Skip to main content

Ubakaji watumiwa kama silaha Libya?


Kiongozi wa Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) amesema kuwa kuna ushahidi kwamba kiongozi wa Libya, Kanali Muammar Gaddafi, aliamuru kubakwa kwa mamia ya wanawake kama silaha ya kupambana na waasi nchini mwake.

Wanajeshi wakiuzingira mji wa Misrata

Luis Moreno-Ocampo alisema kuwa ubakaji ni mbinu mpya inayotumiwa na Kanali Gaddafi katika ugandamizaji.

Alisema kuna uwezekano mkubwa kuwa wanajeshi waaminifu kwa Kanali Gaddafi walipewa madawa kama vile Viagra ili kunoa uchu wao wa kuwabaka wanawake.

Hadi kufikia sasa Serikali ya Libya haijasema lo lote kuhusu madai hayo.

Kanali Gaddafi

Mwezi uliopita, Bwana Moreno-Ocampo aliomba majaji wa mahakama hiyo ya ICC kutoa amri ya kuwakamata Kanali Gaddafi, mwanawe Saif al-Islam, na kiongozi wa Ujasusi nchini humo Chifu Abdullah al-Sanussi.

Aliwalaumu kwa kutekeleza uhalifu mara mbili dhidi ya binadamu - mauaji na mateso. Alisema watu hao watatu ndio wanaopaswa kujitwika lawama zote za mashambulizi dhidi ya raia tangu mwanzo wa maasi dhidi ya Serikali yaliyoanza Februari, wakati kati ya watu 500 na 700 wanadaiwa kuuawa.

Serikali ya Libya haitambui mamlaka ya mahakama ya ICC.

Mfumo mpya wa ugandmizaji

Mnamo Jumatano, Bwana Moreno-Ocampo alisema kuwa amri za kuwakamata zikitolewa huenda akaongezea mashtaka ya ubakaji juu ya yale mengine.

Aliwambia waandishi wa habari katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa mjini New York kuwa amekusanya ushahidi unaoonyesha kuwa kiongozi huyo wa Libya aliamua kuwaadhibu wanawake kwa kutumia ubakaji kama silaha kwa matumaini kuwa hatua hiyo itawatisha wananchi wengine wasiasi dhidi yake.

Hajawahi kutumia utaratibu huu kuwathibiti wananchi. Ubakaji ni sera yake mpya ya ugandamizaji. Hiyo ndiyo sababu mwanzoni tulikuwa na tashwishi lakini sasa tumeanza kushawishika

Luis Moreno Ocampo

Alieleza kuwa ni vigumu kujua kiwango kamili cha ubakaji kilichotekelezwa.

"Katika maeneo mengine watu wanaozidi 100 walibakwa. Jambo tunalojaribu kuamua hivi sasa ni iwapo Gaddafi anapaswa kujitwika lawama ya ubakaji huu au vitendo hivyo vilifanywa na wanajeshi wenyewe katika kambi zao," alifafanua.

Bwana Moreno-Ocampo alisema pia kuwa mashahidi kadhaa walithbitisha kwamba Serikali ya Libya ilinunua madawa aina ya Viagra katika vifurushi vikubwa vikubwa ili kutekeleza sera hiyo na "kuchochea uwezakano wa ubakaji."

"Tunajaribu kuchunguza ni akina nani walihusika katika maamuzi hayo," aliongezea.

Mnamo Machi, mwaka huu, mwanamke mmoja raia wa Libya, Eman al-Obeidi, aligonga vichwa vya habari alipoingia kwa ghafula kwenye hoteli moja mjini Tripoli na kusema kuwa alikuwa amebakwa na wanajeshi waaminifu kwa Kanali Gaddafi. Anaendelea kupata nafuu katika kambi moja ya wakimbizi nchini Romania.Chanzo ni www.bbckiswahili.

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.