Skip to main content

SHULE YA MSINGI KIBINDU HATARINI KUFUNGIWA

Mbunge wa Jimbo la Chalinze, Ridhiwani Kikwete akikagua vyumba vya madarasa vya Shule ya Msingi Kibindu, wilayani Bagamoyo, Pwani vilivyobmoka na kuezuliwa paa kutokana na mvua kubwa iliyonyesha hivi karibuni.
SHULE ya msingi Kibindu,Chalinze wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani,ipo hatarini kufungiwa kutokana na vyumba vya madarasa kuanguka na miundombinu yake kuwa chakavu hivyo kuhofiwa kuhatarisha maisha ya wanafunzi na walimu.
Aidha shule hiyo imekuwa ikiezuliwa baadhi ya majengo yake mara kwa mara kutokana na kutofanyiwa ukarabati tangu shule hiyo ijengwe zaidi ya miaka 50 iliyopita.
Kutokana na hali hiyo wanafunzi wa shule hiyo wanakabiliwa na ukosefu wa vyumba vya madarasa vilivyo bora na imara hali inayosababisha wanafunzi 200 kulundikana katika chumba kimoja.
Akizungumzia hali hiyo mbunge wa jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete ambae yupo katika ziara ya siku 10 jimboni humo akitembelea maeneo mbalimbali ikiwemo shule hiyo ambayo baadhi ya majengo yake yameanguka ,alisema hayuko tayar kushuhudia wanafunzi wakiendelea kusoma katika mazingira ya hatari.
Ridhiwani alilazimika kutoa kauli hiyo baada ya kukagua madarasa hayo na kushuhudia vyumba vinne vinavyotumika kuwa hatarini kubomoka kutokana na kutawaliwa na nyufa.
"Nimesikitishwa sana na ningekuwa na uwezo ningeifunga hii shule isitumike kwani shule inafunguliwa tarehe 14 mwezi huu ,wanafunzi watakuja kusomea wapi ,wakati pia majengo yaliyobakia yanaweza kuanguka wakati wowowte pia,ni lazima juhudi za lazima zifanyike kuokoa maisha ya wanafunzi hawa" alisema Mbunge huyo.
Ridhiwani alisema kuwa atawsiliana na mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Bagamoyo Ibrahim Matovu ili waone ni namna gani wataweza kuelekeza nguvu zao katika shule hiyo ili iwe katika mazingira bora .
Diwani wa kata ya Kibindu Mawazo Mkufya alisema taarifa za uchakavu wa miundombinu ya shule hiyo tayari amezifikisha ngazi ya halmashauri, ambapo nae kwa upande wake aliomba shule hiyo ifungiwe ili ukarabati ufanyike
Mtendaji wa kijiji Cha Kibindu Juma Mgaza, alisema shule hiyo ina matatizo ya kuezuliwa mara kwa mara wakati wa mvua kutokana na miundombinu yake kuwa chakavu.
Mgaza aliitaka halmashauri ya wilaya hiyo kufanyia kazi changamoto hiyo kubwa ambayo ni hatarishi kwa wanafunzi.
Shule ya msingi Kibindu kwa sasa ina wanafunzi 907 wa darasa la kwanza hadi la saba ambao wanatarajia kuanza mhula wa masomo kwa mwaka 2015 wiki ijayo huku ikiwa na vyumba vinne kati ya 14 vinavyohitajika.
Mbali ya hayo vyumba vya madarasa vimeanguka na vingine vimeweka nyufa kubwa ambazo zinahofiwa kuanguka wakati wowowte na kusababisha athari kwa wanafunzi na walimu.VICTOR SIMON

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.