.
“Licha ya kuonesha hali hiyo, sisi ACT Wazalendo tunafarijika kwamba chama kimekuwa chama pekee nje ya CCM na vyama vinavyounda Ukawa kilichotajwa na wapiga kura,” alisema Tugara.
Alisema kutokana na kufanya vizuri katika kampeni na bidii kubwa ambayo mgombea urais wa chama hicho na wagombea wengine wamekuwa wakifanya, wanaamini kuwa utafiti ungefanyika leo wangefanya vizuri zaidi.
Tugara alitoa mwito kwa wagombea wa chama hicho popote walipo kuchukulia matokeo ya utafiti huo kama changamoto ya kuongeza bidii zaidi katika kampeni zao. Kadhalika aliwahimiza wagombea na makampeni meneja na viongozi wa chama kuwekeza nguvu zaidi kwa makundi ya wananchi ambayo katika utafiti huo yanaonekana bado kuunga mkono chama tawala.
Alitoa mwito kwa taasisi nyingine kufanya tafiti nyingine kabla ya Uchaguzi Mkuu kwa kuwa wanatambua utafiti ni moja ya maoni ya wananchi kuhusu siasa, ingawaje hawawezi kubashiri hali itakavyokuwa siku ya uchaguzi.
Kuhusu kampeni alisema tayari uongozi wa chama hicho umefika mikoa zaidi ya 10 na kuendelea kuwa na mtandao mpana hali ambayo ilisababisha kusimamisha wagombea wengi zaidi ya vyama vingine ukiondoa CCM. Imeandikwa na Oscar Mbuza na Lucy Lyatuu.CHANZO:HABARI LEO

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.