Skip to main content

Marando Adaiwa Kuruka Kuhusika Kumtuhumu Nape Kunufaika Na Mabilioni Ya Fedha Za EPA; Nape Amtaka Awaombe Radhi Watanzania


Nnauye








Katibu wa NEC, CCM Itikadi na Uenezi Taifa Nape Nnauye amedai kunasa barua za Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA na wakili maarufu nchini Mabere Marando akikana kuwaambia Watanzania kuwa Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi CCM, Nape Mnauye alifaidika na fedha za Mfuko wa Madeni ya Nje (EPA).

Amesema kutokana na kuupata ushahidi wa nyaraka hizo, anamtaka Marando kuchagua kufanya siasa au kuendelea na kazi yake ya uwakili kwa kuwa kuendelea na vyote kutamgharimu.

Nape aliyasema hayo jana kwenye mkutano mkubwa wa hadhara uliofanyika mjini hapa mkoani Rukwa na kuhudhuriwa na maelfu ya wakazi wa nji huo na vitongoji vyake.

“ Kimsingi namheshimu sana Marando lakini kitendo cha kuchanganya uwakili na siasa karibuni kitamgarimu, hasa siasa za majitaka za CHADEMA”, alisema Nape huku akishangiliwa na mamia ya wananchi waliofurika kwenye mkutano huo.

Nape alisema, hivi karibu alipomtaka Katibu Mkuu wa CHADEMA Dk. Wilibrod Slaa aache unafiki kwa kueleza kwanini analipwa na chama cheke sh. milioni 7.5 kwa mwezi tena bila kuzilipia kodi, wakati aliwahi kupinga wabunge kulipwa mshahara usiofikia kiasi hicho kuwa ni kubwa, badala ya kujibu yeye, CHADEMA ilimtumia Marando kutoa shutuma kuwa Nape naye ni miongoni mwa waliofaidika na fedha za EPA, hivyo ni fisadi.

Katika madai hayo Marando alidai Nape alipewa fedha hizo za wizi na mfanyabiashara Jayantkumar Patel ambaye kwa mujibu wa maelezo aliyokaririwa Marando na baadhi ya vyombo vya habari alidai Patel alimtaja Nape kwenye tume ya Rais ya iliyokuwa inashughulikia swala la EPA.

“Nilishituka kusikia yale maneno yakisemwa na mtu ninayemheshimu, nikajua ndio matatizo ya kuchanganya siasa na uwakili, siasa zenyewe za CHADEMA. Lakini cha ajabu baada ya siku chache Marando amemwandikia Jeetu Patel akikanusha taarifa ile na kuisukumia CHADEMA” Alisema Nape na kuongeza: “Nadhani ni muhimu Marando akachagua sasa kufanya siasa au kuendelea na kazi yake ya uwakili kabla aibu kubwa haijamkuta”.

Akionyesha kujiamini kuwa na nyakaraka za uthibitisho, Nape alisema anazo barua za mawasiliano kati ya Jeetu Patel na Marando zinazoonyesha Marando akikataa katakata kuhusika na kauli iliyonukuliwa kwenye vyombo vya habari kwamba Nape alinufaika na fedha za EPA.

Kwa mujibu wa Nape barua ya Jeetu Patel ya Mei 16, 2011 kwenda kwa Marando ikimtaka aeleze kwanini alimhusisha Nape na fedha za EPA huku akijua si kweli, huku barua nyingine ikiwa ya Marando ya tarehe hiyo hiyo, kwenda kwa Jeetu Patel akajitetea kwamba aliwashauri CHADEMA wasimshutumu Nape kwa EPA bila mafanikio, naye akaamua kuuaminisha uma jambo asiloliamini.

“Wananchi yapo mengi kama hili ambayo viongozi wa CHADEMA huwadanyeni kupitia kwenye mikutano au vyombo vya habari, lakini kwa kutojua baadhi yenu huwa mnawaami . Kitendo hiki kinamfanya Marando na chama chake wasiaminike kwa umma.

Nape alisema, bila aibu Marando anamkana Antoni Komu na Chama chake cha CHADEMA kuwa hakuunga mkono shutuma hizo dhidi ya Nape huku akijua wazi kuwa CHADEMA ilibidi wamtumie Marando kuwaeleza watanzania jambo ambalo hata yeye haliamini na kwamba kwa kufanya hivyo kwakuwa Marando ni wakili wa baadhi ya watuhumiwa wa kesi za EPA Watanzania wataamini kwa haraka.

“ Je wananchi tuendelee kumwamini Marando na chama chake?” Nape alihoji umati wa wananchi kwenye mkutano huo wakajibu “hawaaminiki hao”.

Nape alisema kutokana na kukana alichosema, sasa asimame na kuwaomba radhi Watanzania kwa kuwadangaya kuhusu tuhuma hizo. “Sasa namshauri kwanza atoke kuwaomba radhi watanzania kwa kuwadanganya katika hili na mengine mengi aliyotumiwa na CHADEMA kusema bila kuyaamini kama alivyofanya kwa hilo.


Nape alisema Marando aspoomba radhi Watanzania ataitoa hadharani barua husika ili Watanzania waisome waone unafiki wa Chadema na viongozi wake.

Kuhusu madai ya Chadema kwamba nchi haitatawalika, Nape alisema wanaodai nchi haitawaliki hawana mapenzi wala uchungu na nchi hii, ndo maana kwao hata nchi ikichafuka si tatizo ili mradi wanapata wanachotaka.

Aliwatahadharisha Watanzania kutohangaika na baba wa kambo wakati baba mzazi yupo. Akimaanisha vyama vya upizani ni baba wa kambo na CCM ndio baba mzazi.

Alisema mabadiliko makubwa yanayoendelea ndani ya CCM ndio matarajio ya watanzania kwa kuwa CCM inafahamu kuwa wasipoyapata watayatafuta nje na hapo CCM itakuwa imepoteza haki ya kuongoza nchi, hivyo ni muhimu wana CCM wakawapatia watanzania mabadiliko wanayoyataka.

Katika hatua nyIngine baadhi ya wananchi waliohudhuria mkutano huo, wamedai kwamba haijawahi kutokea mkutano wowote uliofanyika katika miaka ya karibuni mjini Mpanda kupata watu wengi kiasi cha waliohudhuria jana mkutano wa Nape.

“Chadema pia waliwahi kuja hapa juzi juzi, lakini kwa kweli umati huu wa aleo umevunja rekodi, wale hawakupata watu kama hawa” alisema mkazi mmoja wa mji huo, Samel Msakazi.

Naye Katibu wa NEC, Uchumi na Fedha Nchemba Mwigulu akizungumza kwenye mkutano huo aliwataka watanzania kutokubali kugawanywa na wanasiasa uchwara wanaotaka kuwatumia kwa malengo yao binafsi,bali waendelee kuienzi amani nchini ambayo imejengwa kwa muda mrefu.

Wajumbe hao wa sekretarite mpya ya CCM watamalizia ziara yao ya siku nne mkoani Rukwa jana asubuhi. (Imeandikwa na Bashiri Nkoromo kutoka Mpanda)

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them ...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Mwana muziki Marufu kwa jina la Chuck Brown Afariki Dunia Akiwa na umri wa miaka 75

View Photo Gallery — Chuck Brown dies at 75: The “godfather of go-go” has died By Chris Richards, Updated: Wednesday, May 16, 4:42 PM Chuck Brown, the gravelly voiced bandleader who capitalized on funk’s percussive pulse to create go-go, the genre of music that has soundtracked life in black Washington for more than three decades, died May 16 at the Johns Hopkins University hospital in Baltimore. He was 75. The death, from complications from sepsis, was confirmed by his manager, Tom Goldfogle. Mr. Brown had been hospitalized for pneumonia. Known as the “Godfather of Go-Go,” the performer, singer, guitarist and songwriter developed his commanding brand of funk in the mid-1970s to compete with the dominance of disco. Like a DJ blending records, Mr. Brown used nonstop percussion to stitch songs together and keep the crowd on the dance floor, resulting in marathon performances that went deep into the night. Mr. Brown said the style got its name because “the music j...