Skip to main content

0PERETIONI KAMATA SUKARI ...

Mkuu wa Kituo cha poliosi Himo Afande Majura( Kushoto) akimuonyesha Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Mh Lazaro Nyalanmdu na Mbunge wa Vunjo Mh Mrema baadhi ya magari yaliyokamatwa yakiwa na bidhaa mbali mbali za magendo ikiwemo sukari.
Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Mh Lazaro Nyalandu akitoa maagizo kwa watendaji wa mamlaka mbali za serikali katika Mji mdogo wa Himo mara baada ya kukamilisha ziara yake ya kutembelea na kukagua masoko na vituo vya Biashara mipakani katika Mkoa wa Kilimanjaro.
----


Kiasi hicho kikubwa cha sukari kimekamatwa katika maeneo mbali mbali ya mpaka wa Tanzania na Kenya na kuhifadhiwa katika ghala la polisi kituo cha Himo, ikiwa ni mwendelezo utekelezaji wa agizo la Waziri Mkuu Mh Mizengo Pinda aliezitaka Mamlaka zote za ulinzi na Usalama nchini kuhakikisha kuwa, bidhaa hiyo haivuki mipaka ya ili kukabiliana na uhaba mkubwa wa bidhaa hiyo hapa nchini.

Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Mh Lazaro Nyalandu akiwa katika ziara ya kutembelea masoko na vituo vya biashara mipakani, amefika katika eneo la Himo na kushuhudia kiasi hicho kikubwa cha sukari huku Mbunge wa Jimbo la Vunjo Mh Augustino Lyatonga Mrema akiiomba serikali kutoa agizo la kuzitaka Mamlaka husika kuwauzia wananchi bidhaa hiyo mara moja bila kusubiri taratibu zinazotumia muda mrefu huku wananchi wakiendelea kuteseka kwa kukosa bidhaa hiyo muhimu.



Kwa upande wake Mbunge wa Vunjo Mh Augustino Mrema amesema, uhaba wa sukari nchini unatokana na bei nzuri ya bidhaa hiyo katika nchi za jirani hali inayowavutia wafanyabiashara wenye tamaa kupeleka bidhaa hiyo katika nchi za Kenya na Uganda.
“ Sukari ya Tanzania inauzwa nchini Kenya kwa bei mara mbili zaidi ya hapa nchini. Miji yetu ya mipakani ina njia za panya lukuki huku vyombo vyetu vya ulinzi na usala vikiwa na watendaji wachachache na vitendea kazi duni. Ninaiomba serikali kuzipa uwezo mamlaka zake ili ziweze kufanya kazi kwa ufanisi, ninaomba pia sukari ilioyokamatwa iuzwe mara moja kwa wananchi na askari au raia walifanikisha kukamatwa kwa bidhaa hizi wapewe motisha ya asilimia kumi ya kile walichokamata. Tukifanya hivi, biashara zote za magendo mipakani zitakoma.”

Naye Mkuu wa Wilaya ya Moshi Mussa Samizi aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, ameahidi kuongeza nguvu katika operesheni hiyo na kuwaomba wananchi kuvisaidia vyombo vya dola katika zoezi hilo kwa kutoa taarifa sahihi mara wanapoona vitendo hivyo vya kuvusha sukari na bidhaa nyingine hasa kastika njia za panya ambazo haziwezi kufikiwa na vyombo vya dola kwa urahisi.
Katika hatua nyingine, Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Mh Lazaro Nyalandu, amewata Watanzania kushindana kikamilifu na majirani zetu katika kutumia vyema fursa za kibiashara zilizoko katika maeneo ya mipaka ya nchi yetu na nchi jirani.

Akizungumza na Viongozi na watendaji mbali mbali wa serikali wa Mkoa wa Kilimanjaro, Mh Nyalandu amesema hadi sasa, ni watanzania wachache sana wanaofanya biashara zenye tija katika masoko na vituo vya biashara mipakani.

“Masoko yetu yamejaa bidhaa za wageni kwa zaidi ya asilimia 70 huku sisi tukiambulia asilimia 30 na bidhaa zetu tunazowauzia nyingi ni bidhaa ghafi, baada ya muda mfupi wenzetu wanaziongeza thamani na kutuuzia tena kwa bei ya juu. Lazima tuchukue hatua, tufanye kama wao, tuwapelekee bidhaa mpaka nchini mwao, tujenge masoko na mifumo thabiti itakayowavutia kuja nchini na kufanya biashara ki halali, nchi ipate kodi, wao wafaidike na sisi tufaidike pia.”

Ziara ya Mh Nyalandu kutembelea masoko na vituo vya biashara mipakani ilianzia katika Mpaka wa Tanzania na Kenya katika Mji wa Namanga ikiwa na lengo la kutembelea maeneo hayo kote nchini. Baada ya kutembelea vituo vya Himo na Holili, msafara wa Naibu Waziri utatembelea kituo cha Horohoro Mkoani Tanga kabla ya kuhamia kanda ya Ziwa.

Ziara ya ghafla ya Viongozi hao ilivutia umati mkubwa wa wananchi na wafanyabiashara wa maeneo ya Himo na Holili hali iliyolawalazimu viongozi hao kuzungumza na wananchi. Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Mh Lazaro Nyalandu, akalipongeza Jeshi la Polisi na Mamlaka za Usalama katika Miji ya Mpakani ya Himo na Holili kwa jitihada kubwa ya kupambana na biashara za magendo katika eneo hilo.

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Uganda Police issue fresh terror alert

  By Chris Kiwawulo, The Police have issued a fresh terror alert against a possible attack on Uganda by four terrorists from Kazakhstan. Police spokesperson Judith Nabakooba “We have received a security notification in form of an orange notice of four terrorists originating from Kazakhstan who are planning to travel to foreign countries in order to commit attacks and participate in hostile acts,” Police spokesperson Judith Nabakooba said in a statement on Monday. Nabakooba named the four active members of radical organizations as; Nassiruauly Kairat, Umurzakov Marat Eskendirovich, Kovtun Denis Valerevich and Mazhibayen Alimzhan Akhlazhanovich. By press time, a search on the international web has not yielded anything on the named persons.Last evening, police said that in collaboration with other security agencies vigilance has been stepped up to avert the terrorists’ evil plans. Police have in the past issu...

Poland’s GROM special services mastermind found dead

Brigadier General Slawomir Petelicki, responsible for the formation of the GROM special services unit in the 1990s, was found dead at his apartment, Saturday, with bullet wounds to the head. Sławomir Petelicki, 1946-2012. Photo: Archive/PAP/Radek Pietruszka Police spokesman Maciej Karczynski informed that Petelicki’s body was found by his wife in the garage of his Warsaw apartment on Saturday. He was 65. Primary investigations point to suicide as the cause of death. It is expected that prosecutors will decide on an investigation into Petelicki’s death on Monday. After examining the scene of the incident, “the body of General [Petelicki] has been taken to a forensic laboratory, although a post-mortem will probably take place on Monday,” prosecutor Katarzyna Calow-Jaszewska from the Warsaw District Prosecution told the PAP news agency. “He was a tough man, a brilliant soldier and commander,” Colonel Krzysztof Przepiorka, head of the ...