Skip to main content

Lema, Nassari wadai watamtoa Muhongo bungeni kwa mabavu


Mbunge wa Arusha mjini (Chadema) Godbless Lema
Mbunge wa Arusha mjini (Chadema) Godbless Lema
Mbunge wa Arusha mjini (Chadema) Godbless Lema amesema atamtoa kwa mabavu bungeni Waziri wa nishati na madini,Profesa Sospetre Muhongo katika kikao kijacho cha Bunge endapo atakuwa hajaondolewa kwenye nafasi hiyo.
Mkakati huo wa Lema umeungwa mkono na Mbunge wa Arumeru Mashariki (Chadema), Joshua Nassari ambaye pia amepanga kumtoa bungeni kwa nguvu, Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Bajeti, Andrew Chenge.
“Keshokutwa nakwenda bungeni kufanya kazi moja tu, nikimkuta Muhongo bungeni ndipo nitafukuzwa ubunge moja kwa moja,” alisema Lema huku akishangiliwa wananchi na kuongeza; “Nikimkuta Muhongo bungeni na Chenge bado ni viongozi mimi nitakwenda kumshika Muhongo nimtoe bungeni kwa sababu Katiba inaruhusu kila raia kukemea uovu.”
Profesa Muhongo na Chenge ni miongoni mwa viongozi ambao Bunge liliazimia wawajibishwe na mamlaka zao kutokana na kashfa ya uchotwaji mamilioni ya fedha katika Akaunti ya Tegeta Escrow.
Hata hivyo, wakati Rais Jakaya Kikwete akilihutubia Taifa, Desemba 22 mwaka jana kupitia wazee wa Dar es Salaam, alitangaza kumweka kiporo Profesa Muhongo kwa siku mbili au tatu, ahadi ambayo haijatekelezwa.
Tayari Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Jaji Frederick Werema anayehusishwa na sakata hilo alishatangaza kujiuzulu na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka akifutwa kazi.
Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo.
Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo.
Kauli ya Lema
Akihutubia mkutano wa hadhara uliofanyika juzi katika Viwanja vya Relini mjini Moshi, Lema alisema Januari 27 mwaka huu ataingia bungeni akiwa na lengo moja tu la kumtoa kwa mabavu, Profesa Muhongo.
“Eti Tibaijuka kapewa tu bilioni moja kaondoka, waziri mwenye dhamana hajavuliwa nyadhifa. Rais Kikwete vipi?” alihoji.
Lema alidai kwamba sakata hilo, katibu binafsi wa Rais ambaye hata hivyo hakumtaja kwa jina, ndiye aliyeandika barua kuruhusu fedha za escrow zitoke lakini hadi sasa yuko salama na hajawajibishwa.
Pia, alihoji sababu za Jaji Werema kutofikishwa mahakamani wakati ndiye aliyefanya makosa katika kutoa ushauri uliozaa sakata la escrow badala yake watu wadogo ndiyo wanashtakiwa.
“Leo tunaona watu wanapelekwa mahakamani, Rais Kikwete nikuulize swali, ulisema siyo fedha za Serikali ni za watu binafsi mbona mnashika watu mnawapeleka mahakamani?” alihoji Lema.
Alisema Sh306 bilioni za escrow zingeweza kujenga nyumba 15,000 za walimu, kununua mashine 300 za CT -Scan na kujenga barabara ya lami yenye urefu wa kilomita 600 lakini zimeliwa na wachache.
Kauli ya Nassari
Akihutubia, Nassari alisema yupo bega kwa bega na Lema katika kumtoa kwa nguvu bungeni Profesa Muhongo, huku akisema Bunge lijalo litawaka moto.
“Lema umesema hapa ukimkuta Muhongo bungeni uko tayari kuvuliwa ubunge na mimi si mdogo wako? Tuko pamoja,” alisema na kuongeza:
“Nitamwambia Lema kaba kule na wewe Sugu (Joseph Mbilinyi, Mbunge wa Mbeya Mjini) kaba kule halafu mimi narukia pale kwenye Siwa, tunaondoa Siwa tutamfuata Muhongo alipo,” alisema.
Nassari aliwataka wananchi wa Moshi kufuatilia kikao hicho cha Bunge na akisema haiwezekani maazimio ya Bunge yasitekelezwe kwa ukamilifu wake na kwa wakati.
Chanzo: Mwananchi

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.