Skip to main content

Magufuli: Epukeni matapeli wa kisiasa


Mgombea Urais kupitia CCM, Dk John Magufuli akihutubia wakazi wa Mtwara mjini kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika kwenye Uwanja wa Mashujaa mjini humo jana. (Picha na Adam Mzee).ningehangaa
MGOMBEA Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia CCM, Dk John Magufuli, amewataka Watanzania kuwa makini wasije kudanganywa na matapeli wa kisiasa watakaokuja na ahadi za uongo.
Akizungumza katika Uwanja wa Mashujaa mjini Mtwara jana, Dk Magufuli alisema matapeli hao watakuja na ahadi nyingi, akawataka wananchi wawasikilize na kuwapima kwa kauli na sifa zao kwa kuwa kuahidi ni rahisi kuliko kutekeleza.
“Tusije tukadanganywa na matapeli wa kisiasa, wakinamama mnafahamu matapeli wa mjini walivyo na maneno matamu. Maendeleo ni changamoto na yataletwa na sisi Wanamtwara,” alisema.
Miongoni mwa matazamio ya Dk Magufuli ya Serikali atakayoiongoza kama akichaguliwa kuwa rais, ni ujenzi wa reli ya kisasa kutoka Mtwara kupitia Songea mpaka Mbambabay, baada ya kuboresha Bandari ya Mtwara na kuwa ya kisasa kama ya Dar es Salaam.
Alisema bandari itaboreshwa ili pia iongeze ajira kwa wakazi wa mji huo huku mizigo ya nchi za Zambia na Malawi, ikipitia mkoani humo.
Aidha, alisema Serikali ya Awamu ya Tano atakayoiongoza, itajielekeza zaidi katika kukuza uchumi kwa watu. Akizungumza katika mikutano mikubwa na midogo katika wilaya za Newala, Tandahimba na Mtwara Vijijini kuhusu zao la korosho, Dk Magufuli alisema katika uongozi wake, lazima korosho ilete uchumi mzuri kwa wakazi wa Mtwara.
“Mimi shahada yangu ya tatu (PHD) nimesomea korosho. Hakuna anayeweza kunidanganya. Korosho siyo tu tunda la ndani, bali hata ganda ni uchumi kwa kuwa linatengeneza gundi na dawa ya kuzuia kutu,” alisema Dk Magufuli.
Alisema korosho ya Tanzania ni tofauti na korosho nyingine duniani, kwa kuwa yenyewe huanza kuvunwa wakati maeneo mengine duniani wamemaliza kuvuna.
Kwa mujibu wa Dk Magufuli, katika uongozi wake hataruhusu korosho kuuzwa ghafi nje ya nchi, bali Serikali itahakikisha kunajengwa viwanda vitakavyotumia malighafi ya korosho ili zao hilo lipande bei.
Kuhusu tatizo la stakabadhi ghalani ambalo limekuwa likilalamikiwa na wakulima, Dk Magufuli alisema wamuachie yeye atahakikisha kero ya mfumo huo inaondoshwa na wakulima hawadhulumiwi haki yao.
Akiwa Mtwara vijijini, alisema Tanzania imegundua gesi mkoani Mtwara, hivyo akaahidi kuhakikisha gesi hiyo inaanza kunufaisha wakazi wa Mtwara kabla ya kunufaisha wananchi wa mikoa mingine.
Katika hilo, alisema atasimamia ujenzi wa viwanda vikubwa, vya kati na vidogo, ili vitoe ajira kwa vijana wa Mtwara, ambao watakuwa wamesoma katika shule mbalimbali, ambazo kuanzia mwakani kutoka shule ya awali mpaka kidato cha nne, itakuwa bure.
Awali kabla ya kutoa ahadi hizo na zingine nyingi katika sekta mbalimbali, Mjumbe wa Kamati Kuu (CC) ya Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, William Lukuvi, alisema Dk Magufuli ndiye mgombea pekee wa urais kwa sasa aliyetembea kwa barabara umbali mrefu.
Kwa mujibu wa Lukuvi, Dk Magufuli ambaye amemaliza awamu ya kwanza ya ziara ya kampeni katika mikoa saba, kutoka Katavi, Rukwa, Songwe, Mbeya, Njombe, Ruvuma na kumalizia Mtwara jana kwa barabara, pia ndiye mgombeapekee wa urais aliyechaguliwa katika mchakato bora na ulio wazi.
“Wako wanaodai kulikuwa na mizengwe wakati wa kumpata mgombea wa CCM. Ngoja niwaambie, walikuwa wagombea 38, tukachuja mpaka wakabakia watano na Magufuli akiwepo. Tukachuja tena katika mchakato wa wazi mpaka watatu na Magufuli akawepo na wakati wa kumpata mmoja, ambaye ndiye Magufuli, mchakato ulirushwa moja kwa moja na televisheni nchi nzima.“Sasa tuwaulize wenzetu walikuwa wangapi na walimpataje huyo mgombea wao, mbona hatukuwaona?” Alihoji na kuongeza kuwa Dk Magufuli ni mgombea safi na hata marafiki zake si wa hovyo na watu wa hovyo wanaogopa kumkaribia.
Lukuvi alisema kama Watanzania wanataka bora rais, basi huyo si Dk Magufuli, lakini kama wanataka rais bora, basi kati ya wagombea wote wa urais, hakuna aliye bora kama Dk Magufuli.

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.