Skip to main content

SHULE YA MSINGI KIBINDU HATARINI KUFUNGIWA

Mbunge wa Jimbo la Chalinze, Ridhiwani Kikwete akikagua vyumba vya madarasa vya Shule ya Msingi Kibindu, wilayani Bagamoyo, Pwani vilivyobmoka na kuezuliwa paa kutokana na mvua kubwa iliyonyesha hivi karibuni.
SHULE ya msingi Kibindu,Chalinze wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani,ipo hatarini kufungiwa kutokana na vyumba vya madarasa kuanguka na miundombinu yake kuwa chakavu hivyo kuhofiwa kuhatarisha maisha ya wanafunzi na walimu.
Aidha shule hiyo imekuwa ikiezuliwa baadhi ya majengo yake mara kwa mara kutokana na kutofanyiwa ukarabati tangu shule hiyo ijengwe zaidi ya miaka 50 iliyopita.
Kutokana na hali hiyo wanafunzi wa shule hiyo wanakabiliwa na ukosefu wa vyumba vya madarasa vilivyo bora na imara hali inayosababisha wanafunzi 200 kulundikana katika chumba kimoja.
Akizungumzia hali hiyo mbunge wa jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete ambae yupo katika ziara ya siku 10 jimboni humo akitembelea maeneo mbalimbali ikiwemo shule hiyo ambayo baadhi ya majengo yake yameanguka ,alisema hayuko tayar kushuhudia wanafunzi wakiendelea kusoma katika mazingira ya hatari.
Ridhiwani alilazimika kutoa kauli hiyo baada ya kukagua madarasa hayo na kushuhudia vyumba vinne vinavyotumika kuwa hatarini kubomoka kutokana na kutawaliwa na nyufa.
"Nimesikitishwa sana na ningekuwa na uwezo ningeifunga hii shule isitumike kwani shule inafunguliwa tarehe 14 mwezi huu ,wanafunzi watakuja kusomea wapi ,wakati pia majengo yaliyobakia yanaweza kuanguka wakati wowowte pia,ni lazima juhudi za lazima zifanyike kuokoa maisha ya wanafunzi hawa" alisema Mbunge huyo.
Ridhiwani alisema kuwa atawsiliana na mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Bagamoyo Ibrahim Matovu ili waone ni namna gani wataweza kuelekeza nguvu zao katika shule hiyo ili iwe katika mazingira bora .
Diwani wa kata ya Kibindu Mawazo Mkufya alisema taarifa za uchakavu wa miundombinu ya shule hiyo tayari amezifikisha ngazi ya halmashauri, ambapo nae kwa upande wake aliomba shule hiyo ifungiwe ili ukarabati ufanyike
Mtendaji wa kijiji Cha Kibindu Juma Mgaza, alisema shule hiyo ina matatizo ya kuezuliwa mara kwa mara wakati wa mvua kutokana na miundombinu yake kuwa chakavu.
Mgaza aliitaka halmashauri ya wilaya hiyo kufanyia kazi changamoto hiyo kubwa ambayo ni hatarishi kwa wanafunzi.
Shule ya msingi Kibindu kwa sasa ina wanafunzi 907 wa darasa la kwanza hadi la saba ambao wanatarajia kuanza mhula wa masomo kwa mwaka 2015 wiki ijayo huku ikiwa na vyumba vinne kati ya 14 vinavyohitajika.
Mbali ya hayo vyumba vya madarasa vimeanguka na vingine vimeweka nyufa kubwa ambazo zinahofiwa kuanguka wakati wowowte na kusababisha athari kwa wanafunzi na walimu.VICTOR SIMON

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

RAIS WA ZANZIBAR DKT. SHEIN AFANYA MAHOJIANO NA MAMLAKA YA VITAMBULISHO VYA TAIFA

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt.Ali Moh amed Shein,alipokuwa akifanya mahojiano na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa kupitia ZBC TV na kutoa wito kwa Watanzania hasa wa Zanzibar kushiriki kikamilifu katika zoezi la uandikishaji vitambulisho hivyo,ambapo zoezi hilo  linatarajia kuwanza Oktoba 15 mwaka. Mazungumzo hayo yalifanyika Ikulu mjini Zanzibar leo,(kulia) Mtangazji wa ZBC TV Nasra Nassor. Picha na Ramadhan Othman,Ikulu

Uganda Police issue fresh terror alert

  By Chris Kiwawulo, The Police have issued a fresh terror alert against a possible attack on Uganda by four terrorists from Kazakhstan. Police spokesperson Judith Nabakooba “We have received a security notification in form of an orange notice of four terrorists originating from Kazakhstan who are planning to travel to foreign countries in order to commit attacks and participate in hostile acts,” Police spokesperson Judith Nabakooba said in a statement on Monday. Nabakooba named the four active members of radical organizations as; Nassiruauly Kairat, Umurzakov Marat Eskendirovich, Kovtun Denis Valerevich and Mazhibayen Alimzhan Akhlazhanovich. By press time, a search on the international web has not yielded anything on the named persons.Last evening, police said that in collaboration with other security agencies vigilance has been stepped up to avert the terrorists’ evil plans. Police have in the past issu...