Skip to main content

Ubakaji watumiwa kama silaha Libya?


Kiongozi wa Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) amesema kuwa kuna ushahidi kwamba kiongozi wa Libya, Kanali Muammar Gaddafi, aliamuru kubakwa kwa mamia ya wanawake kama silaha ya kupambana na waasi nchini mwake.

Wanajeshi wakiuzingira mji wa Misrata

Luis Moreno-Ocampo alisema kuwa ubakaji ni mbinu mpya inayotumiwa na Kanali Gaddafi katika ugandamizaji.

Alisema kuna uwezekano mkubwa kuwa wanajeshi waaminifu kwa Kanali Gaddafi walipewa madawa kama vile Viagra ili kunoa uchu wao wa kuwabaka wanawake.

Hadi kufikia sasa Serikali ya Libya haijasema lo lote kuhusu madai hayo.

Kanali Gaddafi

Mwezi uliopita, Bwana Moreno-Ocampo aliomba majaji wa mahakama hiyo ya ICC kutoa amri ya kuwakamata Kanali Gaddafi, mwanawe Saif al-Islam, na kiongozi wa Ujasusi nchini humo Chifu Abdullah al-Sanussi.

Aliwalaumu kwa kutekeleza uhalifu mara mbili dhidi ya binadamu - mauaji na mateso. Alisema watu hao watatu ndio wanaopaswa kujitwika lawama zote za mashambulizi dhidi ya raia tangu mwanzo wa maasi dhidi ya Serikali yaliyoanza Februari, wakati kati ya watu 500 na 700 wanadaiwa kuuawa.

Serikali ya Libya haitambui mamlaka ya mahakama ya ICC.

Mfumo mpya wa ugandmizaji

Mnamo Jumatano, Bwana Moreno-Ocampo alisema kuwa amri za kuwakamata zikitolewa huenda akaongezea mashtaka ya ubakaji juu ya yale mengine.

Aliwambia waandishi wa habari katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa mjini New York kuwa amekusanya ushahidi unaoonyesha kuwa kiongozi huyo wa Libya aliamua kuwaadhibu wanawake kwa kutumia ubakaji kama silaha kwa matumaini kuwa hatua hiyo itawatisha wananchi wengine wasiasi dhidi yake.

Hajawahi kutumia utaratibu huu kuwathibiti wananchi. Ubakaji ni sera yake mpya ya ugandamizaji. Hiyo ndiyo sababu mwanzoni tulikuwa na tashwishi lakini sasa tumeanza kushawishika

Luis Moreno Ocampo

Alieleza kuwa ni vigumu kujua kiwango kamili cha ubakaji kilichotekelezwa.

"Katika maeneo mengine watu wanaozidi 100 walibakwa. Jambo tunalojaribu kuamua hivi sasa ni iwapo Gaddafi anapaswa kujitwika lawama ya ubakaji huu au vitendo hivyo vilifanywa na wanajeshi wenyewe katika kambi zao," alifafanua.

Bwana Moreno-Ocampo alisema pia kuwa mashahidi kadhaa walithbitisha kwamba Serikali ya Libya ilinunua madawa aina ya Viagra katika vifurushi vikubwa vikubwa ili kutekeleza sera hiyo na "kuchochea uwezakano wa ubakaji."

"Tunajaribu kuchunguza ni akina nani walihusika katika maamuzi hayo," aliongezea.

Mnamo Machi, mwaka huu, mwanamke mmoja raia wa Libya, Eman al-Obeidi, aligonga vichwa vya habari alipoingia kwa ghafula kwenye hoteli moja mjini Tripoli na kusema kuwa alikuwa amebakwa na wanajeshi waaminifu kwa Kanali Gaddafi. Anaendelea kupata nafuu katika kambi moja ya wakimbizi nchini Romania.Chanzo ni www.bbckiswahili.

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...

Uganda Police issue fresh terror alert

  By Chris Kiwawulo, The Police have issued a fresh terror alert against a possible attack on Uganda by four terrorists from Kazakhstan. Police spokesperson Judith Nabakooba “We have received a security notification in form of an orange notice of four terrorists originating from Kazakhstan who are planning to travel to foreign countries in order to commit attacks and participate in hostile acts,” Police spokesperson Judith Nabakooba said in a statement on Monday. Nabakooba named the four active members of radical organizations as; Nassiruauly Kairat, Umurzakov Marat Eskendirovich, Kovtun Denis Valerevich and Mazhibayen Alimzhan Akhlazhanovich. By press time, a search on the international web has not yielded anything on the named persons.Last evening, police said that in collaboration with other security agencies vigilance has been stepped up to avert the terrorists’ evil plans. Police have in the past issu...