Skip to main content

Mabasi manne ya Wakenya yatua Samunge


Send to a friend
Tuesday, 12 April 2011 22:17

Mussa Juma, Loliondo

WAGENI kutoka nchi jirani ya Kenya wakiwa ndani ya mabasi madogo manne, jana walitinga katika Kijijini Samunge kupata kikombe cha dawa kwa Mchungaji Mstaafu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri(KKKT), Ambilikile Mwasapila.

Wakenya walianza kuingia kwa wingi kijijini Samunge kuanzia alfajiri na kunywa kikombe dawa inayotolewa na Mwasapila. Sambamba na Wakenya hao, Watanzania wenye asili ya kiasia zaidi ya 30 pia walifika kijijini hapo na walipata kikombe Samunge baada ya kutua na ndege nne za kukodi jana asubuhi.

Mkutano wa kijiji leo Samunge
Mkutano huo wa kijiji cha Samunge unatarajiwa kufanyika leo wenye ajenda kuu ya mgogoro wa mapato ya ushuru wa magari na helkopta zinazofika huko wakati huu.

Mwenyekiti wa Kijiji cha Samunge, Michael Lengume, alisema wananchi wataombwa na Halmashauri ya Kijiji kutoa idhini ya kuanza kukusanya mapato ya Sh2,000 kwa siku kwa kila gari na ndege Sh150,000.

Awali, kijiji hicho kilikuwa kikikusanya ushuru huo, lakini baadaye kutokana na maagizo toka Waziri wa Nchi ofisi ya Waziri Mkuu (Sera), William Lukuvi, kazi ya kukusanya ushuru iliagizwa kufanywa na halmashauri na gharama zilipanda hadi Sh5,000.

Katika gharama hizo, halmashauri itachukuwa Sh2,000 na ofisi za wakuu wa mikoa Sh3,000 kwa kila gari ambapo gharama za helkopta kutua Samunge ni Sh150,000. Diwani wa Kata ya Samunge, Jackon Sandea, alisema jana kuwa wataanza kukusanya ushuru huo kesho kwa kuwa ni haki yao.

"Mbona vijiji vingine vinakusanya fedha zao bila shida. Kwa mfano, wageni wanaopanda Mlima Oldonyolengai kijiji kinakusanya fedha, watu waliowekeza vijiji vya Loliondo wanapokea fedha zao, sasa kwa nini wanatuingilia sisi," alihoji Sandea.

Alisema fedha za ushuru wa magari ni haki yao, kwani zinasaidia huduma za usafi, ujenzi wa vyoo, masuala ya afya na ulinzi kwa wanaofika Samunge.

Uwanja wa ndege Wasso wazidiwa uwezo
Uwanja mdogo wa ndege wa Wasso uliopo Loliondo Wilaya ya Ngorongoro, umezidiwa uwezo kutokana na idadi kubwa ya ndege zinazotua kwa siku kupeleka wagonjwa kijiji cha Samunge.

Wakizungumza na Mwananchi jana katika uwanja huo, Msimamizi wa Uwanja, Gabriel Masare na Afisa Uendeshaji wa Uwanja wa Ndege wa Arusha, Fredrick Kimaro, walisema ongezeko la ndege zinazotua hapo ni zaidi ya asilimia 75 ya awali.

Masare alisema, awali kabla ya tiba ya Samunge, uwanja huo ulikuwa ukipokea wastani wa ndege moja kwa wiki, lakini sasa ndege kati ya tatu na sita zinatua kila siku.

Alisema kutokana na ongezeko hilo, changamoto kadhaa zimeibuka ambazo ni uwanja huo kukosa huduma nyingi muhimu ikiwepo maji, umeme na eneo la kupumzika wasafiri viti na chakula.

Kimaro alisema, kwa sasa uwanja huo unapaswa kuwa na umeme kwani baadhi ya ndege hulala hapo.

safari za ndege zaanza Samunge
Kutokana na idadi kubwa wa wasafiri, makampuni ya ndege ya Coastal Air, Air Excel na ndege ya binafsi ya Babu Sembeke wa Moshi yamenzisha usafiri wa kwenda Samunge.

Kwa mujibu wa Kimaro, wastani wa gharama za ndege yenye uwezo wa kubeba watu sita kwenda na kurudi Samunge kwa jumla ya Dola za Marekani2,400.

"Kumekuwepo mazungumzo ya kuanzisha safari za ndege kila siku au kwa wiki nadhani muda si mrefu wataanza kwani sasa wanakodiwa na watu kuja hapa,"alisema Kimaro

Usafiri wa Helkopta nao washika kasi
Usafiri wa helkopta za kukodi toka Jijini, Arusha, mjini Moshi na Jijini Dar es Salaam umeshamiri Samunge kwa sasa.

Mwenyekiti wa kijiji cha Samunge, Michael Lengume alisema wastani wa helkopta nne zinatua kwa siku Samunge na wagonjwa mbali mbali. Habari hii imeandikwa katika gazeti la Mwananchi.

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.